Halisi herbal and natural remedy

Halisi herbal and natural remedy Let's learn and grow together!

Passionate about the healing power of plants. 🌱 This page offers educational videos on herbalism, including plant identification, harvesting, preparation, and safe use of herbal remedies.

JE UNA NUKSI/ UMEFUNGWA KIROHO..?Leo nitaongea kiroho zaidi, huu mmea una faida za kisayansi lakini pia za kiroho.NOTE: ...
29/01/2025

JE UNA NUKSI/ UMEFUNGWA KIROHO..?

Leo nitaongea kiroho zaidi, huu mmea una faida za kisayansi lakini pia za kiroho.

NOTE: Wengi mambo yakianza kwenda kombo husingizia nuksi ila kiukweli ni kwamba maisha wanayoishi, uchumi wao, ukosefu wa maarifa, stress, n.k ndio visababishi, unakuta mtu analalamika pesa inaisha haraka kumbe ni yeye mwenyewe ana matumizi mabovu.

Ila pia katika jicho la tatu Mikosi, nuksi, vifungo, n.k haya mambo yapo, unaweza kuyapata kwa sababu ya watu yaani kichawi au kwa kutokana na mtindo wa maisha (kupitia njiani, kusibiwa na jini, kuzini sana na watu wengi, n.k).

Endapo umefanya uchunguzi na umethibitisha una mikosi, nuksi, vifungo, n.k basi ufanye hivi.

1.kanunue chumvi ya mawe.

2.kachume kivumbas / mvumbasi / mavumbasi (kwa wenzetu wahindi na bara la asia umepewa heshima kubwa kwa kupewa majina k**a
Sacred plant (mmea mtakatifu), Mother Medicine of Nature (mama wa dawa za asili), The Queen of Herbs (malkia wa mitishamba), The Incomparable One (hakuna mmea wa kuulinganisha nao)...Ni mmea muhimu ambao nauonaga unajiotesha sehem nyingi sana ila nashangaaga watu wanavyoubeza )

Ogea asubuhi na usiku, uwe unanuia hio mikosi na nuksi zikutoke, mfano

Mimi fulani bin fulani nakuamuru wewe kivumbasi mmea wenye nguvu na chumvi mtoa mikosi, nuksi, vifungo, n.k ., kivumbasi wewe ni tiba na ni kinga unatumika kutukinga binadamu kwa kufukuza wadudu k**a mbu wanaotuletea madhara wanadamu, nakuomba unifukuzie watu wanaonitakia, kunipangia na kunifanyia mabaya, futa nuksi zinazoniandama, chumvi unavyowekwa kwenye haya maji unayeyuka basi ndivyo ambavyo mikosi, nuksi, vifungo, alama za wabaya ndani yangu zitayeyuka na kupotea kabisa, wewe chumvi ni mweupe yafanye maisha yangu yawe na nuru angavu ya weupe kwa kunitolea hili giza jeusi linaloniandama n.k , Kwa uwezo wako Mwenyezi Mungu ulieumba hivi vitu na kuvipa neema na uwezo huu basi naomba kibali na baraka zako zoezi hili lifanikiwe.....uwe unanuia hivo, ukimaliza ingiza chumvi na kivumbasi kwenye ndoo kisha ogea, usiogee chooni.

ogea siku saba.

Pia waweza tumia chumvu ya mawe na magadi au chumvi ya mawe na mchai chai, n.k k**a huu mvumbasi umeukosa.

Muhimu kuzidi vyote: Sali sana.

Je huu ni uchawi..?
Hapana huu sio uchawi, tunatumia vitu alivyoumba Mungu kwa nia nzuri, uchawi ni pale mtu anatumia kwa nia mbaya mfano kutengeneza malimbwata, kufarakanisha watu, kubaribu nyota za watu n.k, hii unajifanyia wewe kwa nia njema kabisa bila kumdhuru yeyote, na kikubwa ukimtegemea Mungu.

Address

Dar Es Salaam

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Halisi herbal and natural remedy posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Halisi herbal and natural remedy:

Videos

Share