Paul Makonda Yupo Kazini

Paul Makonda Yupo Kazini MAHALI SAHIHI KWA WOTE WANAOUNGA MKONO KAZI ZA MKUU WA MKOA WA ARUSHA MHE. PAUL MAKONDA🫶

27/01/2025

RAIS SAMIA KUWA MGENI RASMI MAADHIMISHO SIKU YA WANAWAKE KITAIFA JIJINI ARUSHA.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kuwa Mgeni rasmi kwenye maadhimisho ya siku ya wanawake duniani ambapo Kitaifa maadhimisho yanatarajiwa kufanyika Jijini Arusha, tarehe nane mwezi Machi 2025.

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Paul Christian Makonda amebainisha hayo leo Ijumaa Januari 24, 2025 wakati akizungumza na wanahabari Ofisini kwake Jijini Arusha, akisema maadhimisho hayo yataambatana na shughuli mbalimbali kwa siku nne mfululizo, ikiwemo maonesho ya kibiashara, Michezo mbalimbali kwa wanawake pamoja na burudani zikazoambatana na nyama Choma za Ng'ombe zaidi ya mia tano.

Ametumia fursa hiyo pia kuwataka wanawake wa Mkoa wa Arusha kuchangamkia fursa mbalimbali zitakazoambatana na maadhimisho hayo, akiwaalika wanawake kufika kwenye Ofisi za Wakuu wa Wilaya kwaajili ya kuwasilisha mawazo yao mbalimbali yatakayowasaidia kuweza kunufaika na Uenyeji wa Arusha kwenye maadhimisho hayo ya siku ya wanawake Kitaifa.

Mhe. Makonda amesema tayari Mkoa umeanza maandalizi ya Maadhimisho hayo, akiisihi jamii ya Mkoa wa Arusha kwa maana ya mtu mmoja mmoja pia kujiandaa, kwani kutakuwa na utoaji wa zawadi maalum kwa wanawake/ akinamama, zawadi ambazo zitatolewa na Watu mbalimbali kwa Wazazi wao k**a sehemu ya shukrani kwa malezi.

24/01/2025
LEOPARD TOURS WATOA PIKIPIKI 20 KWA POLISI ARUSHA, KUFADHILI MATIBABU KWA WASIOJIWEZAMtendaji Mkuu wa Leopard Foundation...
24/01/2025

LEOPARD TOURS WATOA PIKIPIKI 20 KWA POLISI ARUSHA, KUFADHILI MATIBABU KWA WASIOJIWEZA

Mtendaji Mkuu wa Leopard Foundation inayomilikiwa na Kampuni Mama ya Leopard Tour inayojishughulisha na masuala ya Utalii Mkoani Arusha, Ndugu Zuher Fazal leo Ijumaa Januari 24, 2025 kwaniaba ya Taasisi hiyo, amekabidhi Pikipiki 20 kwa Jeshi la Polisi Mkoani Arusha katika jitihada za kusaidia kuimarisha ulinzi na usalama Mkoani Arusha.

Wakati wa makabidhiano hayo kwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Paul Christian Makonda, Ndugu Fazal amemshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa usimamizi wake mzuri wa sekta ya utalii nchini, akisema kuimarika kwa Sekta hiyo pamoja na mafanikio makubwa yanayopatikana chini ya Serikali ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, ndicho kilichowahamasisha kujitoa kuchangia Vitendetakazi hivyo kwa Jeshi la Polisi.

Kwa Upande wake Mhe. Makonda,licha ya kuishukuru Leopard Foundation, ameahidi kuendelea kutengeneza mazingira mazuri kwa wafanyabiashara wa Mkoa wa Arusha kwaniaba ya Mhe. Rais Samia ili wafanyabiashara hao waendelee kuwa chachu ya maendeleo ya uchumi wa Mkoa wa Arusha kupitia fursa mbalimbali za ajira wanazozizalisha pamoja na mchango wao wanaourudisha kwenye Jamii.

Leopard Foundation inayotoa usaidizi wa Kijamii katika mapambano dhidi ya umaskini pamoja na kusaidia katika elimu, usimamizi wa mazingira na afya, imeingia makubaliano pia na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha katika kusaidia huduma za matibabu kwa wahitaji wasiojiweza kiuchumi wanaofika Ofisini kwa Mkuu wa Mkoa kwaajili ya matibabu.

BILIONI 14.4 KULIPWA FIDIA, UTEKELEZAJI MRADI WA MAGADI SODA WILAYANI MONDULI.Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk...
23/01/2025

BILIONI 14.4 KULIPWA FIDIA, UTEKELEZAJI MRADI WA MAGADI SODA WILAYANI MONDULI.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan ameridhia kutoa Jumla ya Shilingi Bilioni 14.4 k**a fidia kwa Wakazi wa Vijiji vinne vilivyopo kwenye Kata ya Engaruka Wilayani Monduli Mkoani Arusha ikiwa ni muendelezo wa mkakati wa Serikali ya awamu ya sita katika uendelezaji wa miradi ya Kimkakati yenye tija kwa Taifa.

Kwaniaba ya Rais Samia leo Alhamisi Januari 23, 2025, Waziri wa Viwanda na biashara Mhe. Dkt. Seleman Jaffo wakati akizindua ugawaji wa fidia hizo kwa awamu ya kwanza yenye takribani Bilioni 6.2, amewataka wasimamizi wa zoezi hilo kuhakikisha kuwa ulipaji wa fidia hizo unamalizika kabla ya Februari 15, 2025, na kuaigiza shirika la Taifa la Maendeleo (NDC) kushughulikia malalamiko yote ya ya fidia kwa wananchi wa eneo hilo.

Katika hatua nyingine Waziri Jafo aliyeambatana na Viongozi mbalimbali akiwemo Naibu Waziri wa Wizara ya ardhi Mhe. Jofrey Pinda, amesema serikali imeweka mpango maalum wa kuhakikisha kuwa eneo la Engaruka linakuwa na barabara zinazopitika muda wote sambamba na upatikanaji wa umeme mkubwa wa Kilowati 33 ili kusaidia katika shughuli za uendeshaji wa viwanda viwili vikubwa vinavyotarajiwa kutekeleza mradi huo.

Akizungumza katika Uzinduzi huo, Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Paul Makonda, amesema Arusha ni miongoni mwa mikoa yenye bahati na kadri siku zinavyosonga, Mkoa huu utatoa fursa mbalimbali za maendeleo kwenye sekta za Kilimo, Madini na Michezo, zitakazosaidia wananchi kujikwamua na umaskini akihimiza kuendelea kupewa kipaumbele cha ajira kwa wazawa wakati wa utekelezaji wa miradi mbalimbali inayotekelezwa kwenye Mkoa wa Arusha.

Akisoma taarifa ya utekelezaji wa mradi huo wa Kimkakati, Mkurugenzi mwendeshaji wa NDC Dkt.Nicolaus Shombe amesema mradi huo wa magadi soda umechukua zaidi ya miaka 29 tangu mchakato wake ulipoanza baada ya NDC kufanya utafiti wake na kubaini uwepo wa magadisoda yenye kufikia mita za ujazo Bilioni 3.8 sawa

Waziri wa Viwanda na Biashara Dkt. Selemani Jafo akiwasili kwenye uzinduzi wa zoezi la ulipaji fidia katika mradi wa mag...
23/01/2025

Waziri wa Viwanda na Biashara Dkt. Selemani Jafo akiwasili kwenye uzinduzi wa zoezi la ulipaji fidia katika mradi wa magadi soda, hafla hiyo inayofanyika leo Januari 23, 2025 eneo Engaruka Monduli mkoani Arusha.

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mhe. Paul Christian Makonda ameshiriki mazishi ya Baba mzazi wa Mtangazaji wa Jahazi HD , marehe...
23/01/2025

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mhe. Paul Christian Makonda ameshiriki mazishi ya Baba mzazi wa Mtangazaji wa Jahazi HD , marehemu Burhani Mandi aliyefariki January 20, 2025 Jijini Dar es Salaam na kuzikwa Leo katika makaburi ya Njiro Jijini Arusha.

MKURUGENZI WA UN WOMEN NA RC MAKONDA, WAJADILI USHIRIKIANO KATIKA MASUALA YA KIJINSIAMkurugenzi wa Nchi wa shirika la Um...
22/01/2025

MKURUGENZI WA UN WOMEN NA RC MAKONDA, WAJADILI USHIRIKIANO KATIKA MASUALA YA KIJINSIA

Mkurugenzi wa Nchi wa shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia masuala ya wanawake (UN Women), Hodan Addou, amefanya ziara Mkoani Arusha ambapo amekutana na Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mhe. Paul Christian Makonda, kujadili masuala muhimu yanayohusu usawa wa kijinsia na uwezeshaji wa wanawake katika masuala ya kiuchumi.

Katika mazungumzo yao yaliyofanyika Ofisini kwa Mkuu wa Mkoa huo leo tarehe 22 Januari, 2024, Mhe. Makonda amesema kuwa, Mkoa wa Arusha umekuwa ukiendesha shughuli za kuwawezesha wanawake kiuchumi sambamba na kuzuia masuala ya ukatili wa Kijinsia kwa wanawake na Watoto na uhamasishaji wa wanawake kushiriki katika masuala ya Uongozi wa ngazi mbalimbali.

Mhe. Makonda ameongeza kuwa, Kupitia Mradi wa UN WOMEN ujulikanao k**a WLER “Strengthening Women And Girls’ Meaningful Participation, Leadership, And Economic Rights”. Ulionufaisha Halmashauri tatu (3) za Mkoa wa Arusha wanawake wamekuwa wakipatiwa elimu kuhusu masuala ya kiuchumi na kutojihusisha na mikopo umiza badala yake kutumia fursa ya Mikopo isiyo na riba ya 10% inayotolewa kwenye Halmashauri zote Nchini.

“Tuna dhamira ya kuhakikisha kuwa wanawake na wasichana wa Arusha wanapewa nafasi za kiuchumi, kijamii, na elimu. Tunaamini kuwa kwa kushirikiana na UN Women, tunaweza kufanya mabadiliko makubwa,” amesema Mhe. Makonda.

Kwa upande wake Mkurugenzi Hodan Addou amesema kuwa UN Women imekuwa ikifanya kazi kwa karibu na Serikali katika kuhakikisha kuwa wanawake wanapata nafasi sawa katika sekta zote za maendeleo na kusisitiza umuhimu wa kushirikiana katika mipango ya maendeleo jumuishi inayozingatia mahitaji ya wanawake vijijini na wale walioko katika mazingira magumu.

“Uwezeshaji wa wanawake si tu suala la haki za binadamu bali ni msingi wa maendeleo endelevu na tunafurahi kuona Mkoa wa Arusha ukichukua hatua madhubuti katika kusimamia usawa wa kijinsia,” amesema Bi. Addou.

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Paul Makonda Ndani ya Mkutano Mkuu Maalum wa Chama cha Mapinduzi CCM Taifa, unaofanyika kati...
19/01/2025

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Paul Makonda Ndani ya Mkutano Mkuu Maalum wa Chama cha Mapinduzi CCM Taifa, unaofanyika katika Ukumbi wa Jakaya Kikwete Convection Centre Dodoma.

ARUSHA MBIONI KUFANYWA KUWA KITOVU CHA UTALII WA MATIBABU UKANDA WA AFRIKA MASHARIKI.Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Paul Ch...
11/01/2025

ARUSHA MBIONI KUFANYWA KUWA KITOVU CHA UTALII WA MATIBABU UKANDA WA AFRIKA MASHARIKI.

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Paul Christian Makonda na Waziri wa Afya nchini Tanzania Mhe. Jenista Mhagama, wamekubaliana kukutana Dodoma Makao Makuu ya Wizara hiyo, kufanya mazungumzo ya pamoja ya kupanga utekelezaji wa ndoto na Maono ya Mhe. Makonda ya kuufanya Mkoa wa Arusha kuwa Kitovu cha Utalii wa Matibabu kwa Ukanda wa Afrika ya Mashariki.

Wakati wa Mazungumzo yao Makao makuu ya Mkoa Jijini Arusha, Mhe. Makonda amemueleza Waziri Mhagama kuwa Mkoa unatekeleza kwa kasi agizo la Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan la kukuza utalii wa aina mbalimbali Mkoani hapa, akisema kupatikana kwa Hospitali itakayokuwa na Huduma za kibingwa na Kibobezi sambamba na madaktari bingwa kutoka ndani na nje ya nchi, kutasaidia kuwavuta watu wanaoizunguka Tanzania na Raia wa kigeni kusafiri kufuata matibabu hayo Mkoani Arusha na hivyo kukuza utalii na kusisimua pato la Mkoa wa Arusha.

Waziri Mhagama, Kando ya Kumshukuru Mhe. Makonda kwa kusimamia vyema utoaji huduma za kiafya Mkoani Arusha ikiwemo Programu ya Kliniki yake ya afya iliyofanyika mwaka 2024, amemuahidi kuwa atamuita Jijini Dodoma, kujadiliana pamoja Mkakati madhubuti wa kutekeleza maono ya kujenga Hospitali mpya ya kibingwa ama kuiongezea uwezo Hospitali ya Mkoa ya Mount Meru ili kukidhi viwango vinavyohitajika Kimataifa.

Aidha wawili hao Katika mazungumzo yao leo Januari 10, 2025, wamekubaliana kuendelea kushirikiana katika kutimiza dhamira ya Rais Samia katika kuwapatia wananchi huduma bora za kiafya, ambapo Waziri Mhagama amesema Wizara yake pia ipo mbioni kuupatia Mkoa wa Arusha mashine mpya ya MRI k**a sehemu ya maboresho ya utoaji wa huduma za kiafya Mkoani hapa na kuondokana na changamoto ya ukosefu wa mashine hiyo muhimu kwa matibabu mbalimbali.

RC MAKONDA AKUTANA NA WAZIRI MBARAWA, RELI YA KASKAZINI KUBORESHWA ILI KUIMARISHA UTALII.Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Pau...
10/01/2025

RC MAKONDA AKUTANA NA WAZIRI MBARAWA, RELI YA KASKAZINI KUBORESHWA ILI KUIMARISHA UTALII.

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Paul Christian Makonda leo Jumatano Januari 08, 2024 amekutana na kuzungumza na Waziri wa Uchukuzi, Mhe. Prof. Makame Mnyaa Mbarawa ambapo Waziri Mbarawa ameridhia ombi la Mhe. Makonda la kuboresha reli ya Kaskazini (Tanga-Arusha) katika kuboresha huduma za Utalii Mkoani Arusha kwa kupunguza foleni.

Katika mazungumzo yao, Mhe. Makonda mbali ya kusema kuwa sekta ya uchukuzi ni muhimu kwenye kukuza na kuimarisha utalii Mkoani Arusha, amesema kuboreshwa reli hiyo pamoja na kujengwa kwa bandari kavu Mkoani Arusha kutaondoa wingi wa malori ya mizigo barabarani pamoja na kusaidia katika matunzo ya barabara katika kuzisaidia kudumu muda mrefu zaidi.

Kulingana na Mhe. Mbarawa, Arusha ni Mkoa muhimu kwa Utalii na uchukuzi ukiwa wa tatu kwa miruko ya ndege nchini Tanzania, akiahidi kuendelea kushirikiana na serikali ya Mkoa katika kufanikisha utekelezaji wa ilani ya Chama Cha Mapinduzi CCM ikiwemo kusimamia maboresho ya uwanja wa ndege wa Arusha, unaotarajiwa kuanza kufungwa taa hivi karibuni ambapo Serikali ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan tayari imeshatenga Bilioni 11 za kufunga taa kwenye uwanja huo wa ndege Arusha.

ARUSHA KUWA MWENYEJI WA MKUTANO WA KIMATAIFA WA 73 WA SEKTA YA ANGA DUNIANI.Mkoa wa Arusha utakuwa mwenyeji wa Mkutano m...
10/01/2025

ARUSHA KUWA MWENYEJI WA MKUTANO WA KIMATAIFA WA 73 WA SEKTA YA ANGA DUNIANI.

Mkoa wa Arusha utakuwa mwenyeji wa Mkutano mkubwa wa 73 wa Baraza la Kimataifa la viwanja vya ndege kwa Kanda ya Afrika utakaowakutanisha Wataalamu mbalimbali kutoka kwenye mashirika ya ndege, Makampuni na taasisi za Kimataifa za usafiri wa anga zaidi ya 400, ukitarajiwa kufanyika kwa siku saba kuanzia Aprili 24- 30, 2025.

Waziri wa Uchukuzi Prof. Makame Mbarawa Kwenye ukumbi wa Mikutano uwanja wa ndege Arusha wakati akizungumza na wanahabari leo Januari 08, 2025, amesema maandalizi ya mkutano huo yanakwenda vizuri, akiushukuru Uongozi wa Mkoa wa Arusha chini ya Mhe. Paul Christian Makonda kwa ushirikiano wao, akiwasihi wakazi wa Arusha kutumia ujio wa wajumbe wa mkutano huo kujipatia kipato na kujinufaisha Kiuchumi.

Kwa upande wake Mhe. Paul Christian Makonda aliyeambatana na Mhe. Mbarawa, ameshukuru Serikali ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan na wizara hiyo kwa Kuiteua Arusha kuwa mwenyeji wa mkutano huo wa kimataifa, akiahidi usalama wa kutosha pamoja na huduma nzuri kwenye maeneo ya malazi na kumbi za mikutano kwa wageni wote kwa siku zote saba za kufanyika Mkutano huo.

Kulingana na ratiba iliyotolewa na Waziri Mbarawa, Wajumbe hao zaidi ya mia nne, kwenye siku zao saba za kuwa Mkoani Arusha wametenga siku moja kwaajili ya kutembelea maeneo mbalimbali ya vivutio vya Utalii Mkoani Arusha suala ambalo linatajwa na Mhe. Makonda kwamba litakuwa sehemu nyingine ya kusisimua uchumi wa Mkoa wa Arusha kupitia sekta ya Utalii na sekta nyingine mtambuka za vyakula, usafiri, sehemu za starehe, hoteli na nyumba za kulala wageni.

RC MAKONDA ATAKA KASI ZAIDI MRADI WA UJENZI JENGO LA UTAWALA JIJI LA ARUSHA.Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Paul Christian M...
10/01/2025

RC MAKONDA ATAKA KASI ZAIDI MRADI WA UJENZI JENGO LA UTAWALA JIJI LA ARUSHA.

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Paul Christian Makonda leo Alhamisi Januari 09, 2025, amekagua maendeleo ya Ujenzi wa Jengo la Utawala la Halmashauri ya Jiji la Arusha na kuagiza mkandarasi anayesimamia Ujenzi huo kwa awamu ya pili (Phase 2) kuhakikisha kuwa anakamilisha kazi yake mwezi Mei mwaka huu badala ya mwezi Julai iliyokuwa imepangwa awali.

Mhe. Makonda amefikia uamuzi huo baada ya kuelezwa kuwa mradi huo umekuwa ukisuasua bila sababu za msingi ilihali tayari Rais Samia Suluhu Hassan alikwisha idhinisha zaidi ya Bilioni 6 za ujenzi wa awamu ya pili ya Jengo hilo la Ghorofa sita, Akitaka pia taratibu za kimkataba na Ujenzi kwa awamu ya tatu kuanza kuandaliwa haraka badala ya kusubiri kukamilika kwa ujenzi awamu ya pili.

Katika Hatua nyingine Mhe. Makonda pia amesisitiza Halmashauri zote za Mkoa wa Arusha kutumia wenyeji wa Arusha na wenye sifa kwenye tenda mbalimbali ili kukuza pato la Mkoa pamoja na kuwataka Madiwani, Wataalamu na Viongozi wa Halmashauri zote za Mkoa wa Arusha kushik**ana na kuhakikisha kila wanachokifanya kinakuwa na matokeo chanya kwa Wananchi k**a sehemu ya Kumpa sifa na Shukrani Rais Samia Suluhu Hassan anayehakikisha mara zote kuwa serikali yake haiwi kikwazo kwa maendeleo na ustawi wa wananchi wake.

Kwa upande wake Mstahiki Meya wa Jiji la Arusha Mhe. Maximilian Iranghe na Mkuu wa wilaya hiyo Mhe. Felician Mtahengerwa, wamemshukuru Mhe. Makonda kwa namna anavyokuza uwajibikaji Mkoani Arusha, wakiahidi kushirikiana na Wataalamu na Watendaji wengine katika kusimamia kikamilifu maelekezo ya Mhe. Paul Christian Makonda ili kuhakikisha kuwa wananchi wananufaika na Ujenzi wa Jengo hilo haraka iwezekanavyo.

07/01/2025

VIDEO Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba amesifu utendaji kazi wa Mkuu wa Mkoa wa Arusha Paul Makonda na kusema kuwa ameumudu Mkoa vizuri na kurejesha hadhi ya Jiji hilo.———————————————————————————————— “Wewe ume-fit kila kazi ukipewa huwa una-fit, nilimwambia wakati ule uko mwenezi nikamwambia umetenda haki nafasi hiyo kwasababu Mwenezi wa Chama hapaswi kutambulishwa anapopita mtaani anapaswa kutambuliwa kuwa yule pale anapita, Chama kubwa k**a CCM Mwenezi wake hatakiwi kuzidiwa umaarufu na Aziz Ki" - Dr. Mwigulu.

06/01/2025

MKUU WA MKOA WA ARUSHA MHE. PAUL MAKONDA AMPIGA SPANA MBUNGE WA ARUSHA MJINI MRISHO GAMBO MBELE YA WATU “SIPENDI,UMAARUFU WA KIJINGA UNACHOMEKEA VIONGOZI”

RC MAKONDA AMTAKA GAMBO KUHUDHURIA VIKAO VYA HALMASHAURI NA VYA MKOA, KUTOENDEKEZA SIASA CHONGANISHI.Mkuu wa Mkoa wa Aru...
06/01/2025

RC MAKONDA AMTAKA GAMBO KUHUDHURIA VIKAO VYA HALMASHAURI NA VYA MKOA, KUTOENDEKEZA SIASA CHONGANISHI.

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Paul Christian Makonda Leo Jumatatu Januari 06, 2024 amemtaka Mbunge wa Arusha Mjini Mhe. Mrisho Mashaka Gambo, kuachana na siasa za uchonganisha na badala yake ahudhurie vikao vya Mipango ngazi ya Halmashauri na vya ngazi ya Mkoa ili kujadili pamoja kuhusu changamoto na suluhu za masuala mbalimbali yanayohusu Mkoa wa Arusha.

Mhe. Makonda akiambatana na Waziri wa ujenzi Mhe. Abdallah Ulega, ametoa kauli hiyo leo wakati wa Ukaguzi wa ujenzi wa barabara ya Mianzini- Olemringaringa inayojengwa kwa kiwango cha lami, akisema kutohudhuria vikao hivyo na badala yake kusubiri kuwasilisha changamoto zao kwa Viongozi wa kitaifa wanaofika mkoani hapa kwa ziara za kikazi ni uchonganishi usiokubalika na unaokwamisha shughuli za maendeleo.

Kulingana na Mhe. Makonda aliyeambatana na Waziri wa Ujenzi na Watendaji wakuu wa Wizara hiyo kwenye kukagua miradi mbalimbali ya Ujenzi Mkoani Arusha, amewaambia wananchi wa Ilboru, Arumeru kuwa masuala mbalimbali yanajadiliwa na kupatiwa ufumbuzi na maelekezo ndani ya Vikao mbalimbali vya mipango vinavyoitishwa ngazi ya Halmashauri na ngazi ya Mkoa na ni wajibu wa kila Kiongozi husika kuhudhuria ili kuwa na kauli ya pamoja na utekelezaji wa pamoja kwenye masuala ya maendeleo ndani ya Halamshauri na Mkoa wa Arusha kwa ujumla.

TANZANIA KUACHANA NA TAA ZA BARABARANI ZENYE KUTUMIA UMEME.Waziri wa Ujenzi Mhe. Abdallah Ulega Leo Jumatatu Januari 06,...
06/01/2025

TANZANIA KUACHANA NA TAA ZA BARABARANI ZENYE KUTUMIA UMEME.

Waziri wa Ujenzi Mhe. Abdallah Ulega Leo Jumatatu Januari 06, 2024 akiwa Jijini Arusha kwenye Kikao cha Bodi ya barabara Mkoa wa Arusha, Ameagiza mamlaka zote zinazohusika na ufungaji wa Taa za barabarani nchini Tanzania kuachana na mifumo ya taa zinazotumia umeme na badala yake zifungwe taa zinazotumia nishati ya Jua ili kuondokana na gharama kubwa za uendeshaji wa Taa hizo za barabarani.

Mhe. Ulega ametoa tamko hilo ikiwa ni utekelezaji wa ombi lililotolewa na Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Paul Christian Makonda aliyewasilisha kwa Waziri huyo pamoja na Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Nchemba akiomba usaidizi katika ufungaji wa taa za barabarani zinazotumia nishati jua, ili kuondokana na gharama kubwa za uendeshaji wa Taa zinazotumia umeme.

Katika utekelezaji wake, Waziri Ulega ameiagiza Wakala wa barabara Mjini na Vijijini TARURA pamoja na Wakala wa barabara Tanzania TANROAD kushirikiana pamoja kuhakikisha Jiji la Arusha linafungwa taa kwenye maeneo yote muhimu ili Jiji hilo liweze kuwa na hadhi ya kuvutia zaidi watalii na mikutano mbalimbali ya kitaifa na kimataifa pamoja na kuufanya Mkoa huo kuwa na hadhi ya kustahimili Ofisi nyingi za kidiplomasia zilizopo Jijini Arusha.

RC MAKONDA AWAKUTANISHA MAWAZIRI WA FEDHA NA UJENZI, BARABARA ZA ARUSHA KUPATIWA UFUMBUZI.Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwi...
06/01/2025

RC MAKONDA AWAKUTANISHA MAWAZIRI WA FEDHA NA UJENZI, BARABARA ZA ARUSHA KUPATIWA UFUMBUZI.

Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba na Waziri wa Ujenzi Mhe. Abdallah Ulega wamefika Mkoani Arusha mapema leo Januari 06, 2024 na kuhudhuria Kikao cha Bodi ya Barabara Mkoa wa Arusha ambapo wameahidi kutekeleza kikamilifu maombi ya Mkuu wa Mkoa Mhe. Paul Christian Makonda ya kuzijenga na kukarabati barabara za Mkoa wa Arusha ili kuchagiza uchumi wa Mkoa na kukuza sekta ya Utalii mkoani hapa.

Akiwakaribisha Mawaziri hao walioambatana na Watendaji wakuu wa Wizara zao akiwemo Katibu Mkuu wa Ujenzi Balozi Mhandisi Aisha Amour, Mhe. Makonda ameeleza kuhusu ubovu wa barabara za Arusha, akiwaomba Mawaziri hao kuharakisha ujenzi na maboresho yake kutokana na umuhimu wa barabara hizo katika kukuza uchumi na utalii wa Arusha pamoja na uthabiti kuelekea kwenye msimu wa michuano ya Kandanda ya barani Afrika (AFCON) inayotarajiwa kuchezwa Arusha, Dar Es salaam, Zanzibar kwa kushirikiana na nchi za Kenya na Uganda mnamo 2027.

Katika Maelezo yake Waziri Mwigulu ameahidi Wizara yake kuharakisha utoaji wa fedha za ujenzi na kuziweka baadhi ya barabara kwenye Bajeti ijayo ya serikali kuu huku Mhe. Ulega akiagiza kuanza mara moja kwa upembuzi wa baadhi ya barabara pamoja na kufungwa taa zinazotumia nishati jua, akisema serikali pia inatanua barabara kuu ya Bagamoyo- Arusha ili kuondoa msongamano kwa wageni na wenyeji wanaofika Arusha kutokea Uwanja wa ndege wa Kilimanjaro na wote wanaotumia barabara hiyo inayounganisha nchi za jirani pamoja na mikoa ya Kaskazini na Mashariki mwa Tanzania.

Address

Arusha

Telephone

+255788821721

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Paul Makonda Yupo Kazini posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Paul Makonda Yupo Kazini:

Videos

Share