22/12/2025
Kampuni ya Azam Media Group imelaani vikali mfululizo wa matukio yaliyojitokeza jana katika Uwanja wa Dandora jijini Nairobi, Kenya wakati wa matangazo ya moja kwa moja ya mechi kati ya Nairobi United FC na Gor Mahia FC saa 10:00 jioni, ambapo gari la OB (Outside Broadcast) lilivamiwa na wahuni hivyo vifaa vya Matangazo vilivyokuwepo ndani ya gari hilo kuharibiwa
Wakati Azam Media Group ikiendelea kujitahidi kuinua na kuunga mkono ukuaji wa Ligi Kuu ya Kenya kwa kuhakikisha ligi hiyo inaonekana kwa kiwango cha juu kupitia matangazo ya moja kwa moja, matukio k**a haya ya uharibifu si tu kikwazo bali pia yanaonyesha taswira ya kusikitisha ya Ligi Kuu ya Kenya.