Rubondofm

Rubondofm District radio station
provide News content, sports, music and current affairs.

Waziri wa Habari na Utamaduni, Sanaa na Michezo Prof Palamagamba Kabudi ametoa wito kwa vyombo vya utangazaji kuwa na Ma...
13/02/2025

Waziri wa Habari na Utamaduni, Sanaa na Michezo Prof Palamagamba Kabudi ametoa wito kwa vyombo vya utangazaji kuwa na Matumizi fasaha ya Lugha ya Kiswahili ili kusaidia kukua kwake.

Mhe Waziri ameyasema hayo Alhamis Februari 13, 2025 kwenye ukumbi wa New Generation Jijini Dodoma ambapo mkutano wa mwaka wa vyombo vya utangazaji unafanyika.

Amewataka Waandishi wa Habari kuandaa vipindi kwa kuzingatia ueledi na ufasaha wa matamshi yanayozingatia matumizi sahihi ya lugha yatakayochochea maendeleo kwa jamii


Ripoti ya Kampeni ya Msaada wa kisheria ya Mama Samia MSLAC,imekabidhiwa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Geita Februari 4, 20...
06/02/2025

Ripoti ya Kampeni ya Msaada wa kisheria ya Mama Samia MSLAC,imekabidhiwa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Geita Februari 4, 2025.

Ripoti hiyo imepokelewa na Katibu Tawala Wilaya ya Geita Bi Lucy Beda kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya Hashim Komba.

Mratibu wa kampeni hiyo Scholastica Mality pamoja na mambo mengine amesema kampeni imefika katika kata 10 na vijiji 31 badala ya 30 vilivyopangwa na kubaini kero na malalamiko mbalimbali yanayotakiwa kutatuliwa na viongozi wa ngazi ya Halmashauri na Wilaya.

Kwa upande wake Katibu tawala Bi Lucy amepongeza timu hiyo kwa kazi nzuri na kwamba kero zilizoibuliwa zitafanyiwa kazi.

Pia amemshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuandaa kampeni hiyo ambayo imetatua kero za wananchi hasa wa maeneo ya pembezoni.

Timu iliyokuwa ikitekeleza Kampeni ya Msaada wa Kisheria ijulikanayo k**a Mama Samia Legal Aid Compaign leo Februari 4,2...
04/02/2025

Timu iliyokuwa ikitekeleza Kampeni ya Msaada wa Kisheria ijulikanayo k**a Mama Samia Legal Aid Compaign leo Februari 4,2025 imekabidhi repoti yake ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Geita.

Kiongozi wa Timu hiyo kutoka Wizara ya Katiba na Sheria Bi Scolastica Mality amesema timu hiyo imefanikiwa kwa asilimia 100 kwa kuzifikia kata 10 na vijiji 31 badala ya 30 vilivyopangwa

Kata zilizofikiwa ni Lwamgasa, Katoro, Ludete, Magenge, Kakubilo, Nyawilimilwa, Nkome, Bugulula, Isulwabutundwe na Nyarugusu ambapo jumla ya wananchi 30,954 wamefikiwa katika Kampeni hiyo na zaidi ya migogoro 81 imesikilizwa huku migogoro 10 ikitatuliwa hapo hapo.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Geita Dkt Modest Burchad ameishukuru timu hiyo kwa kazi waliyoifanya na kusema Halmashauri itaendelea kutoa ushirikiano kila wakati.

Timu hiyo ilianza utekelezaji wa Kampeni ya Msaada wa Kisheria Januari 26,2025 na kuhitimisha Februari 4,2025.

Wimbo wa don't touch umerindima katika shule za Msingi na Sekondari katika kampeni ya Msaada wa kisheria ya Mama Samia.W...
01/02/2025

Wimbo wa don't touch umerindima katika shule za Msingi na Sekondari katika kampeni ya Msaada wa kisheria ya Mama Samia.

Wimbo huo ambao unamuelimisha mwanafunzi na mtoto chini ya umri wa Miaka 18 kutokuguswa na mtu yeyote kwenye sehemu nyeti za mwili wake ikiwemo matiti, makalio na sehemu za siri umeshika hatamu katika kampeni hii ili kuwajengea uelewa wanafunzi kukataa aina hiyo ya ukatili.

Katika shule ya Msingi Nyamalele kata ya Nkome, Afisa Dawati la usaidizi wa kisheria Halmashauri ya Wilaya ya Geita Rachel Malimi amewaongoza wanafunzi hao kuimba wimbo huo.

Wakazi wa kata ya nkome wametakiwa kuacha kuelewana na kufifisha jitihada za kukabiliana na vitendo vya Ukatili wa Kijin...
01/02/2025

Wakazi wa kata ya nkome wametakiwa kuacha kuelewana na kufifisha jitihada za kukabiliana na vitendo vya Ukatili wa Kijinsia.

Wito huo umetolewa Januari 31,2025 na WP 8313 CPL Salome Michael Aswile kwenye mkutano wa hadhara wa Kampeni ya Msaada wa kisheria ya Mama Samia MSLAC.

Amesema baadhi ya wananchi wakikubaliana na watu wanaotenda Ukatili bila kujua athari zake.

Katika Ukatili mwingine ni baadhi ya wanawake kuwanyima tendo la ndoa waenzi wao na kwamba kufanya hivyo ni Ukatili wa Kijinsia, hivyo amewataka wanaume wanaofanyiwa hivyo kuripoti matukio hayo kwenye dawati la jinsia ili wasaidiwe.

Imeelezwa kuwa migogoro mingi hutokea kwenye familia baada ya Mwaume kufariki Dunia na kumuacha mjane kutokana wanaukoo ...
01/02/2025

Imeelezwa kuwa migogoro mingi hutokea kwenye familia baada ya Mwaume kufariki Dunia na kumuacha mjane kutokana wanaukoo kukaa kugawa Mali zote hadi ambazo hatikiwi kugawa.

Hayo yamesemwa na Kiongozi wa Kampeni ya Msaada wa kisheria ya Mama Samia MSLAC, Halmashauri ya Wilaya ya Geita Scholastica Bality wakati akizungumza na wananchi wa Kata ya Nkome.

Amesema katika kazi yao ya Huduma ya Msaada wa kisheria, wamekutana na malalamiko mengi ya namna hiyo na kwamba ni vema kuzingatia taratibu za kisheria katika kugawa mirathi.
pia amewasisitiza wananchi hao kuandika Wosia ili kupunguza au kumaliza kabisa changamoto hizo ambazo huleta madhara makubwa kwenye jamii.

viwanja 400 vimetambuliwa, na baadhi vimeandaliwa hatimiliki katika kata ya Nkome Halmashauri ya Wilaya ya Geita.Hayo ya...
01/02/2025

viwanja 400 vimetambuliwa, na baadhi vimeandaliwa hatimiliki katika kata ya Nkome Halmashauri ya Wilaya ya Geita.

Hayo yamesemwa na Judith Karia Afisa Ardhi Halmashauri ya Wilaya ya Geita, ambapo amewataka wananchi kulipia urasimishaji unaoendelea.

Amesema Wananchi wanachangia fedha hiyo ili iweze kusaidia kuandalia vigingi vitakavyotumika kubaini mipaka ya eneo la mwananchi husika

Amesema mtu akitaka kumuuzia mwingine kiwanja kilicho rasimishwa ni vizuri afike kwanza ofisi za Ardhi ili mtaalamu akapime kujiridhisha kwamba kiwanja hicho hakina mwingiliano wa zaidi ya mtu mmoja kwenye kiwanja kimoja.

"hivyo ukitaka Kununua kiwanja na kuuza kiwanja nkome ni vema kuwasiliana na ofisi ya aridhi ili kuondoa ujenzi holela" alisema Karia.

Kwa upande wa ujenzi amesema vema kutafuta vibali vya ujenzi kabla ya kujenga.

amesema gharama za ujenzi ni shilingi elfu 25, ambayo haitaathiri bajeti ya mtu anaetaka kujenga.

Elimu ya Msaada wa kisheria ya Mama Samia MSLAC imewafikia wanafunzi wa shule ya Sekondari Kakubilo ambapo wameelimishwa...
31/01/2025

Elimu ya Msaada wa kisheria ya Mama Samia MSLAC imewafikia wanafunzi wa shule ya Sekondari Kakubilo ambapo wameelimishwa juu ya Ukatili wa Kijinsia, Haki za Binadamu na Ukatili wa Kijinsia.

Baadhi ya wanaume wanaofanya ukatili wa Kijinsia Kwa wake zao wametakiwa kubadili tabia na kuanza kuenenda kwa kuzingati...
31/01/2025

Baadhi ya wanaume wanaofanya ukatili wa Kijinsia Kwa wake zao wametakiwa kubadili tabia na kuanza kuenenda kwa kuzingatia Sheria za nchi.

Akitoa elimu kwa Wananchi wa Kabayole WP 8313 CPL Salome Michael Aswile, Afisa Dawati la Jinsia na Watoto amesema baadhi ya wanaume wanawazuia wake zao kufanya kazi licha ya kuwa mwanamke na uwezo wa kufanya kazi.

Pia amewataka wanawake kuheshimu ndoa zao pindi wanapopata fursa ya kufanya kazi za uzalishaji mali ili kuendelea kudumisha maadili ya watanzania.

Kampeni ya Msaada wa kisheria ya Mama Samia MSLAC imeendelea kufungua fikra za wananchi ambapo suala la migogoro ya ardh...
31/01/2025

Kampeni ya Msaada wa kisheria ya Mama Samia MSLAC imeendelea kufungua fikra za wananchi ambapo suala la migogoro ya ardhi imefafanuliwa na kutakiwa kupima na kurasmisha maeneo yao.

Wito huo umetolewa na Afisa Ardhi Halmashauri ya Wilaya ya Geita, Judith Karia wakati akitoa elimu kwa wakazi wa Kabayole kata ya Kakubilo Januari 30, 2025.

27/01/2025
Wananchi 779,191 wamefikiwa na kampeni ya  huduma ya Msaada wa kisheria ya Mama Samia (MSLAC) ambapo wanawake ni  zaidi ...
26/01/2025

Wananchi 779,191 wamefikiwa na kampeni ya huduma ya Msaada wa kisheria ya Mama Samia (MSLAC) ambapo wanawake ni zaidi ya 389,000 na wanaume wakiwa zaidi 396,000 na kuibua migogoro 9069.

Akizungumza kwenye uzinduzi wa kampeni hiyo Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhe. Ruben Shigella kwa niaba ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Dotto Biteko, amesema kampeni hiyo imetatua na kupata suluhu ya kudumu migogoro zaidi ya 1505.

Amesema takwimu hizo zinaenda kuongezeka baada ya kampeni hiyo kuanza katika Mkoa wa Geita na kuwataka wananchi kujitokeza kwa wingi ili mambo hayo (migogoro) yaweze kutatuliwa.

Amesema Mkoa wa Geita k**a ilivyo Mikoa mingine inakabiliwa pia na migogoro ya ardhi, madini, mirathi ambapo baadhi ya Ndugu wanaungana wanadhulumu Mali za watoto na wajane.

Amewaomba watakaojitokeza kwenda kupata msaada wa kisheria unaosimamiwa na kufadhiliwa na Dkt Samia Suluhu Hassan, yale mambo yatakayobainika na kupelekwa mahak**ani waende wakatoe ushahidi.


Wakazi wa Mkoa wa Geita wametakiwa kujitokeza kwa wingi  kwenye Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia (MSLAC), uta...
24/01/2025

Wakazi wa Mkoa wa Geita wametakiwa kujitokeza kwa wingi kwenye Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia (MSLAC), utakaozinduliwa katika Viwanja vya CCM Kalangalala Januari 26, 2025.

Kampeni hiyo ya huduma ya msaada wa Kisheria ya mama Samia (MSLAC) unaratibiwa na Wazara ya Katiba na Sheria na utafanyika kwa kipindi cha siku tisa kwenye Mkoa wa mzima wa Geita kwa kuwafikia wananchi wa chini katika Kata kumi za kila Halmashari.

Huduma za kisheri zitakazotolewa kwa wananchi ni kupokea, kusikiliza, kusuluhisha na kutoa elimu kuhusu migogoro ya Ardhi,Haki za Binadamu, Utawala bora, mirathi, Ndoa, Ukatili wa Kijinsia, Madai, Jinai pamoja na Usajili wa vyeti vya kuzaliwa na Kifo.

Akizungumza kwenye mafunzo kwa wataalamu watakaotoa huduma kwenye kampeni hiyo kutoka Halmashauri 6 za mkoa wa Geita, Katibu Tawala Mkoa Mohamed Gombati ametoa wito ya kuwafikia wananchi ambao wanapswa kupata huduma hizo na kwamba itasaidia kupunguza gharama na muda wa kuwafikia wananchi.

Amewasihi wataalamu wa Halmashauri kushirikiana na wale wa Wizara katika kutekeleza majukumu hayo ili kutimiza lengo la kukuza na kutimiza upatikanaji wa haki kwa wote kupitia msaada wakisheria nchini.

Naye, Candid Nasua Wikili wa Serikali Ofisi ya Wizara ya Katiba na Sheria amesema kampeni hiyo inatokana na sheria za huduma za msaada wa kisheria sura ya 21 ya mwaka 2017, na mahitaji makubwa ya wananchi kupata msaada wa huduma za kisheria kwasababu ya kukosa uwezo wa kumudu gharama za mawakili.


Baadhi ya wagonjwa katika Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Geita,  iliyopo kata  Nzera wamekuwa wakikabiliwa na cha...
17/01/2025

Baadhi ya wagonjwa katika Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Geita, iliyopo kata Nzera wamekuwa wakikabiliwa na changamoto ya kung'atwa na mbwa wakati wanapofika kupatiwa matibabu Hospitalini hapo.

Taarifa hiyo imetolewa na Mganga Mfawidhi wa Hospitali hiyo kwa k**ati ya siasa ya Chama Cha Mapinduzi CCM Wilaya ya Geita, ilipofanya ziara ya kukagua Utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

Amesema changamoto hiyo ilisababishwa na Hospitali kukosa uzio na kwamba wanyama mbalimbali walikuwa wakiingia Hospitalini hapo.

Pia kwasababu za kiusalama vitu vingi vilikuwa vikipotea Kwa kukosa uzio kwani mlinzi alikuwa haweza kuzunguka eneo lote la Hospitali ili kudhibiti Hali hiyo.

Kwasasa Uongozi Mzima wa Hospitali wanaishukuru Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kutoa fedha zilizowezesha ujenzi wa uzio ambo utakuwa mwarobaini wa changamoto zilizokuwepo.

Kamati ya Siasa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilayani Geita imempongeza Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Geita ...
13/01/2025

Kamati ya Siasa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilayani Geita imempongeza Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Geita kwa Usimamizi mzuri wa Fedha za Miradi ya Maendeleo.

Hayo yameelezwa katika Ziara ya Siku mbili Januari 9 na10, 2025 iliyofanywa na Kamati hiyo chini ya Mwenyekiti wake Komredi Barnabas Mapande katika jimbo la Busanda na Geita.

Mapande ameipongeza ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Geita kwa kusimamia vema fedha za miradi zinazoletwa na Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kamati hiyo ikiwa katika Hospitali ya Wilaya kata ya Nzera ambapo imetembelea ujenzi wa Uzio wa Ukuta wenye thamani ya Shilingi Milioni 225,000,000 imesema Uzio huo ni muhimu kwa Hospitali hiyo ili kuweka mazingira mazuri yenye utulivu na usalama kwa Watumishi na hata wagonjwa kutoka Sehemu mbalimbali wanaofika Kupata huduma katika hospital hiyo.

Mradi wa maji miji 28, mji wa Geita wenye thamani zaidi ya shilingi bilioni 120 umefikiwa kwenye hatua kubwa ya ulazaji ...
12/01/2025

Mradi wa maji miji 28, mji wa Geita wenye thamani zaidi ya shilingi bilioni 120 umefikiwa kwenye hatua kubwa ya ulazaji wa mabomba, ambapo baada ya takribani miezi mitatu mradi huo utafikia asilimia 60 ya ukamilishwaji.

Hayo yamezungumzwa na Mkurugenzi wa mamlaka ya maji na usafi wa mazingira Geita GEUWASA, Frank Changawa, baada ya k**ati ya siasa ya CCM Wilaya ya Geita ikiwa katika ziara ya kukagua utekelezaji wa ilani ya Chama hicho 2020-2025 kutembelea na kukagua mradi huo wa maji miji 28.

Changawa amesema mkataba wa mradi huo ulioanza april 11, 2023 ni miezi 32, ambapo kwa Sasa umefikiwa asilimia 40 ukiwa kwenye hatua ya ulazaji mabomba na baada ya miezi mitatu utafikia asilimia 50 au 60.

Akiongea kwa niaba ya k**ati ya siasa CCM Wilaya ya Geita kwenye mradi huo, mwenyekiti wa UWT Wilaya ya Geita Paulina Majogolo amesema mradi huo wa miji 28 utaenda Kumaliza changamoto ya ukatili wa kijinsia kwa wanawake.

HABARI na

Mradi wa miji 28, mji wa Geita wenye thamani zaidi ya shilingi bilioni 120 umefikiwa kwenye hatua kubwa ya ulazaji wa ma...
12/01/2025

Mradi wa miji 28, mji wa Geita wenye thamani zaidi ya shilingi bilioni 120 umefikiwa kwenye hatua kubwa ya ulazaji wa mabomba, ambapo baada ya takribani miezi mitatu mradi huo utafikia asilimia 60 ya ukamilishwaji.

Hayo yamezungumzwa na Mkurugenzi wa mamlaka ya maji na usafi wa mazingira Geita GEUWASA, Frank Changawa, baada ya k**ati ya siasa ya CCM Wilaya ya Geita ikiwa katika ziara ya kukagua utekelezaji wa ilani ya Chama hicho 2020-2025 kutembelea na kukagua mradi huo wa maji miji 28.

Changawa amesema mkataba wa mradi huo ulioanza april 11, 2023 ni miezi 32, ambapo kwa Sasa umefikiwa asilimia 40 ukiwa kwenye hatua ya ulazaji mabomba na baada ya miezi mitatu utafikia asilimia 50 au 60.

Akiongea kwa niaba ya k**ati ya siasa CCM Wilaya ya Geita kwenye mradi huo, mwenyekiti wa UWT Wilaya ya Geita Paulina Majogolo amesema mradi huo wa miji 28 utaenda Kumaliza changamoto ya ukatili wa kijinsia kwa wanawake.

HABARI na

Address

BOMANI
Geita
30101

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Rubondofm posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Rubondofm:

Videos

Share