
26/12/2024
Kupitia ukurasa wake wa instagram msemaji wa klabu ya simba sc AHMED ALLY ameandika haya.....
Dodoma Jiji jana kafungwa magoli mawili ya Uwongo, Moja la Offside na pili Penati ya uongo lakini Kocha wao hajalalamika kuonewa wala kudhulumiwa zaidi amesema AMESTAHILI KUFUNGWA
Rejea mechi ya Dodoma Jiji Vs Simba, baada ya sisi kufunga goli la Penati ya halali alitoa mapovu kulaumu Waamu*i yote ni kuaminisha watu kuwa tumemdhulumu na kutaka kutia dosari kazi nzuri inayofanywa na Simba Sports msimu huu
Nimeyasema haya ili Wana Simba tuone vita ni kubwa iliyombele yetu ni namna gani Wapinzani hawapendi kufungwa na sisi lakini wanafurahi kufungwa na wengine, ndio maana haishangazi kuona tunapata ushindi wa jasho na damu
Wale wanaosema tunashinda lakini tunashikilia roho sio kwa sababu tuu ya ubora ni kwa sababu wapinzani wanauma meno kupitiliza na sisi ndio tunapenda ushindani wa aina hiyo
Kuelekea mechi zijazo Wana Simba tunapaswa kuunganisha nguvu kweli kweli, tupambane kwa nguvu sawa kuhakikisha tunatimiza malengo yetu
Nguvu Moja๐ช Ubaya Ubwela ๐ฆ