Rubondofm

Rubondofm District radio station
provide News content, sports, music and current affairs.

05/01/2026

Halmashauri ya Wilaya ya Geita imetoa mikopo yenye thamani ya shilingi milioni 500 kwa vikundi maalum vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa mikopo ya asilimia 10 ya mapato ya ndani, kwa lengo la kuwawezesha kiuchumi na kuboresha maisha yao.

Hafla ya kukabidhi mikopo hiyo imefanyika katika viwanja vya Halmashauri ya Wilaya ya Geita, ikiongozwa na Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Geita, Bi. Janet Mobe.

Akizungumza katika hafla hiyo, Bi. Mobe amewataka wanavikundi waliopata mikopo hiyo kuitumia kwa malengo yaliyokusudiwa, kufanya kazi kwa bidii pamoja na kurejesha kwa wakati, ili kutoa fursa kwa vikundi vingine kunufaika na mikopo hiyo.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Kamati ya Uchumi, Halmashauri ya Wilaya ya Geita, Mheshimiwa Paschal Mapung’o, amewakumbusha wanavikundi umuhimu wa matumizi sahihi ya fedha hizo, akisisitiza kuwa mikopo hiyo ni chachu ya maendeleo endapo itatumika kwa uangalifu na nidhamu ya hali ya juu

Naye Mkuu wa Divisheni ya Maendeleo ya Jamii wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita, Bw. Jonas Kilave, ameeleza kuwa zaidi ya vikundi 200 viliomba mikopo hiyo, ambapo baadhi vilikidhi vigezo na kupata mikopo huku vingine vikishindwa kukidhi masharti na hivyo kutopata kwa awamu hii

Baadhi ya wanavikundi waliopata mikopo hiyo wameeleza kufurahishwa na hatua hiyo, wakiahidi kufanya kazi kwa bidii, kuendeleza miradi yao na kurejesha mikopo kwa wakati ili na vikundi vingine vipate nafasi ya kunufaika

01/01/2026

Kutokana na changamoto ya kiuchumi inayokabili baadhi ya familia na kusababishia watoto wao kukatisha masomo, Uongozi wa Shule ya Ave Maria imeamua kusomesha Wanafunzi 20 wanaotoka katika mazingira magumu Kwa mwaka huu 2026.

Hatua ambayo imepongezwa na Kaimu Afisa Elimu Manispaa ya Geita Mwalimu Nkwabi Lutubija wakati akiwa Mgeni rasmi katika hafla ya Ave Maria Gate together iliyofanyika Januari Mosi, 2026.

Katika kuunga mkono hatua hiyo ameahidi kutoka madaftari kwa watoto waliopata ufadhili huo, huku akisisitiza wazazi wa watoto hao kuwasimamia watoto hao ili watimize ndoto yao.

Mkurugenzi wa Shule ya Ave Maria Ndg Andrew Mathius Bahangaja, amesema uamuzi huo ni katika kusaidia watoto walio katika mazingira magumu na kupunguza mdondoko wa Wanafunzi unaosababishwa na changamoto mbalimbali ikiwemo uchumi, watoto kwenda kufanya kazi mgodini na kuamua kuacha masomo.

Amesema baada ya kutangaza mpango huo jumla ya watoto 78 walijitokeza lakini waliamua kuanza na watoto 20 pekee.

Ameongeza kuwa mpango huo ni endelevu na Kila mwaka watakuwa wakichukua watoto 12.

Baadhi ya wazazi Wamesema uamuzi wa shule hiyo itakuza mahusiano na jamii na pia wazazi waamke katika kusimama watoto kielimu kwakuwa Dunia ya Sasa ni elimu.

31/12/2025
30/12/2025

Muungano wa vikundi vilivyonufaika na mikopo ya asilimia 10 inayotolewa na Halmashauri ya Wilaya ya Geita Mkoa wa Geita vimepeleka furaha kwa watoto yatima na walio na mazingira Magumu katika kituo cha Albayaan Islamic kilichopo ndani ya Mamlaka ya Mji Mdogo wa Katoro.

Afisa Maendeleo ya jamii wa kata ya Katoro Lita Kelly Mwakaleja amesema vikundi hivyo vilivyotoa mikopo ni wanufaika wa mikopo ya Halmashauri ya Wilaya ya Geita na vipo ndani ya Mamlaka ya Mji Mdogo wa Katoro na ameiomba jamii kuiga mfano huo.

Nao baadhi ya wanavikundi walioungana wakitoka katika Mamlaka ya Mji Mdogo wa Katoro ambao ni David Ezekiel Kalemela kutoka Ludete na Zephania Hosea kutoka kikundi Cha Mashujaa Katoro wakizungumza kwa niaba ya wenzao wamesema wameguswa na kutoa misaada hiyo kwa watoto hao ili kuwapatia faraja kuelekea kumaliza na kuukaribisha Mwaka mpya.

Mkurugenzi wa kituo hicho Shekhe Abobakar Nyerere ameshukuru kwa msaada huo uliowafikia watoto zaidi ya 60.

Na

30/12/2025

MKUU WA WILAYA GEITA AKABIDHI WALIMU MADAWATI 677.


Katika jitihada za kutatua changamoto ya uhaba wa madawati katika shule mbalimbali za msingi, Halmashauri ya Wilaya ya Geita imeamua kutumia mapato yake ya ndani kugharamia ununuzi wa madawati hayo.

Akizungumza katika hafla ya kugawa madawati zaidi ya 600 kwa shule za Halmashauri hiyo, Mkuu wa Wilaya ya Geita, Hashim Komba, ameipongeza menejimenti ya Halmashauri na Baraza la Madiwani kwa uamuzi wao wa kutenga fedha za ndani kwa ajili ya kutatua changamoto hiyo inayowakumba wanafunzi na walimu.

Kwa upande wake, Kaimu Afisa Elimu Msingi wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita, Ibrahim Bunangoi, amesema wamepokea kwa mikono miwili maelekezo ya Mkuu wa Wilaya katika kuhakikisha suala la uhaba wa madawati linafanyiwa kazi.

Baadhi ya walimu waliopokea madawati hayo wamesema wanashukuru kwa msaada huo na kuipongeza Serikali kwa kuchukua hatua ya kutatua changamoto hiyo.

Halmashauri ya Wilaya ya Geita ina jumla ya shule za msingi 238, zenye wanafunzi 258,318.

Hata hivyo, madawati yaliyotolewa ni 677, ambayo yanaweza kutumika na wanafunzi 2,031.

Hii ina maana kuwa bado kuna upungufu mkubwa wa madawati katika shule nyingi za wilaya hiyo.

Hivyo, wadau wa elimu wanashauriwa kuendelea kushirikiana na Serikali ili kuondoa changamoto hiyo na kuhakikisha kuwa watoto wote wanapata fursa ya kujifunza katika mazingira bora.

Habari na

23/12/2025

Mbunge wa Jimbo la Katoro Mhandisi Kija Limbu Ntemi amewataka Wananchi wa Jimbo la Katoro kuendelea kudumisha amani kuelekea sikukuu ya Krismas na Mwaka mpya.

Pia ametuma salam za sikukuu ya Krismas Kwa wananchi huku akiwakumbusha Watanzania kumuombea Rais Samia Suluhu Hassan na viongozi wengine, ili waongoze nchi kwa Utulivu

23/12/2025

Maafisa ugani katika wilaya ya Nyang'hwale Mkoani Geita wametakiwa kuwafikia wakulima na kuwasaidia kufanya kilimo cha kisasa kwa kuwa wamewezeshwa na serikali kutekeleza majukumu yao.

Mkuu wa wilaya ya Nyang'hwale Grace Kingalame ametoa agizo hilo kwa maafisa ugani wakati wa hafla ya ugawaji wa madawati 50 yaliyotolewa na chama kikuu cha ushirika Mkoa wa Geita GCU katika kijiji cha Nyang'holongo kilichopo kata ya Nundu.

Kingalame amewaagiza maafisa ugani wilayani humo kwenda kuwatembelea wakulima katika maeneo yao ya kazi ili waweze kulima mazao kwa kilimo cha kisasa.

18/12/2025

Mkuu wa mkoa wa geita Martine Shigela, ameipongeza kampuni ya uchimbaji dhahabu Mkoa wa Geita GGML kwa ufanisi wake katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo ndani ya Halmashauri ya Manispaa ya Geita.Mheshimiwa shigela ametoa pongezi hizo kwenye Kikao cha kamati ya ushauri ya Mkoa , ambapo pamoja na mambo mengine amebainisha kuwa katika miradi 35 iliyokuwa na changamoto 32 imekamilika kwa ufanisi asilimia 100

18/12/2025
Habari picha na
18/12/2025

Habari picha na

Address

BOMANI
Geita
30101

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Rubondofm posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Rubondofm:

Share