Karibu katika hafla ya Funga mwaka tarehe 21 Disemba 2024 pale viwanja vya CCM Kalangalala Geita Mjini
Baadhi ya wakazi wa Mji wa Geita wametoa maoni yao kuhusu mbinu mbalimbali wanazotumia watia nia wa nafasi za uongozi kuelekea uchaguzi Mkuu wa mwakani 2025.
Kijana amezaliwa, Tafadhali mpeni keki yake
WAKAZI WA MTAA WA KATOMA, WASTAAFU NA VIJANA WAKITOA MAONI YAO KUHUSU RUSHWA KWENYE UCHAGUZI
Taasisi ya Kuzuia na kupambana na rushwa Mkoa wa Geita katika taarifa yake Kwa waandishi wa Habari imesema katika kipindi Cha Januari hadi Machi, 2024 jumla ya kesi 20 ziliendelea katika Mahakama mbalimbali za Mkoa wa Geita ambapo katika kesi hizo, zilizofunguliwa Mpya ni 3, zilizokuwa zinaendelea Mahakamani ni 17.
Kaimu Mkuu wa Taasisi hiyo Mkoa huo wa Geita, Azza E. Mtaita amesema katika kesi 17 zilizokuwa zinaendelea Mahakamani, zilizotolewa maamuzi ni 4 ambapo, 2 Jamhuri ilishinda, kesi 01 iliondolewa kwa kibali Cha mashtaka kukosewa na kesi 01 Jamhuri ilishindwa kuthibitisha pasipo kuacha shaka.
Pamoja na hayo TAKUKURU Geita katika kipindi hicho Cha Januari hadi Machi 2024, imefuatilia Utekelezaji wa miradi ya maendeleo 24 yenye thamani ya shilingi 27, 155,743,651.
#TakukuruTv