Taimediatz

Taimediatz Habari za ukweli na uhakika ndani na nje ya Tanzania kwa wakati sahihi.

15/01/2026

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt.Samia Suluhu Hassan, ametoa pole kutokana na changamoto ya kuzimwa kwa mtandao siku na baada ya Uchaguzi Mkuu Oktoba 29, 2025.
β€œKwa Washirika wetu katika Jamii ya Kidiplomasia na wageni wanaoishi hapa nchini Tanzania, ninatoa pole ya dhati kutokana na hali ya kutokuwa na uhakika, usumbufu wa huduma, na kufungwa kwa mtandao wa intaneti. Nawaahidi kuwa tutakuwa makini kuhakikisha usalama wenu na kuzuia hali k**a hiyo kujirudia katika siku zijazo.”

Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema hayo katika hafla ya kufungua mwaka mpya 2026 pamoja na Mabalozi wanaowakilisha nchi zao nchini Tanzania, Wawakilishi wa Heshima, na Wakuu wa Mashirika ya Kimataifa leo Januari 15, 2026, Ikulu Chamwino.

✍🏿
πŸ¦…

15/01/2026

Waziri wa Uchukuzi, Prof. Makame Mbarawa amewataka wadau wote wanaosimamia ujenzi wa Kiwanja cha ndege cha Kimataifa cha Msalato kushirikiana ili ujenzi huo ukamilike ifikapo Mwezi Mei mwaka huu.

Akizungumza jijini Dodoma, Januari 14, 2026 wakati akikagua maendeleo ya ujenzi huo, Prof. Mbarawa amesema hatua ya ukamilishaji wa ujenzi (finishing), inahitaji umakini, kujali thamani ya fedha na ubora wa vifaa unaoendana na mahitaji.

β€œMameneja wa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS), Mamalaka ya Viwanja vya ndege (TAA), Mamlaka ya Usafiri wa Anga (TCAA) pamoja na Zimamoto na Uhamimiaji shirikianeni kikamilifu ili vifaa na mifumo ya uendeshaji isomane na kurahisisha utendaji wa kazi kiwanjani hapo”, amesisitiza Prof. Mbarawa.

Kwa upande wake, Meneja wa TANROADS mkoa wa Dodoma Eng. Zuhura Amani amesema wamejipanga kumsimamia kikamilifu mkandarasi anaejenga kiwanja hicho ili kikamilike kwa wakati.

✍🏿
πŸ¦…

15/01/2026

Mbunge wa Jimbo la Kigoma mjini ambaye pia ni msanii wa kizazi kipya, Baba Levo, amenzawadia mke wake gari mpya aina ya Range Rover.

✍🏿
πŸ¦…

15/01/2026

Wagombea Urais nchini Uganda wa chama tawala cha National Resistance Movement (NRM) Yoweri Museveni, mwenye umri wa miaka 81, pamoja na mpinzani wake mkubwa Bobi Wine wamepiga kura katika uchaguzi mkuu unaofanyika leo nchini humo uliogubikwa na changamoto mbalimbali.

Museveni amelalamika kuwepo kwa changamoto za kiufundi wakati wa upigaji kura kwa kutumia mashine za kielektroniki.

Kwa upande wake mgombea wa upinzani , Bobi Wine, ameelezea mazingira ya uchaguzi yamegubikwa na changamoto mbalimbali zikiwemo kuzimwa kwa huduma ya intaneti pamoja na hitiliafu za kiufundi za vifaa vya kupigia kura.

✍🏿
πŸ¦…

15/01/2026

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimesema katika miaka 33 tangu kusajiliwa kwake kimepitia majaribu mazito ya kuwapoteza mashujaa wao waliouawa kikatili.

Akiongea na Watanzania Leo Januari 15,2026 Naibu Katibu Mkuu wa Chama hicho , Amani Golugwa, amesema kutokana na majaribu waliyopitia ingekuwa chama kingine kingeshasambaratia.
β€œSafari ya miaka 33 ya machozi, jasho na damu. Katika safari hii Chadema imepitia majaribu mazito ambayo chama kingine chochote kingeshasambaratika. Tumelipa gharama kubwa ya mapambano ya kidemokrasia. Tumepoteza mashujaa wetu, wengi waliouawa kikatili.”

✍🏿
πŸ¦…

15/01/2026

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimetangaza kuwatembelea na kuwafariji wahanga wa ukatili wa kutisha wa Oktoba 29,2025 na siku zilizofuata katika kipindi kuelekea miaka 21 ya chama hicho.

Hayo yamesemwa na Naibu Katibu Mkuu CHADEMA bara , Amani Golugwa, wakati anaongea na Watanzania kuelekea kilele cha kumbukizi ya kuzaliwa chama hicho.
Aidha amesema Chama hicho pia kitawatembelea Magerezani wafungwa wa kisiasa wanaoshikiliwa na Serikali kwa makosa wanayodai ni ya uongo.

✍🏿
πŸ¦…

14/01/2026

Waziri MkΓΉu Dkt. , ameagiza watumishi watakaoharibu wafukuzwe kazi na sio kuhamishwa kituo cha kazi.

Dkt. Nchemba ametoa maagizo hayo leo Jumatano, Januari 14, 2026 jijini Dodoma,alipofungua Kikao kazi cha Mawaziri, Naibu Mawaziri, Makatibu Wakuu na Manaibu Makatibu Wakuu wa Wizara za Kisekta mkoani humo.

✍🏿
πŸ¦…

14/01/2026

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Paul Makonda (baba_keagan), amekutana na kufanya mazungumzo na Msanii wa Muziki wa kizazi kipya Ally Kiba kuhusu maandalizi ya mashindano ya Ramadhan Cup mwaka 2026.

Mazungumzo ya Waziri Makonda, na Msanii Ally Kiba, yamefanyika Januari 14, 2025 Mtumba jijini Dodoma, ambapo Makonda amemuhakikishia msanii huyo kuwa, wizara itatoa ushirikiano wa kutosha kufanikisha mashindano hayo.

✍🏿
πŸ¦…

14/01/2026

Waziri Mkuu Dkt. , ameagiza kuhusu kazi zinazoweza kufanywa na Watanzania ziachwe zifanywe na Watanzania na sio raia wa kigeni.

Dkt. Nchemba ametoa maagizo hayo alipofungua Kikao cha Mawaziri, Naibu Waziri, Makatibu Wakuu na Manaibu Makatibu Wakuu wa Wizara na Kisekta kujadili fursa za ajira ndani na nje ya nchi .

✍🏿
πŸ¦…

14/01/2026

amewajibu wale wote waliokuwa wanamcheka baada ya gari zake kuonekana zimebebwa kurudishwa kwa mmiliki wake.

✍🏿
πŸ¦…

14/01/2026

Hatimaye ameanza kupata watetezi baada ya kuchekwa na watu wengi kwenye mitandao ya kijamii kuhusu kuonekana kwa gari anazodaiwa kumiliki kurudishwa kwa mmiliki halali.

Msanii na mwanaharakati awatolea uvivu wote wanaomcheka Chief Godlove baada ya tukio hilo.

✍🏿
πŸ¦…

14/01/2026

Naibu Waziri wa Habari, Uramaduni, Sanaa na Michezo, Hamis Mwinjuma, amemshukuru Waziri wa Nchi - Ofisi ya Rais (Kazi Maalum) Prof. Palamagamba Kabudi, kwa ushirikiano na maelekezo yaliyolenga kuendeleza wizara kipindi walipofanya kazi pamoja.

Ametoa shukrani hizo wakati alipopata nafasi ya kumuaga waziri huyo, na kumkaribisha Waziri wa Wizara hiyo, Paul Makonda, Januari 13, 2026, Mtumba jijini Dodoma.

✍🏿
πŸ¦…

Address

Mwenge
Dar Es Salaam

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Taimediatz posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share