SMILE FM TZ

SMILE FM TZ Radio � Broadcasts, Advertisements production,Events plan

Wananchi, Young Africans Sc wamefufua matumaini ya kufuzu robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika kufuatia ushindi wa 3-...
04/01/2025

Wananchi, Young Africans Sc wamefufua matumaini ya kufuzu robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika kufuatia ushindi wa 3-1 dhidi ya Kunguru wa Lubumbashi, TP Mazembe katika dimba la Benjamin Mkapa.

Wawakilishi hao wa Tanzania kwenye CAFCL wamefikisha pointi nne baada ya mechi nne na kukwea mpaka nafasi ya tatu kwenye Kundi A wakiwa pointi sawa na MC Alger waliopo nafasi ya pili.

FT: Yanga Sc 🇹🇿 3-1 🇨🇩 TP Mazembe
⚽ 32' Mzize
⚽ 56' Aziz Ki
⚽ 60' Mzize
⚽ 15' Faty (P)

MSIMAMO KUNDI A
1. 🇸🇩 Al Hilal—mechi 3—pointi 9
2. 🇩🇿 MC Alger —mechi 3—pointi 4
3. 🇹🇿 Yanga Sc—mechi 4—pointi 4
4. 🇨🇩 TP Mazembe—mechi 4—pointi 2

🚨 Klabu ya Arsenal iko tayari kumsajili mshambuliaji wa Man United Marcus Rashford ila klabu ya Arsenal hawako tayari ku...
04/01/2025

🚨 Klabu ya Arsenal iko tayari kumsajili mshambuliaji wa Man United Marcus Rashford ila klabu ya Arsenal hawako tayari kutoa ada ya Usajili zaidi ya £25m , 🏴󠁧󠁢󠁥󠁮󠁧󠁿

Source TransferdotCom

Leo imetimia miaka mitatu ya Semaji Ahmed Ally k**a Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Simba SC.Una neno kwakeJambo gani...
03/01/2025

Leo imetimia miaka mitatu ya Semaji Ahmed Ally k**a Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Simba SC.

Una neno kwake

Jambo gani linakuvutia zaidi katika utendaji wake wa kazi?

  FEI NA SIMBA NGOMA NGUMU..!!KIUNGO wa Azam FC, Feisal Salum amekata mzizi fitna kuhusu maneno yanayoendelea kusemwa kw...
03/01/2025



FEI NA SIMBA NGOMA NGUMU..!!

KIUNGO wa Azam FC, Feisal Salum amekata mzizi fitna kuhusu maneno yanayoendelea kusemwa kwamba huenda akatimikia Simba, akifunguka kuwa k**a ataondoka anapocheza sasa basi hawezi kujiunga na timu yoyote Bongo.

Fei alisema kuwa, endapo ataondoka Azam hawezi kujiunga na timu yoyote ya ndani kwa sasa ikiwamo Simba ambayo inatajwa sana kuwa atatimkia huko wakati wowote.

Alisema kuwa, akili yake kwa sasa ni kutafuta timu ya kwenda kucheza njeya nchi ili akaongeze kipaji chake na sio ndani kwani tayari ameshafanikiwa kujijenga katika ligi ya nyumbani.

wewe k**a mwanaume utajuaje k**a pisi kali yako imekubali show yako ni ishara gani utaziona
03/01/2025

wewe k**a mwanaume utajuaje k**a pisi kali yako imekubali show yako ni ishara gani utaziona

03/01/2025

Emmanuel Senzighe Project Manager wa Mradi wa Kilimo Tech Acceletor kutoka Sahara Ventures ni shirika linaloshiriki project mbalimbali za vijana katika Ubunifu na Ujasiriamali wa Teknolojia za kisasa.

.

03/01/2025

Umetulia endelea kusikiliza 95.3 Smile Fm mkoa wa manyara.........

Mitaa yote

Unatusikiliza kutoka kipande gani wanetu...........🔥▶🔥
03/01/2025

Unatusikiliza kutoka kipande gani wanetu...........🔥▶🔥

Menejimenti na Wafanyakazi wa SMILE FM 95.3 Babati Mkoa wa Manyara Tunakushukuru kwa kutusikiliza na Kutufuatilia kwenye...
31/12/2024

Menejimenti na Wafanyakazi wa SMILE FM 95.3 Babati Mkoa wa Manyara Tunakushukuru kwa kutusikiliza na Kutufuatilia kwenye Mitandao Yetu ya Kijamii yote Facebook, Instagram,Youtube, TikTok,Mwaka mzima wa 2024.Umekuwa ni msikilizaji mwema kwetu ukifuatilia vipindi vyetu mbalimbali Katika Radio hata kwenye Kurasa zetu za Kijamii Tunakuahidi kuendelea kukuletea maudhui bora mbalimbali ya kukujenga,kukuelimisha na kukuburudisha.

TUNAKUTAKIA HERI YA SIKUKUU NJEMA YA MWAKA MPYA 2025 SMILE FM
#2025 🔥🔥🇹🇿🇹🇿🇹🇿💪🏿💪🏿💪🏿💪🏿

Happy New Month January 1,2025   ya mwezi Mpya na mwaka mpya 2025.   #2025
31/12/2024

Happy New Month January 1,2025 ya mwezi Mpya na mwaka mpya 2025.

#2025

Ebu Tuambie Mwaka Mpya Umekukuta Ukiwa wapi? kuwa mkweli ulikuwa wapi?
31/12/2024

Ebu Tuambie Mwaka Mpya Umekukuta Ukiwa wapi? kuwa mkweli ulikuwa wapi?

Picha ya Pamoja na Emmanuel Senzighe (Mwenye shati jeupe) Project Manager wa Mradi wa Kilimo Teck acceletor kutoka Sahar...
30/12/2024

Picha ya Pamoja na Emmanuel Senzighe (Mwenye shati jeupe) Project Manager wa Mradi wa Kilimo Teck acceletor kutoka Sahara Ventures akiwa na watumishi wenzake Katika mradi huo mara Baada ya kumaliza kufanya kipindi maalumu Katika studio za Radio ya Smile Fm.

Hakika Mungu Humpenda mtu mwenye Subra yaani mtu mwenye (kusubili)  kuamini kupata au kukosa Sio kwa kupenda yeye bali n...
27/12/2024

Hakika Mungu Humpenda mtu mwenye Subra yaani mtu mwenye (kusubili) kuamini kupata au kukosa Sio kwa kupenda yeye bali ni mungu ndiyo mpangaji wa yote (kadal) na pia Humpenda mtu mwenye kupendelea kuwakumbusha wenzake kufanya matendo mema yenye kumpendeza mungu

Smile Fm Tunakutakia Ijumaa Kareem wewe na Familia yako

Disemba 26 ya kila mwaka duniani kote wakristo huitumia siku hii k**a siku ya kufungua zawadi na kutoa chochote kwa wape...
26/12/2024

Disemba 26 ya kila mwaka duniani kote wakristo huitumia siku hii k**a siku ya kufungua zawadi na kutoa chochote kwa wapendwa wao.

Smile Fm Tunakupa zawadi ya Boxing fleva day wewe msikilizaji wetu kwa kupata zawadi ya kusikiliza Muziki mchanganyiko

Je umepata zawadi? ya BOXING DAY?

25/12/2024

TUKIO KUBWA LA BURUDANI KWA MWAKA 2024 BABATI MANYARA.

Novemba 7.2024 ilikuwa ni Siku kubwa ya Ki historia kwa wapenda Burudani ya Muziki Babati mkoani manyara kwani ilikuwa ni nafasi ya ku enjoy burudani,live performance Pamoja na kupata picha na mastaa mbalimbali waliowahi kufanya vizuri miaka ya nyuma kuanzia miaka ya 2000.

Ugeni huo wa list ya zaidi ya wasanii 10 walifika kwenye studio za radio ya Smile Fm kwa ajili ya mahojiano mafupi na kuzungumza na mashabiki zao kupitia masafa ya 95.3.

ilikuwa ni Legends Tour ambayo imeacha kumbukumbu nzuri kutoka kwa mashabiki na wapenzi wa muziki wa zamani ilifanyika Babati katika uwanja wa Mpira wa Tanzanite Kwaraa huku steji ikishambuliwa na wakali kibao k**a
















na wengine kibao

🔥 Novemba 7 pale Tanzanite Kwaraa ilitisha zaidi Kwa udhamini wa kupitia kinywaji chake cha

Tuambie Tukio gani la Burudani lilikukosha zaidi mwaka 2024

Shangwe na Burudani inasikika kwenye Masafa ya 95.3 Kazi ni Moja tu kuongeza Sauti ya Radio yako Hadi Majirani waseme Ke...
25/12/2024

Shangwe na Burudani inasikika kwenye Masafa ya 95.3 Kazi ni Moja tu kuongeza Sauti ya Radio yako Hadi Majirani waseme Kelele Kelele!!

TUNAKUPAWEWE

Smile Fm inakutakia shangwe na furaha Katika siku muhimu Leo ya  Krismasi 🎄 iwe yenye furaha na amani kwako na familia Y...
25/12/2024

Smile Fm inakutakia shangwe na furaha Katika siku muhimu Leo ya Krismasi 🎄 iwe yenye furaha na amani kwako na familia Yako ..

Mkuu wa mkoa wa Manyara  ameeleza kuwa hakuna sababu yoyote itakayozuia kukosa huduma ya madarasa kwa wanafunzi waliofau...
23/12/2024

Mkuu wa mkoa wa Manyara ameeleza kuwa hakuna sababu yoyote itakayozuia kukosa huduma ya madarasa kwa wanafunzi waliofaulu kujiunga na kidato cha kwanza mwaka 2025.

Ameeleza hayo wakati akitoa ripoti ya tathmini juu ya miradi mbalimbali kwa waandishi wa habari ofisini kwake, ambapo idara ya elimu imewekewa mikakati bora kwa mwaka 2024/25.

Hata hivyo Sendiga ametaja moja ya jukumu kuu la serikali ni kutoa kipaumbele katika sekta ya elimu kila ifikapo januari kwa sababu za uandikishaji wa wanafunzi wa awali na wale ambao wataanza darasa la kwanza.

Mkoa wa manyara unatarajia kuandikisha watoto zaidi ya elfu 66 kwa elimu ya awali na watoto wa darasa la kwanza zaidi ya elfu 59,ambapo kwa pamoja wataanza masomo ifikapo januari 13 mwaka 2025.

Aidha Queen ameongeza serikali inaendelea kutekeleleza miradi mbali mbali ya elimu,ambapo wamepokea takribani bilioni 33 kwa ajili ya kuboresha miundo mbinu katika idara hiyo,pia ameomba wazazi na walezi kushirikiana na walimu kupanga namna bora ya upatikanaji wa lishe kwa wanafunzi watakapokuwa wakiendelea na masomo.

Pamoja na hayo Sendiga Amekamilisha hotuba yake kwa kumshukuru rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania ,Samia Suluhu,wananchi wa mkoa huo, viongozi wenzake katika serikali kwa ushirikiano na upendo walionesha kwa kipindi cha mwaka 2024 na kusisitiza wazazi kuwa makini kwa watoto katika kusherehekea sikukuu za mwishoni mwa mwaka akiongeza mkoa ni salama kwa watu wote.

Address

Negamsi
Babati
255

Opening Hours

Monday 05:00 - 00:00
Tuesday 05:00 - 00:00
Wednesday 05:00 - 00:00
Thursday 05:00 - 00:00
Friday 05:00 - 00:00
Saturday 05:00 - 00:00
Sunday 05:00 - 00:00

Telephone

+255684728971

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when SMILE FM TZ posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to SMILE FM TZ:

Videos

Share

Category