Gilly Bonny Tv

Gilly Bonny Tv Independent Media.
(3)

03/02/2025

"Mchango wa serikali katika kuwasaidia wananchi wa makosa ya jinai kwa mwaka 2024 tulitoa takribani mawakili 380 kutoka kwenye matawi yetu yaliyosambaa nchi nzima. Vile vile TLS k**a nilivyosema tumekuwa tukishirikiana na serikali hususan Wizara ya Katiba na Sheria. Vile vile tumeshirikiana katika kuendesha huduma ya msaada wa kisheria wa Watanzania wa hali ya chini waliopo pembezoni inayoenda kwa jina la Mama Samia Legal Aid,"Rais wa Chama Cha Mawakili Tanganyika (TLS) Boniface Mwabukusi.

03/02/2025

"Mheshimiwa Mgeni rasmi. Nikijaribu kuangalia dira ya Taifa ya maendeleo na hali ilivyo ya kisheria, sisi matarajio yetu ni kwamba wakati tukiendelea kuboresha na kujipanga, tuhakikishe kwamba tunaweka utaratibu wa kisheria wa kuhakikisha kuwa sheria na sera zinatungwa katika namna ya ushirikishwaji wa kutosha wa wananchi katika ngazi zote. Jambo la pili, kujenga na kuimarisha ushirikiano wa serikali na sekta binafsi k**a ambavyo tumekwisha kuanza. Kwa hiyo tunaposhirikiana na serikali hatulambi asali,"Rais wa Chama Cha Mawakili Tanganyika (TLS) Boniface Mwabukusi.

03/02/2025

Vijana wa Generation Samia (Kizazi cha Mafanikio) wametangaza kushiriki mbio za marathon kesho, Februari 4, 2025, mkoani Dodoma, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 48 ya Chama cha Mapinduzi (CCM).

Mbio hizo zinatarajiwa kuvutia maelfu ya washiriki kutoka maeneo mbalimbali ya nchi.

Msemaji wa Generation Samia, Sonata Nduka, amesema ushiriki wao ni ishara ya kuthamini mchango wa Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika kuinua uchumi wa vijana kupitia uwekezaji na fursa za ajira.

Maadhimisho ya miaka 48 ya CCM yatafanyika Februari 5, 2025.

Generation Samia wametoa wito kwa vijana wenzao kujitokeza kwa wingi kushiriki hafla hiyo, wakisisitiza kuwa hiyo ni fursa ya kuonesha mshik**ano na kuhimiza maendeleo ya Tanzania.

Rais Samia Suluhu Hassan anatarajia kupokea tuzo ya ‘The Gates Goalkeepers Award' iliyoandaliwa na taasisi ya ‘The Gates...
03/02/2025

Rais Samia Suluhu Hassan anatarajia kupokea tuzo ya ‘The Gates Goalkeepers Award' iliyoandaliwa na taasisi ya ‘The Gates Foundation’ kwa kutambua mchango wake katika Sekta ya Afya.

Waziri wa Afya, Jenista Mhagama amesema Rais Samia ndiye kiongozi wa kwanza kupata tuzo hiyo kwa bara la Afrika, ambapo ni kufuatia ripoti ya utafiti wa demografia na afya ya mwaka 2022 inayoonesha kupungua kwa vifo vitokanavyo na uzazi kwa kiwango cha asilimia 80 pamoja na watoto chini ya miaka mitano.

03/02/2025

Tarehe 22 Februari 2025, Viongozi wa dini nchini kwa umoja wao wataungana kuliombea Taifa sambamba na kumuombea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan, ambapo pamoja na hayo wataiombea amani Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) kwa vita inayoendelea, ambayo imesababisha vifo vya askari wawili wa JWTZ.

03/02/2025

Leo tarehe 22 Februari 2025, Viongozi wa dini nchini kwa umoja wao wataungana kuliombea Taifa sambamba na kumuombea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Aidha viongozi wa dini hao wametangaza kua wanategemea Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania , Dr. Samia Suluh Hassan kuwa mgeni rasmi wa tukio hilo.

03/02/2025

Leo tarehe 22 Februari 2025, Viongozi wa dini nchini kwa umoja wao wataungana kuliombea Taifa sambamba na kumuombea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan, ambapo pamoja na hayo wataiombea amani Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) kwa vita inayoendelea, ambayo imesababisha vifo vya askari wawili wa JWTZ.

03/02/2025

“Waheshimiwa niungane na wote waliotangulia kumshukuru Mwenyezimungu. Kwa neema ha uhai na kutuwezesha kukutana tena. Nimefurahi kujumuika nanyi kwenye kilele cha wiki ya sheria na kuzindua shughuli za mahak**a nchini kwa mwaka 2025.

Mheshimiwa jaji Mkuu, nikiangalia kauli mbiu mliyokuja nayo mwaka huu inayosema Tanzania ya 2050, nafasi za taasisi zinazosimamia haki madai katika kufikia malengo makuu ya Dira ya Taifa ya maendeleo.

Kauli mbiu hii inanipa faraja kwamba agizo langu nililolitoa wakati napokea taarifa ya k**ati ya kuangalia taasisi ya haki jinai sasa linakwenda kufanyiwa kazi,”Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan.

03/02/2025

Naibu Waziri wa Nishati, Mhe Judith Kapinga amesema ni azma ya Serikali kuhakikisha wananchi wanapata umeme wa uhakika na unaotabirika kwa ajili ya shughuli za kijamii na kimaendeleo.

Mhe. Kapinga ameyasema hayo leo Januari 03, 2025 bungeni jijini Dodoma wakati akijibu swali la la Mbunge wa Lushoto Mhe. Shabani Shekilindi aliyetaka kufahamu ni lini Serikali itaondoa changamoto ya kukatika umeme katika Wilaya ya Lushoto kwa kuweka suluhisho la kudumu.

"Tutafuatilia kwa hii wiki moja kufahamu ni nini changamoto ya kukatika kwa umeme Wilaya ya Lushoto, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge iwapo kuna matengenezo tutahakikisha yanakamilika kwa haraka." Amesisitiza Mhe. Kapinga

Akijibu swali Mbunge wa Nkasi Kusini, Mhe. Vicent Mbogo aliyetaka kufahamu uwepo wa nishati ya umeme katika Kijiji cha Msamba-Masokolo, Lyapinda, Izinga na Lyele na katika Vitongoji vya Kisenga na Lupata, Mhe. Kapinga amesema Wilaya ya Nkasi ina jumla ya vijiji 90 ambapo vyote vimepatiwa huduma ya umeme vikiwemo vijiji vya Lyele na Lyapinda.

Aidha, amesema Kitongoji cha Lupata kilichopo katika Kijiji cha Lyapinda kitapata umeme kupitia mradi wa Vitongoji 15 vya Mbunge utakaotekelezwa na Mkandarasi aitwae M/s STEG International Services Ltd ambaye ameshakamilisha hatua za upimaji na usanifu.

Ameongeza kuwa, uhakiki wa Kitongoji cha Kisenga umekamilika na Kitongoji hicho kitapatiwa umeme kupitia mradi wa vitongoji (HEP IIB).

PICHA: Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt, Samia Suluhu Hassan Katika Matukio tofautitofauti aliposhiriki  ...
03/02/2025

PICHA: Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt, Samia Suluhu Hassan Katika Matukio tofautitofauti aliposhiriki Maadhimisho ya Siku ya Sheria Nchini kwa mwaka 2025 yaliyofanyika Viwanja vya Chinangali Mkoani Dodoma leo February 03,2025.

Maadhimisho hayo yanaongozwa na kaulimbiu isemayo "Nafasi ya Taasisi zinazosimamia Haki Madai katika kufikia malengo Makuu ya Dira ya Maendeleo ".

02/02/2025

Alichosema Msemaji wa timu ya Tabora United, Christina Mwagala baada ya kupokea kichapo cha 3-0 nyumbani kwao dhidi ya Simba SC.

02/02/2025
02/02/2025

VIDEO : Msemaji wa klabu ya Simba, Ahmed Ally akiwamwagia sifa wachezaji wa klabu yake baada ya ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Tabora United katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC.

02/02/2025

Katibu wa Jumuiya ya Watanzania Waishio Nchini China ikijumuisha Wafanyabiasha na Wanafunzi Ndugu. Alawi Abdullah amesema hayo Leo Tarehe 2 Februari 2025 wakati akizungumza na Waandishi wa Habari Jijini Dar es Salaam

02/02/2025

Ahadi ni deni, Jumatatu kesho wana Simba mkanyoe ndevu hizi 😂😂

Mdomo uliponza kichwa

02/02/2025

Katibu wa Jumuiya ya Watanzania Waishio Nchini China ikijumuisha Wafanyabiasha na Wanafunzi Ndugu. Alawi Abdullah ametoa wito kwa Watanzania kuchangamkia fursa ya kushiriki katika Maonyesho ya Kimataifa ya Biashara ya CANTON FAIR, yatakayofanyika katika jiji la Guangzhou, nchini China, kuanzia tarehe 15 Aprili hadi 2 Mei 2025.

Akizungumza na Waandishi wa Habari Leo Tarehe 2 Februari 2025 Jijini Dar es Salaam, katibu Huyo amesema Maonyesho haya ni fursa kubwa kwa wafanyabiashara na viwanda vya Tanzania kuonesha bidhaa zao na kuendeleza ushirikiano wa kibiashara na mataifa mengine.

Aidha hiyo ni hatua muhimu katika kuhakikisha kuwa Watanzania wanaendelea kufaidika na fursa za kibiashara na kiuchumi duniani

02/02/2025

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amefanya kazi kubwa ya kuing'arisha Chamwino kwa kutatua changamoto mbalimbali za wananchi wa Jimbo hilo.

Hayo yamebainishwa leo Februari 02, 2025 na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko, wilayani Chamwino mkoa wa Dodoma mara baada ya uwasilishwaji wa taarifa ya utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM kwa kipindi cha miaka 5, (2020 2025) iliyowasilishwa na Mbunge wa jimbo hilo ambaye pia ni Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Deogratius Ndejembi.

"Nimemsikiliza Mhe. Ndejembi akieleza kazi kubwa ambayo Serikali imeifanya hapa Chamwino, ni dhahiri kwamba Serikali ya CCM chini ya Uongozi wa Dkt. Samia imefanya kazi kubwa ya kuing'arisha Chamwino na kutatua changamoto mbalimbali za wananchi wa Jimbo hili. Hongereni sana, " Amesema Mhe. Biteko

Aidha, amewataka kuendelea kuisimamia Serikali kuanzia ngazi ya chini ili kuendelea kuyagusa maisha ya wananchi kikamilifu na kutatua kero na changamoto walizonazo.

"Ni ukweli usiopingika kwamba Serikali ya CCM imefanya kazi kubwa sana na ya kutukuka ya kuiletea nchi yetu maendeleo. Ninyi hapa Chamwino ni mashahidi wakubwa wa maendeleo yaliyofanywa na Serikali chini ya Uongozi wa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan," ameongeza Dkt. Biteko.

Vile vile, Serikali imewekeza zaidi ya bilioni 13 katika kugharimia elimu ya Sekondari tu katika Wilaya ya Chamwino.

"Tunashuhudia kuendelea kukamilika kwa ujenzi wa Shule hii ya Mkoa ya Sekondari ya ya Bweni ya Wasichana Manchali ambapo Watanzania wote watapata huduma za elimu," ameongeza Dkt. Biteko

Katika hatua nyingine amesema kuwa, uboreshaji wa miundombinu kwa kujenga madaraja, vivuko na barabara za lami ndani ya Jimbo la Chamwino zaidi ya Shilingi bilioni 17.9 zimetumika.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Dodoma, Alhaj, Adam Kimbisa amewahimiza wakazi wa Chamwino kuendeleza umoja na mshik**ano miongoni mwao ili kulinda madanikio yaliyofikiwa.

Pia, amewata kutumiia mvua za msimu kulima kwa wingi na watakapopata mavuno wahifadhi sehemu ya mavuno yao ili kuwa na akiba ya chakula kwa siku zijazo.

Address

Sinza Makaburini
Dar Es Salaam
1110111101(2)

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Gilly Bonny Tv posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Videos

Share