RAIS SAMIA KUWA MGENI RASMI MAADHIMISHO SIKU YA WANAWAKE KITAIFA JIJINI ARUSHA.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kuwa Mgeni rasmi kwenye maadhimisho ya siku ya wanawake duniani ambapo Kitaifa maadhimisho yanatarajiwa kufanyika Jijini Arusha, tarehe nane mwezi Machi 2025.
Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Paul Christian Makonda amebainisha hayo leo Ijumaa Januari 24, 2025 wakati akizungumza na wanahabari Ofisini kwake Jijini Arusha, akisema maadhimisho hayo yataambatana na shughuli mbalimbali kwa siku nne mfululizo, ikiwemo maonesho ya kibiashara, Michezo mbalimbali kwa wanawake pamoja na burudani zikazoambatana na nyama Choma za Ng'ombe zaidi ya mia tano.
Ametumia fursa hiyo pia kuwataka wanawake wa Mkoa wa Arusha kuchangamkia fursa mbalimbali zitakazoambatana na maadhimisho hayo, akiwaalika wanawake kufika kwenye Ofisi za Wakuu wa Wilaya kwaajili ya kuwasilisha mawazo yao mbalimbali yatakayowasaidia kuweza kunufaika na Uenyeji wa Arusha kwenye maadhimisho hayo ya siku ya wanawake Kitaifa.
Mhe. Makonda amesema tayari Mkoa umeanza maandalizi ya Maadhimisho hayo, akiisihi jamii ya Mkoa wa Arusha kwa maana ya mtu mmoja mmoja pia kujiandaa, kwani kutakuwa na utoaji wa zawadi maalum kwa wanawake/ akinamama, zawadi ambazo zitatolewa na Watu mbalimbali kwa Wazazi wao kama sehemu ya shukrani kwa malezi.
VIDEO Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba amesifu utendaji kazi wa Mkuu wa Mkoa wa Arusha Paul Makonda na kusema kuwa ameumudu Mkoa vizuri na kurejesha hadhi ya Jiji hilo.———————————————————————————————— “Wewe ume-fit kila kazi ukipewa huwa una-fit, nilimwambia wakati ule uko mwenezi nikamwambia umetenda haki nafasi hiyo kwasababu Mwenezi wa Chama hapaswi kutambulishwa anapopita mtaani anapaswa kutambuliwa kuwa yule pale anapita, Chama kubwa kama CCM Mwenezi wake hatakiwi kuzidiwa umaarufu na Aziz Ki" - Dr. Mwigulu.
MKUU WA MKOA WA ARUSHA MHE. PAUL MAKONDA AMPIGA SPANA MBUNGE WA ARUSHA MJINI MRISHO GAMBO MBELE YA WATU “SIPENDI,UMAARUFU WA KIJINGA UNACHOMEKEA VIONGOZI”
Siku 3 za funga mwaka Arusha, mambo yalikuwa 🔥🔥🔥
Wanaarusha wapokea mwaka 2025 kimataifa
Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ametoa zawadi kwa vituo vitatu vya watu wenye mahitaji maalum mkoa wa Arusha ikiwa kuwatakiwa kheri ya mwaka mpya wa 2025.
NABII MWAMPOSA AVUTIWA NA MAOMBI YA DEC.9, AALIKA WANANCHI KUSHIRIKI KIKAMILIFU.
Mchungaji na Nabii wa kanisa la Arise and Shine nchini Tanzania Apostle Boniface Mwamposa ametoa rai kwa wananchi wote wa Arusha kujitokeza kwa wingi leo Jumatatu Disemba 09, 2024 kwenye maombi maalum ya kuuombea Mkoa wa Arusha ikiwa ni utekelezaji wa mpango wa Mkuu wa Mkoa Mhe. Paul Christian Makonda.
Kwenye sehemu ya mahubiri yake jana Jumapili Disemba 08, 2024, Nabii Mwamposa ameitaja siku ya leo kama siku ya kukombolewa kiroho, akimpongeza Mhe. Makonda kwa maono yake hayo ya kuikomboa ardhi ya Arusha, akitamani pia kushiriki na wakazi wa Arusha katika maombezi hayo.
Leo Jumatatu wakati wa kuadhimisha miaka 63 ya uhuru wa Tanzania bara, Mkoani Arusha kunafanyika matembezi na maombi maalum ya kuombea Mkoa wa Arusha kuanzia saa mbili kamili asubuhi, matembezi yakianzia kwenye mzunguko wa barabara ya Impala na kumalizikia kwenye mzunguko wa mnara wa Mwenge Jijini Arusha.
NABII MKUU MHE. DK. GeorDavie Royal Mkuu AMTABIRIA Mkuu wa Mkoa wa Arusha #Paul_Makonda KUENDELEA KULA MEMA YA NCHI NA "SIKU MOJA UTANIKUMBUKA"