Video.
"Lissu hawezi akamtukana Mbowe kweye mtandao na wala Mbowe hawezi kufanya hivyo. Waaoleta shida ni wapambe wa Mbowe, wapambe wa Lissu, ndiyo wanaoleta shida”, Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kanda ya Victoria na Mtia nia wa nafasi ya Umakamu Mwenyekiti wa chama hicho bara Ezekia Wenje akizungumza na wanahabari siku ya Ijumaa Januari 3, 2025 mkoani Mwanza.
Video:
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Kanda ya Victoria na Mtia Nia wa Nafasi ya Umakamu Mwenyekiti wa chama hicho Bara, Ezekia Wenje, ameahidi kushirikiana na mwenyekiti yeyote atakayechaguliwa katika uchaguzi wa ndani wa chama hicho.
Akizungumza na wanahabari siku ya Ijumaa, Januari 3, 2025, jijini Mwanza, Wenje amesisitiza umuhimu wa mshikamano ndani ya chama, akisema hawezi kununa endapo atachaguliwa kuwa Makamu Mwenyekiti huku nafasi ya Mwenyekiti ikienda kwa mtu mwingine, kama vile Tundu Lissu.
"Mimi leo nichaguliwe kuwa Makamu Mwenyekiti (CHADEMA), labda Lissu achaguliwe kuwa Mwenyekiti, yaani watu wa CHADEMA wapige kura halafu mimi ninanuna? Lazima niangalie ni namna gani tutatengeneza mahusiano ya kufanya kazi pamoja," amesema Wenje.
Wenje amewahimiza wanachama wa CHADEMA kuzingatia mshikamano na kushirikiana bila kujali matokeo ya uchaguzi wa ndani. Ameongeza kuwa viongozi waliochaguliwa wanapaswa kuonyesha mfano mzuri wa kushirikiana ili kuimarisha chama na kujiandaa kwa uchaguzi mkuu wa mwaka 2025.
Kauli ya Wenje imekuja wakati CHADEMA ikielekea kwenye uchaguzi wa ndani wa chama, ambao unatarajiwa kuamua viongozi wake wa kitaifa na kuimarisha maandalizi kuelekea uchaguzi mkuu ujao.
"Kuomba ni kujidhalilisha, lakini kwa kuwa naomba kwa ajili ya kuwasaidia hawa wenye uhitaji Maalumu acha tu nidhalilike" - Steve Nyerere wakati akikabidhi pikipiki, viti mwendo, chakula na mahitaji mengine kwa watu wenye uhitaji Maalumu katika viwanja vya Karimjee Dar es Salaam, Septemba 31, 2024.
Mhandisi Pamela Masai amefika hii leo kwenye ofisi ndogo za chama Cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA Kinondoni jijini Dar es Salaam na kuchukua fomu ya kuwania nafasi ya Katibu Mkuu wa Baraza la Wanawake wa Chama hicho BAWACHA.
Akizungumza mara baada ya kukabidhiwa fomu hiyo, Pamela amesema kwa kutumikia Chama hicho tangu 2007 bila ya kuwa na cheo Cha juu, sasa ameona ni wakati sahihi kuwania nafasi hiyo ili kuwainua kina mama wa kitanzania na ndani ya Chama hicho kiuchumi ili kuondokana na hali duni ya maisha.
Mgombea wa nafasi ya Katibu Mkuu wa Baraza la Wanawake Chadema (Bawacha) Pamela Massaiy amesema baraza hilo linaongoza kwa rushwa akieleza mkakati wa kukomesha vitendo hivyo.
Japo amesema hana vidhibitisho vya kuwatia hatiani wahusika, kigezo alichokitumia kuibua tuhuma hizo ni wagombea wa nafasi hiyo kuwasafirisha wajumbe kutoka mikoani kufika Dar es Salaam kuwapigia kura.
Matukio ya bata Arusha wakati wanaufunga mwaka Kwa kishindo na mkuu mkoa Mh. Paul Makonda
Tusichekane jamani hakuna wa maana, unaweza usifanye jambo A lakini ukawa mfanyaji mzuri wa jambo B
Video:
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limefanikiwa kudhibiti ajali barabarani katika kipindi cha Sikukuu za Krismasi na Mwaka Mpya 2025 kupitia mikakati kabambe ya ukaguzi wa madereva. Jumla ya madereva 179 walikaguliwa kwa kupimwa ulevi, ambapo madereva 30 walikutwa na kiwango cha ulevi kilichozidi miligramu 80, kinyume na sheria za usalama barabarani.
Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Jumanne Muliro, akizungumza Januari 2, 2025, amesema kati ya madereva waliokamatwa, 22 walikuwa katika Wilaya ya Kinondoni, sita (6) katika Wilaya ya Ilala, na wawili (2) katika Wilaya ya Temeke.
Kamanda Muliro ameongeza kuwa Jeshi hilo limechukua hatua kali kwa kuwafungia leseni za udereva madereva waliokamatwa kwa kipindi cha miezi sita. Hatua hii imechukuliwa kwa mujibu wa kifungu 28 (3)(b) cha Sheria ya Usalama Barabarani, Sura ya 168, iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2002.
Waziri wa nchi,ofisi ya Rais mipango na uwekezaji mhe Kitila mkumbo leo Januari 2, 2025 amezindua na kuweka jiwe la msingi kwenye mradi wa ujenzi wa shule ya sekondari kainam yenye kidato cha tano na cha sita wenye thamani ya Shilingi millioni 428,9000
Akizungumza wakati wa uwekaji wa jiwe hilo la msingi waziri Kitila amesema lengo la mradi ni kuongeza miundombinu ya kidato cha tano na cha sita na kutoa nafasi kubwa ya wanafunzi wengi kuingia kidato cha tano na cha sita
Mkuu wa shule hiyo Emanuel Nikodemus wakati akieleza Maendeleo ya mradi huo amesema shule iyo ilipokea kiasi cha shilingi millioni 428,9000 mwezi mei, 2023 kwa ajili ya ujenzi wa mabweni mawili(2),madarasa sita(6) na matundu tisa ya vyoo ambapo matundu yaliyojengwa ni kumi(10)
Hata ivyo amebainisha jinsi mradi huo ulivyoleta manufaa kwa wanafunzi na wadau wa elimu shuleni hapo ambapo imesaidia kuongezeka kwa idadi kubwa ya wanafunzi wa kidato cha tano na sita kutoka wanafunzi 44 hadi kufikia wanafunzi 612
Hii ni ziara ya kwanza ya waziri wa nchi ,ofisi ya Rais mipango na uwekezaji mhe. Prof Kitila Mkumbo mkoani Manyara kwa mwaka 2025 ambapo ataifanya kwa siku tatu(3) yenye lengo la kutembelea na kukagua miradi mbalimbali ya kimaendeleo katika mkoa huo
Mhandisi Pamela Masai amefika hii leo kwenye ofisi ndogo za chama Cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA Kinondoni jijini Dar es Salaam na kuchukua fomu ya kuwania nafasi ya Katibu Mkuu wa Baraza la Wanawake wa Chama hicho BAWACHA.
Akizungumza mara baada ya kukabidhiwa fomu hiyo, Pamela amesema kwa kutumikia Chama hicho tangu 2007 bila ya kuwa na cheo Cha juu, sasa ameona ni wakati sahihi kuwania nafasi hiyo ili kuwainua kina mama wa kitanzania na ndani ya Chama hicho kiuchumi ili kuondokana na hali duni ya maisha.
Mgombea wa nafasi ya Katibu Mkuu wa Baraza la Wanawake Chadema (Bawacha) Pamela Massaiy amesema baraza hilo linaongoza kwa rushwa akieleza mkakati wa kukomesha vitendo hivyo.
Japo amesema hana vidhibitisho vya kuwatia hatiani wahusika, kigezo alichokitumia kuibua tuhuma hizo ni wagombea wa nafasi hiyo kuwasafirisha wajumbe kutoka mikoani kufika Dar es Salaam kuwapigia kura.
Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mhe. Dkt. Doto Biteko amewahimiza Watanzania kuendeleza upendo mshikamano na kuvumiliana zikiwa nyenzo muhimu za kufikia maendeleo na ustawi wa Taifa.
Dkt. Biteko amesema hayo Kijijini kwao Bulangwa, Wilayani Bukombe Mkoani Geita alipojumuika na maelfu ya wananchi katika hafla ya kuukaribisha mwaka mpya 2025.
Amesema Serikali chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imefanya mambo mengi makubwa na mazuri ambayo yanahitaji kuenziwa na kuendelezwa ili kupata maendeleo ya kweli.
"Maono ya Rais Samia yamewezesha upatikanaji wa maendeleo katika sekta mbalimbali kama ujenzi wa miundombinu ya barabara, shule, vituo vya Afya na maji na hatua hii imetambuliwa kitaifa na kimataifa" amesema Dkt. Biteko
Amesemw pia kuwa maendeleo yaliyofikiwa yamepongezwa na taasisi za kimataifa zikiwemo Benki ya Dunia na Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika ( SADC)
Amewataka Wana Bukombe na Tanzania kuhakikisha mwaka mpya wa 2025 unaenziwa kwa kudumisha upendo, kuvumiliana na kusaidiana ili kila mmoja kuwa chanzo cha furaha kwa mwenzake.
Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Geita, Mhe. Martine Shigella aliishukuru serikali kwa utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo
Amemshukuru Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mhe. Dkt. Biteko kwa jitihada za kuendelea kuwa karibu na wananchi wa Bukombe na Mkoa wa Geita katika upatikanaji wa maendeleo.
" Pamoja na majukumu yako ya kitaifa, Mheshimiwa Naibu Waziri Mkuu umeendelea kuwa nasi karibu nasi kuchochea maendeleo ya Mkoa na Jimbo letu la Bukombe" amesema Shigella
Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Mhe. Fatma Mwassa amepongeza kwa hatua ya kujumuika na kusherekea pamoja na wananchi na kusema hatua hiyo inawezesha wananchi kuwa karibu na viongozi wao
Naye Mwenyekiti wa CCM, Mkoa wa Geita, Nicholaus Kasendamila amewataka wakazi mkoa huo wasifanye makosa kitapofika kipindi cha uchaguzi.
" Tulishakubaliana kwamba mwaka huu ni wa uchaguzi Mkuu na upande wa
Meneja Habari na Mawasiliano wa Simba SC, Ahmed Ally akizungumzia hali ya kikosi cha Simba mara baada ya kuwasili nchini Tunisia kwa ajili ya mchezo wa Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya CS Sfaxien utakaopigwa Januari 05, 2025 katika uwanja wa Olympique Hammadi Agrebi.
Mbunge wa Jimbo la Ubungo, Prof. Kitila Mkumbo ameweka bayana mambo mawili ambayo wanachama cha Chama cha Mapinduzi (CCM) wanapaswa kuyazingatia kuelekea katika Uchaguzi Mkuuu wa mwaka huu 2025.
Mambo hayo ni pamoja na lile la kuendelea kumuunga mkono Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa mgombea pekee wa Nafasi ya urais kupitia Chama hicho.
Prof. Mkumbo ameeleza hayo Jijini Dar es Salaam, Januari 01, 2024 katika mkutano mkuu wa Jimbo la Ubungo wakati alipokuwa akizungumza na Wana CCM kwenye kikao hicho.
"Baadae mwaka huu kama taifa tutakwenda kwenye Uchaguzi Mkuu, CCM kama chama kiongozi kinao utaratibu ama Utamaduni wake iliyojiwekea ambapo mgombea wetu katika nafasi ya Urais akishakuwa madarakani huwa anapewa miaka 10 ya kuongoza mihula miwili,
Kwa hiyo niwaambie hakuna haja ya Kubabaika, kwa sasa Dkt. Samia Suluhu Hassan hana mbadala na ndio maana tunasema Rais Samia tunampa Mitano tena aweze kuongoza Watanzania" amesema Prof. Kitila.
@kitilam @ccm_tanzania