Alama Online Tv

  • Home
  • Alama Online Tv

Alama Online Tv Hapa Ni sehemu ya Habari , Sanaa na Utamaduni

29/10/2022

Maonesho ya Kimataifa ya Utalii Karibu Kusini

TUKUTANE
Cc

HALF TIME:   🇹🇿🏟️ Benjamin MkapaYANGA SC 1-1 SIMBA SC⚽ Aziz Ki 45'⚽ Okrah 15'Dakika 45 za kipindi cha kwanza zimemalizik...
23/10/2022

HALF TIME: 🇹🇿

🏟️ Benjamin Mkapa

YANGA SC 1-1 SIMBA SC
⚽ Aziz Ki 45'
⚽ Okrah 15'

Dakika 45 za kipindi cha kwanza zimemalizika katika dimba la Benjamin Mkapa, Hakuna mbabe.

Ni katika derby ya kwanza ya msimu ya Kariakoo kwenye Ligi kuu ya kandanda Tanzania bara.

Timu ya Taifa ya Wanawake Serengeti Girls imetinga hatua ya robo fainali ya kombe la Dunia la Wanawake chini ya miaka 17...
18/10/2022

Timu ya Taifa ya Wanawake Serengeti Girls imetinga hatua ya robo fainali ya kombe la Dunia la Wanawake chini ya miaka 17 kufuatia sare ya 1-1 dhidi ya Canada na kumaliza katika nafasi ya pili kwenye kundi D ikiwa na alama 4.

Serengeti Girls iliibamiza Ufaransa 2-1 katika mchezo wa pili kufuatia kipigo cha 4-0 dhidi ya kinara Japan mwenye alama 9.

KUNDI D
🇨🇵 Ufaransa 0-2 Japan 🇯🇵
🇹🇿 Tanzania 1-1 Canadá 🇨🇦

Msimamo
🇯🇵 J*P 9
🇹🇿 TAN 4
🇨🇦 CAN 2
🇨🇵 FRA 1

ALEXIA WAMOTO 🔥🔥 BALLON D'OR 2022Nyota wa timu ya Wanawake ya Barcelona  , Alexia Putellas ameshinda tuzo ya Ballon d'or...
17/10/2022

ALEXIA WAMOTO 🔥🔥 BALLON D'OR 2022

Nyota wa timu ya Wanawake ya Barcelona , Alexia Putellas ameshinda tuzo ya Ballon d'or 2022 kwa Wanawake.

Mshambuliaji wa klabu ya Fc Barcelona Robert Lewandowski 🇵🇱 ameshinda tuzo ya Gerd Muller ya mwaka 2022. Tuzo hii hutole...
17/10/2022

Mshambuliaji wa klabu ya Fc Barcelona Robert Lewandowski 🇵🇱 ameshinda tuzo ya Gerd Muller ya mwaka 2022. Tuzo hii hutolewa kwa mshambuliaji bora aliyefunga mabao mengi ndani ya msimu mmoja. 🏟 Mechi: 56 ⚽ Mabao: 57 Goal Machine

MSHINDI WA PILI BALLON D'ORMshambuliaji wa Senegal, Sadio Mane ameshika nafasi ya pili katika viwango vya tuzo ya Ballon...
17/10/2022

MSHINDI WA PILI BALLON D'OR

Mshambuliaji wa Senegal, Sadio Mane ameshika nafasi ya pili katika viwango vya tuzo ya Ballon d'or 2022 nyuma ya kinara Karim Benzema.

Mane anakuwa Mwafrika wa kwanza kuwa kwenye viwango vya juu zaidi vya Ballon d'or tangu George Weah.

BENZAMA D'or 2022Mshambuliaji wa Real Madrid na timu ya Taifa Ufaransa, Karim Benzema ameshinda tuzo ya Ballon d'or 2022...
17/10/2022

BENZAMA D'or 2022

Mshambuliaji wa Real Madrid na timu ya Taifa Ufaransa, Karim Benzema ameshinda tuzo ya Ballon d'or 2022.

JIJI LAJIPANGA KUPAMBANA NA UDUMAVU PAMOJA NA UTAPIAMULO MKALINa. Josephina Kayugwa, DODOMAMGANGA Mkuu wa Halmashauri ya...
17/10/2022

JIJI LAJIPANGA KUPAMBANA NA UDUMAVU PAMOJA NA UTAPIAMULO MKALI
Na. Josephina Kayugwa, DODOMA
MGANGA Mkuu wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dkt. Andrew Method, amewataka Maafisa Lishe kushirikiana na viongozi wa Kata pamoja na Mitaa kuendelea kutoa elimu kwa wamama wajawazito pamoja na wananchi wote kujua umuhimu wa kuwahi kliniki kwaajili ya kujua maendeleo ya kiafya pamoja na kutumia vyakula vyenye lishe ili kuondoa udumavu na utapiamulo mkali.

Dkt. Andrew ameyasema hayo katika kikao cha tathimini ya mkataba wa lishe ngazi ya Kata robo ya kwanza Julai – Septemba 2022/2023 kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Alisema kuwa suala la lishe bora ni jambo la muhimu ambalo kila mwananchi anatakiwa kulijua kwasababu wajawazito wengi wamekuwa hawahudhurii hospitali lakini pia wengi wao hawatumii vyakula vya lishe kitu ambacho kinawaletea matatizo wakati wa kujifungua.

“Kinamama wote wanatakiwa wapatiwe elimu ya kutosha juu ya umuhimu wa lishe pamoja na kwenda kliniki wakati wote wa ujauzito ili kuondokana na haya matatizo, maana wajawazito wamekuwa wakipoteza damu nyingi au kupoteza maisha wakati wa kujifungua.

Inatakiwa k**a wataalamu wa afya tuhakikishe jambo hili la kutoa elimu katika Kata na Mitaa yetu linafanikiwa kwa kiasi kikubwa maana hata k**a mama atajifungua salama k**a hatumii lishe basi mtoto atakuwa na utapiamulo mkali pamoja na udumavu,” alisema Method.

Kwa upande wake Afisa Lishe Jiji la Dodoma, Semeni Juma, alisema katika kupambana na tatizo la utapiamulo jijini la Dodoma linakwisha, uongozi wa Kata na mitaa kwa kushirikiana na wahudumu wa ngazi ya jamii wanatakiwa kuendelea kufanya ufuatiliaji wa watoto walioibuliwa wenye utapiamulo mkali kwenye mitaa na kuhakikisha siku ya afya na lishe inafanyika kwa kila mtaa.

“tunatakiwa kuondoa tatizo la utapiamulo mkali kwa watoto wetu kwa kuhakikisha watendaji wanasimamia vyema uwepo wa program za uzalishaji wa chakula kwa wanafunzi katika shule zote za msingi na sekondari zilizopo kwenye kata.

Pia, katika vituo vyote vya afya kuwepo namba za watendaji wa Kata ili kupata taarifa za watoto wenye utapiamulo, hii itasaidia kujua jinsi gani ya kutatua tatizo hi

SERENGETI GIRLS WAIPA KICHAPO K**A NGOMA UFARANSATimu ya taifa ya Wasichana ya umri chini ya miaka 17 Serengeti Girls im...
15/10/2022

SERENGETI GIRLS WAIPA KICHAPO K**A NGOMA UFARANSA

Timu ya taifa ya Wasichana ya umri chini ya miaka 17 Serengeti Girls imeibamiza Ufaransa U17 bao 2-1 ikiwa ni ushindi wa kwanza kwenye michuano ya kombe la Dunia ya Wasichana

FT: Ufaransa 1-2 Tanzania
⚽ Diana Mnally
⚽ Christer Bahera

Na Josephina Kayugwa, DODOMA.MKUU wa Wilaya ya Dodoma Jabir Shekimweri ametoa wito kwa wakazi  wa Jiji la Dodoma kuwatak...
15/10/2022

Na Josephina Kayugwa, DODOMA.
MKUU wa Wilaya ya Dodoma Jabir Shekimweri ametoa wito kwa wakazi wa Jiji la Dodoma kuwataka kufuata sheria za kunawa mikono ili kujikinga na magonjwa ya mripuko k**a vile kipindupindu, mfumo wa hewa na macho, sheria hizo ni k**a vile kutumia maji safi na salama yanayotiririka, sabuni, kusugua mikono kwa sekunde 15 pamoja kujifuta kwa kutumia kitambaa safi
Ametoa wito huo katika maadhimisho ya siku ya kunawa mikono duniani ambapo katika wilaya ya Dodoma yamefanyika leo tarehe 15 Oktoba, 2022 katika kata ya Mtumba yakiongozwa na kauli mbiu inayosena “Tuungane pamoja kuhakikisha usafi wa mikono kwa wote”
Alisema katika kuzuia magonjwa ya mripuko kila mtu anatakiwa kunawa mikono bila kusahau kufuata utaratibu na sheria zote ambazo zinahitajika kwasababu wengi wamekuwa hawafuati, hivyo hata wakinawa bado vimelea vya magonjwa vinakuwepo katika mikono yao.
“kila mtu antakakiwa kumlinda mwenzake dhidi ya magonjwa ya mripuko kwasababu gonjwa likimpata mmojabasi kila mtu itamathiri maana magonjwa haya ya mripuko huambukiza mtu mmoja baada ya mwingine na husambaa kwa haraka.
“Lakini pia katika vituo vya afya pamoja na sehemu ambayo zinafanya watu wakusanyike basi sehemu hizo Maafisa afya wahakikishe vifaa vya kunawia mikono vinakuwepo mda wote ili viwasaidie watu kutekeleza jambo hili na naamini tutakuwa salama sote,” alisema Shekimweri.
Kwa upande wake Jacobo Ezekieli Mkazi wa kata ya Mtumba alisema wananchi wafanye zoezi hili kwa amani kwa kushirikiana na vingozi wote wa kata bila kusahau kuelimisha ili kila mtu awe na elimu juu ya kunawa mikono.
“Sisi k**a wananchi tunatakiwa kuwa pamoja na viongozi wetu ili tufanikishe jambo hili kwasababu magonjwa ya mripuko ni hatari kwa afya zetu, lakini pia kila mmoja wetu ana wajibu wa kumwambia ukweli mwenzake ili tulindane k**a jamii dhidi ya magojwa hatarishi,” alisema Ezekiel.
Aidha aliwaomba viongozi wa Dini kuendelea kuwahamasisha waumini wakiwa katika sehemu zao za ibada kuzingatia jambo la kunawa mikono kwa kufuata sheria hata wakiwa majumbani kwao.

15/10/2022

CHANGARAWE WAMUENZI WALIMU KWA VITENDO, "ALIKUWA MZALENDO, MCHAPAKAZI"

AFISA Elimu Sekondari Halmashauri ya Mji wa Mafinga Ndg. Steven Semdoe ameungana na Mwalimu Mkuu Peter Mbata pamoja na wanafunzi wa Shule ya Sekondari Changarawe kufanya usafi katika maeneo ya Hospital ya Mji Mafinga ikiwa ni kumbukizi ya Miaka 23 ya kifo Cha Baba wa taifa Mwl. Julius Kambarage Nyerere mapema Leo tar 14/10/2022.

Cc

14/10/2022

ULEMAVU SIO KUSHINDWA KUMUDU SHUGHULI ZA MAISHA

WANAFUNZI Ladiladius Massawe na Theofista Obeid wa shule ya sekondari Mtera wilayani Iringa ni walemavu wa kuona lakini licha ya changamoto hiyo wamefanikiwa katika masomo yao na wana ndoto kubwa hapo baadaye.

Wanafunzi hao wamewaomba watu wengine wenye ulemavu wa aina yoyote kutokubali kupoteza mwelekeo katika maisha kwa kukata tamaa huku wakiwakumbusha wazazi na walezi wa watoto wenye ulemavu kuwapenda watoto wao.

Cc Clement Sanga

14/10/2022

UMUHIMU WA KUZIHAMISHA KAYA 374 KUTUNZA VYANZO VYA MAJI

TUME ya Taifa ya Mipango ya Matumizi ya Ardhi kwa kushirikiana na Ofisi ya Makamu wa Rais imeishauri Serikali katika Halmashauri ya wilaya ya Iringa kuona umuhimu wa kuzihamisha kaya 374 zilizopo kwenye kingo za bwawa la Mtera ili kumaliza shughuli za kibinadamu zinazofanyika kwenye maeneo hayo ambazo ni tishio kwa ustawi wa bwawa hilo ambalo ni nyeti kwenye uzalishaji wa nishati ya umeme nchini.

Cc Clement Sanga

13/10/2022

AFISA USALAMA FEKI ANASWA NA POLISI

JESHI la Polisi mkoani Iringa linamshikilia mtu mmoja Gabriel Kaserikali (34) mkazi wa Mbezi Mwisho Jijini Dar Es Salaam kwa tuhuma za kujifanya mtumishi wa Idara ya Usalama wa Taifa ambaye siku ya tarehe 1/10/2022 alikuwa akipita kwa baadhi ya wajumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM wilaya ya Iringa na kuwaelekeza wajumbe wamchague mmoja wa wagombea aliyejulikana k**a Leonard Mgina ambaye alikuwa anagombea nafasi ya Mwenyekiti wa CCM wilaya hiyo.

Address


Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Alama Online Tv posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Videos

Shortcuts

  • Address
  • Telephone
  • Alerts
  • Videos
  • Claim ownership or report listing
  • Want your business to be the top-listed Media Company?

Share