2skys TV

2skys TV the WORLD'S most FREE-THINKING about news

Shirika la ndege la nchini Tanzania | ATCL | linategemea kupokea ndege mpya ya Boeing Dreamliner 787-8 ambayo itakwenda ...
25/08/2024

Shirika la ndege la nchini Tanzania | ATCL | linategemea kupokea ndege mpya ya Boeing Dreamliner 787-8 ambayo itakwenda kuongeza idadi ya ndege na nguvu katika la Shirika la ndege la ATCL .

— Ndege hiyo itapokelewa katika uwanja wa ndege wa Abeid Karume uliopo huko visiwani Zanzibar na mgeni rasmi anategemewa kuwa Rais wa Zanzibar Dk. Hussein Mwingi .

—Ndege ya Boeing Dreamliner 787-8 ni moja ya ndege bora sana zilizowahi kutengenezwa na kampuni ya Boeing ambayo husukumwa na Injini | Royce Royce Trent 1000 | kubwa mbili ambayo hufanya ndege hiyo kusafiri kwa kasi kubwa ya kilomita 954 kwa saa .

—Ndege ya Boeing Dreamliner 787-8 ina uwezo wa kubeba kiasi cha lita 126,917 ambazo zinaiwezesha ndege hiyo kusafiri kwa umbali wa kilomita 15,000 yaani inaweza kusafiri umbali mrefu bila ya kuhitaji huduma ya ujazaji mafuta .

— Pia ndege hii inauwezo wa kubeba abiria 262 hadi 280 na kubeba kiasi cha tani 15 hadi 20 za mizigo .

— Ujio wa ndege hii unakwenda kupanua mtandao wa njia za usafirishaji katika shirika la ATCL ambapo ni pamoja na kufungua safari mpya za | Kinshasa Goma Muscat na Lagos | .

Chanzo (AstronomyKiswahili)

17/08/2023

😂

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na Rais wa Kenya, Mhe. William Ruto, Rais wa Malawi, Mhe. Dkt...
27/07/2023

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na Rais wa Kenya, Mhe. William Ruto, Rais wa Malawi, Mhe. Dkt. Lazarus Chakwera, Rais wa Madagascar, Mhe. Andry Rajoelina, Rais wa São Tomé na Principe, Mhe. Carlos Vila Nova pamoja na Rais wa Sierra Leone, Mhe. Julius Maada Bio wakati wa Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika Kuhusu Rasilimali Watu (Africa Heads of State Human Capital Summit) uliyofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Dar es Salaam Julai 26, 2023

Mamlaka ya Hali ya Hewa Nchini (TMA) imesema El Nino inatarajiwa kuwepo katika kipindi cha Mvua za Msimu wa Vuli zitakaz...
19/07/2023

Mamlaka ya Hali ya Hewa Nchini (TMA) imesema El Nino inatarajiwa kuwepo katika kipindi cha Mvua za Msimu wa Vuli zitakazoanza kunyesha Oktoba hadi Desemba 2023 ambazo zitasababisha athari katika maeneo mbalimbali

Meneja wa Utabiri wa , Dkt. Mafuru Kantamla, amesema hadi kufikia sasa utabiri umeonesha uwezekano wa kutokea ni asilimia 90, na Mikoa ambayo itaathirika ni Arusha, Manyara, Kilimanjaro, Dar es Salaam, Tanga, Pwani, Lindi na Mtwara

https://2skystvtanzania.blogspot.com/2023/07/tma-yatahadharisha-uwepo-wa-el-nino-kwa.html

11/07/2023

Nimekutana na ujumbe unasambaa kwenye mitandao ya kijamii Twitter, Instagram na hata JF nimeona mtu kaweka u*i kuwa wanafunzi tena wakike ...

02/07/2023

KUNA UKWELI JUU YA MANENO YA DADA HUYU??

Mbunge wa jimbo la Mbarali mkoani Mbeya kupitia tiketi ya chama cha CCM, ndungu Francis Leonard Mtega amefariki dunia le...
01/07/2023

Mbunge wa jimbo la Mbarali mkoani Mbeya kupitia tiketi ya chama cha CCM, ndungu Francis Leonard Mtega amefariki dunia leo kwa ajali ya bodaboda.

Bwana alitoa na bwana ametwaa, jina lake lihimidiwe.

Innalillah wainna ilayhi rajiuun.

23/06/2023

Once again , this is Zayfaa's Furniture, 💥💥💥💥

And for video Advertisement call us 0689079948

Send a message to learn more

22/06/2023

Viumbe watakao tawala dunia.

21/06/2023

Basi kampuni ya mwekezaji kutoka China, New Force/Golden Deer imepata ajali na kuua watu kadhaa.

Wakati ajali hiyo inatokea ndani ya mwezi huu itakuwa ajali ya 3 kwa kampuni hiyo baada ya last week kupata pia ajali maeneo ya Morogoro.

Chanzo ni mwendo wa mashindano.

======

Kamanda wa Polisi, Kamishna Msaidizi wa Polisi, ACP John Makuri amethibitisha tukio la ajali mbaya iliyotokea katika Eneo la Igando Wilaya ya Waging'ombe ikihusisha basi la NewForce lililokuwa linatoka Dar kwenda Sumbawanga.

Kwa mujibu wa Kamanda Makuri, Idadi ya vifo vi 5 na Majeruhi kadhaa wakipelekwa Hospitali ya Kanisa ya Ilembula

Michael Macharia Njiri maarufu kwa jina la Dj Brownskin ameshtakiwa kwa kusaidia kujiua kinyume na kifungu cha 225 (b) c...
12/06/2023

Michael Macharia Njiri maarufu kwa jina la Dj Brownskin ameshtakiwa kwa kusaidia kujiua kinyume na kifungu cha 225 (b) cha kanuni ya adhabu.

Inadaiwa kuwa tarehe 29 Julai 2022, eneo la Kariobangi South, kata ya Buruburu, alitoa usaidizi kwa Sharon Njeri Mwangi ili ajiue.

Kwa kosa la pili, Brownskin anashtakiwa kwa uzembe wa kushindwa kuzuia kosa la jinai, ambapo alishindwa kutumia njia zote za busara kuzuia kujiua.
DJ huyo pia anashtakiwa kwa kuharibu ushahidi, ambapo inadaiwa kuwa

"kwa kujua kuwa simu yake ya mkononi yenye nambari ya kadi ya simu 07**** iliyokuwa mikononi mwake inaweza kuhitajika k**a ushahidi katika kesi ya kisheria, aliiondoa kwa nia ya kuzuia kutumika k**a ushahidi."
Brownskin alikana mashtaka hayo na amezuiliwa kwa siku tatu, akisubiri ripoti ya uangalizi wa utimamu wa akili.

Mshtakiwa alik**atwa tarehe 1 Juni 2023, kuhusiana na kifo cha mkewe.
Tarehe 4 Juni, DCI ilisema DJ huyo alik**atwa baada ya kukaidi wito wa polisi kurekodi taarifa kuhusiana na kifo cha mkewe.

"Katika kanda ya video yenye kuumiza moyo iliyotolewa na bloga maarufu tarehe 1 Aprili, miezi 9 baada ya mabaki ya Njeri ku*ikwa, Dakika zake za mwisho zilirekodiwa na DJ huyo alipokuwa akiweka kitu chenye sumu ndani ya kikombe na kunywa bila kusita. Kisha alianguka kutoka kwenye kochi na kuwaita watoto wake wawili kuwajulisha juu ya kifo chake kinachokuja," DCI ilisema katika taarifa yake na kuongeza kuwa mtuhumiwa alituma video hiyo kwa mpenzi wake mwingine anayeishi nje ya nchi.

Pweza ni aina ya samaki asiye na magamba anayepatikana katika bahari (maji chumvi), umaarufu wake unajulikana kwa kuwa k...
10/06/2023

Pweza ni aina ya samaki asiye na magamba anayepatikana katika bahari (maji chumvi), umaarufu wake unajulikana kwa kuwa kiumbe mwenye "miguu" mingi na umbo la kushangaza kidogo.

Pweza ni moja wapo ya viumbe wenye damu ya Blue, Protein yake kwenye damu huonekana kusaidia kwenye manipulation ya hormone inayosaidia kusukuma damu kwenye mfumo wa uzazi wa Binadamu mwanaume kuwa na nguvu.
(Sababu ya damu yake kuwa Blue na hizo hormone niliwahi ku*itaja kwenye makala za nyuma tulipoongelea Haemoglobin na damu nyekundu ya Binadamu)

Kingine kinachompa Pweza umaarufu na upekee ni wingi wa Ubongo,
Pweza ana bongo zipatazo Tisa (9) zote zikifanya kazi tofauti-tofuati kwa nafasi yake, ukilinganisha Binadamu anao ubongo mmoja tu.

Tafiti za kisayansi zinakisia labda kuwa bongo nyingi zinasaidia kuendesha mwili wake wenye "mikono" mingi, swali linabaki kuwa
"Je, bongo hizo zinawasiliana vipi kuweza kuundesha mwili kwa pamoja?"
Mfano ubongo mmoja unahusika na mguu mmoja, uwiano wa miguu yote kushirikiana kumpeleka pweza sehemu anayoitaka unafanyikaje.!?

Sayansi inasema labda kuna Ubongo mmoja mkuu, unasimamia bongo nyingine 8 zinazofanya kazi kwenye jozi ya mbili (pair)
Au k**a ilivyo kwa Binadamu kuwa na Tezi (glands) ndivyo kwa Pweza ana hivyo vinavyoonekana k**a ubongo.

Jambo lingine linaloonekana la kushangaza kwenye maisha ya Pweza, yeye ni mmoja wa Wanyama wanaokufa baada ya kuzaa mara moja.

Uliwahi kusikia kuhusu viumbe kujifungua kisha vikafa, ikiwemo aina fulani za vinyonga, hilo tutakuja kuliangalia siku nyingine, tuanze na Pweza leo.

Aina zote za Pweza zinaonekana kufa baada ya kuzaa mara moja, Pweza hutaga mayai, huyaatamia au kuyaangalia yakue na kutotoa vitoto na hapo hufa.
Pweza hufa baada ya kupata uzao wake mmoja tu, na hapo huwa na umri wa miaka k**a 2 hadi 3.

Kulingana na aina, Pweza hutaga mayai kati ya elfu 15 hadi laki 5 kwa uzao wake mmoja, kuna wanaotaga mayai 100 hadi 300 wale wenye mayai makubwa yanayoonekana. Mama Pweza huatamia mayai yake bila kutoka eneo la kutagia mpaka atakapoona mayai yanaanza kutotolewa.!

Kipindi chote cha uangalizi na ulinzi wa hali ya juu wa mayai yake, Mama Pweza huwa hatafuti chakula, hivyo wataalamu wa kujifunza tabia za kiumbe huyo wanasema kinachomuua huwa ni njaa.

Pweza huangalia na kulinda mayai yake mpaka yatotolewe kwa kipindi kati ya wiki 4 hadi wiki 53 kulinga na aina ya Pweza na wingi wa mayai ambapo siku hutofautiana, lakini kwa kipindi chote cha kuatamia njaa huwa kitu kinachomuua taratibu mnyama huyu.

Mama Pweza hukaa na mayai yake kipindi chote, huanza kula viumbe vidogo vidogo vinavyokatiza kwenye 18 zake, na hata baadhi udongo, mchanga na mimea midogo midogo iliyo karibu.

Njaa hu*idi kuwa nyingi na hatakiwi kuacha mayai yake, cha ajabu huanza hata kutafuna baadhi ya miguu yake, taratibu huanza kujigeuza kitoweo na kubakiza miguu k**a miwili tu ya mbele, ambayo husaidia kujivua ngozi iliyochoka na kuvaa mpya k**a nyoka.

Kujivua ngozi huwa ni harakati za kupata chakula njaa ikizidi, huanza pia kula ngozi yake mwenyewe na baadhi nyama za mwili wake, hii ni kiwango cha kukaribia kufa maana hukosa kitu cha kula, yote hii huwa ni kulinda mayai yake mpaka yatotolewe.

Mpaka nguvu zinamuishia kabisa, mayai huwa yameanza kutotolewa walau 1 ya 16 ya mayai yote huwa yameanza kutoa vitoto pale Mama Pweza anapokata roho kabisa.
Upendo ulioje huu.!?

Ndani ya siku Tatu tangu kifo cha Mama Pweza mayai karibu yote huwa yametotolewa, na vitoto huwa k**a burungutu la Vumbi linalotembea bila mzazi, chakula chao huwa ni mzoga wa mama yao aliyekufa akiwalindia uhai. Baada ya hapo maelfu ya vitoto hivi huishi vikiwa yatima.

Yatima.!?
Ndio Yatima,
Kwa sababu na Baba pia hufa baada ya kurutubisha jike, kifo chake huwa taratibu pia, na hapo ndipo Sayansi imeendelea kuona ni maajabu ya viumbe hawa.

Kikawaida utafiti wa kisayansi ulijaribu kuchunguza kujiridhisha wa nini pia na Baba Pweza hufa kwa kuzaa mara moja.
Je na k**a Baba hufa haimaanishi basi wanaweza kufa madume wengi k**a walishiriki kurutubisha jike mmoja.!?

Nitakuja kulieleza hilo siku nyingine, hii ni utangulizi wa kukuandaa katika mfululizo wa makala ya "Akili ya Mama Mtu".
Writer Cekam.

Address

Mikocheni Dar Es Salam
Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when 2skys TV posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to 2skys TV:

Videos

Share

Category


Other TV Channels in Dar es Salaam

Show All