Nesto Shayo

Nesto Shayo Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Nesto Shayo, Digital creator, .
(2)

▪︎High Rated Sports Contents Creator || Entertainment || Medical Personnel || Rombo Finest || Psychologist || 🇹🇿 || Dream ✈ to Etihad in Manchester England 🏴󠁧󠁢󠁥󠁮󠁧󠁿 ||

Kibu Denis Prosper ( ) mshambuliaji wa Simba Sc, amekuwa moto wakuotea mbali kwenye kampeni hizi za kimataifa kwenye Kom...
16/01/2025

Kibu Denis Prosper ( ) mshambuliaji wa Simba Sc, amekuwa moto wakuotea mbali kwenye kampeni hizi za kimataifa kwenye Kombe la Shirikisho Barani Afrika msimu wa mwaka 2024/25.

Licha ya wadau mbali mbali kuandika maneno ya kumnyooshea vidole kutokana na kiwango cha msimu uliopita, yeye ameamua kusimama katika ukweli na kuamini kile ambacho anakifanya, tena kwa ustadi wa juu.

Kibu msimu huu kwenye Kombe la Shirikisho amehusika pakubwa katika matokeo chanya ya Club hiyo kwani tangu kuanza kwa kampeni hizi tayari amesha cheka na Nyavu mara tatu. Akifunga goli moja kwenye hatua ya mtoano dhidi ya Al Ahli Tripol baadaye katika hatua ya makundi akifunga magoli mawili muhimu dhidi ya Cs Sfaxien Fc katika uwanja wa Benjamin Mkapa.

Yeye ndiye mchezaji wa Simba anayeonga kwa kupiga mashuti kuelekea Langoni, lakini pia ndiye mchezaji wa Simba anayeongoza kufanya mikimbio (dribbles).

ni Baller.

Rasmi usajili wa wachezaji hawa Said Ntibazonkiza na Luis Miquissone kwenda Kengold Fc umekufa baada ya Pande zote 2 kus...
16/01/2025

Rasmi usajili wa wachezaji hawa Said Ntibazonkiza na Luis Miquissone kwenda Kengold Fc umekufa baada ya Pande zote 2 kushindwana kufikia makubaliano.

Moja ya Sababu ni Matakwa ama mahitaji ya wachezaji kwenye Mkataba kwenda kwa Klabu na Nafasi ya Timu kwenye Msimamo ilipo imechangia kupeperusha Dili hizi za Mastar hawa.

Mishahara mikubwa na baadhi ya vipengele vigumu vya wachezaji hawa vimepelekea Dili hizi kuota mbawa klabu imewaambia haina uwezo wa kutimiza.

Ofisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe alisema beki wa kikosi hicho, Yao Kouassi Attohoula ataendelea kuwa nje ya uwanja baad...
16/01/2025

Ofisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe alisema beki wa kikosi hicho, Yao Kouassi Attohoula ataendelea kuwa nje ya uwanja baada ya kufanyiwa upasuaji huku Maxi Nzengeli ikielezwa anaendelea vizuri na ameshaanza mazoezi.

“Mchezaji wetu Yao hatakuwa sehemu ya kikosi baada ya kufanyiwa upasuaji. Yao atakuwa nje kwa kipindi kisichopungua wiki nne na kisichozidi wiki sita. Maxi anaendelea vizuri na maozezi, k**a mwalimu ataona utimamu wake wa kimwili unafaa kucheza mchezo ujao basi atamtumia lakini kimsingi kwa sasa yupo salama.”

Klabu ya Singida Black Stars imetangaza usajili wa mshambuliaji  wa kimataifa kutoka Ivory Coast Serge Pokou  akitokea A...
16/01/2025

Klabu ya Singida Black Stars imetangaza usajili wa mshambuliaji wa kimataifa kutoka Ivory Coast Serge Pokou akitokea Al Hilal ya Sudan.

Pokoe pia aliwahi kuitumikia Asec Mimosas ya Nchini kwao.

Club ya Young  Africans imetumia fedha nyingi saana kuipata saini ya Winga Jonathan Ikangalombo kutoka As Vita Club.Kwa ...
16/01/2025

Club ya Young Africans imetumia fedha nyingi saana kuipata saini ya Winga Jonathan Ikangalombo kutoka As Vita Club.

Kwa muujibu wa taarifa kutoka Kinshasa, Yanga imelipa kiasi cha $100,000 USD sawa na TSH 252 MILIONI.

Club ya Mc Alger kutoka Algeria tayari wamewasili Nchini Tanzania kwaajili ya mchezo wa mwisho wa Ligi ya Mabingwa  kati...
16/01/2025

Club ya Mc Alger kutoka Algeria tayari wamewasili Nchini Tanzania kwaajili ya mchezo wa mwisho wa Ligi ya Mabingwa katika hatua makundi dhidi ya Klabu Young Africans katika uwanja wa Benjamin Mkapa.

Mchezo huo utachezwa Jumamos hii 18/1/2025 mwendo wa saa 10:00PM (jioni).

Mchezo huo ndio ambao utaamua, hatma ya vilabu vyote viwili ninani ataingia ama atafuzu katika hatua ya Robo fainali.

Mwamuzi bora wa Tanzania msimu uliopita  Ahmed Arajiga na wenzake wanne  wmechaguliwa na Shirikisho la Kandanda Barani A...
16/01/2025

Mwamuzi bora wa Tanzania msimu uliopita Ahmed Arajiga na wenzake wanne wmechaguliwa na Shirikisho la Kandanda Barani Afrika (CAF), kusimamia mchezo wa Kombe la Shirikisho kati ya RS Berkane na Stellenbosch.

Nyota wa zamani wa Club ya Simba Peter Banda, ambaye hivi sasa anaitumikia Nyassa Big Bullets ya Nchini kwao Malawi amef...
15/01/2025

Nyota wa zamani wa Club ya Simba Peter Banda, ambaye hivi sasa anaitumikia Nyassa Big Bullets ya Nchini kwao Malawi amefanyiwa upasuaji kwenye bega la mkono wa kulia katika moja ya hospitali Nchini Kenya hii leo.

Mwamuzi kutoka nchini 🇲🇷Mauritania Patrice Milazar ndiye amepewa jukumu la kuiamua mechi ya mwisho ya hatua ya makundi k...
15/01/2025

Mwamuzi kutoka nchini 🇲🇷Mauritania Patrice Milazar ndiye amepewa jukumu la kuiamua mechi ya mwisho ya hatua ya makundi kati ya 🇹🇿Yanga dhidi ya 🇩🇿MC Algers.

Mchezo huo utapigwa Jumamosi hii na ni muhimu kwa timu zote mbili kwani Yanga itakuwa ikihitaji ushindi ili ifuzu hatua ya robo fainali huku MC Algers ikihitaji sare pekee.

Mchezaji wa kimataifa wa Tanzania Novatus Dismas Miroshi, anayekipiga katika Ligi kuu Nchini Uturuki (Super Liga) kunako...
15/01/2025

Mchezaji wa kimataifa wa Tanzania Novatus Dismas Miroshi, anayekipiga katika Ligi kuu Nchini Uturuki (Super Liga) kunako Klabu ya Göztepe anaendelea kufanya vizuri pamoja Klabu yake msimu huu.

Msimu huu, katika michezo 18, waliyochza Göztepe, tayari wamekusanya alama 31, wakiwa katika nafasi ya nne kwenye msimamo wa Ligi hiyo.

Miroshi amefanikiwa kucheza michezo 11 ya Super Liga akifunga magoli mawili, huku akitoa assist moja ya goli. Shine 🌟

Wakati Yanga inaanza maandalizi ya msimu huu Musonda alikuwa mmoja wa wachezaji waliochelewa kujiunga na timu, jambo amb...
14/01/2025

Wakati Yanga inaanza maandalizi ya msimu huu Musonda alikuwa mmoja wa wachezaji waliochelewa kujiunga na timu, jambo ambalo lilizua uvumi kwamba pengine ataachwa, lakini mwenyewe anafafanua.

“Hapana haikuwa hivyo labda niwaeleze. K**a mtakumbuka ligi ya msimu uliopita ilipokwisha wengine tulikwenda kujiunga na timu za taifa. Kule tulitumia k**a wiki mbili na nusu na baada ya majukumu hayo kumalizika niliomba ruhusa ili nipumzike na uongozi ukakubali, ndio maana nilichelewa kurejea nchini,” anasema.

Mashabiki wa Yanga wanachanganyikiwa wanapomuona Musonda hafungi sana akiwa klabuni kwao, lakini anafunga sana akienda timu ya Taifa ya Zambia ‘Chipolopolo’ na hapa anawapa majibu.

“Labda nikuulize wewe na mashabiki ni mara ngapi wameniona nacheza k**a mshambuliaji wa kati hapa Yanga? Nilipofika hapa nilimkuta Mayele (Fiston) ambaye alikuwa anacheza k**a mshambuliaji wa mwisho. Kwa muda wote mimi nikawa napewa nafasi nyingine pembeni, lakini nikienda timu ya Taifa nitacheza k**a mshambuliaji wa mwisho,” anasema Musonda.

“Unapocheza mbali na uso wa goli kuna ugumu sana kuweza kufanya ambacho unacho. Mimi ni mshambuliaji halisi ndio maana unaona nikipewa nafasi ya kucheza nafasi ya mshambuliaji huwa nafunga, lakini nikitakiwa kucheza mbali lazima mambo yatakuwa magumu. Lakini, mimi ni mchezaji siwezi kukataa kocha akitaka nicheze eneo gani kwa kuwa tunatafuta mafanikio ya timu.

“Naomba mashabiki waelewe mimi ni mshambuliaji wa kati halisi. Nikicheza hapo watayaona mabao, lakini naweza kucheza sehemu zingine k**a kutokea pembeni ikitegemea na mpango wa kocha anataka tucheze vipi dhidi ya timu ipi.”

Nyota huyo anapoulizwa kwa namna anavyoiona Ligi Kuu Bara ilivyo na upinzani, anafikiri Yanga inaweza kutetea tena ubingwa kwa msimu wa nne mfululizo na wa wa tatu mfululizo kwake tangu atue katika timu hiyo, naye anajibua:

“Bila shaka inawezekana kwanini isiwezekane? Kila kitu kinawezekana hatutakiwi kuruhusu mechi mbaya tulizopitia ziamue juu ya msimu wetu mzima. Ligi bado iko wazi sana. Tunatakiwa kuendelea kubadilika kurudi njia ya ushindi k**a ambavyo tunafanya.

SIMBA imerudi nchini ikiwa na tiketi yake mkononi ya kucheza robo fainali ya sita kwenye mashindano ya Caf na kwenye msa...
14/01/2025

SIMBA imerudi nchini ikiwa na tiketi yake mkononi ya kucheza robo fainali ya sita kwenye mashindano ya Caf na kwenye msafara wa timu hiyo alikuwemo mfadhili wao wa zamani, Azim Dewji, ambaye ameshuka na maneno mazito juu ya kikosi hicho kinachonolewa na Kocha Fadlu Davids.

“Kwanza niipongeze Bodi ya Wakurugenzi ya Simba chini ya Mohammed (Dewji), unajua mimi sijasafiri na Simba kwa takribani miaka 32, tangu niliposimama kuifadhili lakini hizi mechi mbili za ugenini nikasema acha niende nikaone timu inachezaje kwa macho yangu,”

“Nilikuwa Tunisia na sasa nimetoka Angola, kiukweli uongozi umefanya kazi ambayo Wanasimba walikuwa wakiililia, hiki kikosi ni bora naweza kusema hatua hii ya kwanza usajili umefanyika wa viwango.

“Unaona namna wachezaji wanacheza kwa ubora hasa hizi mechi za ugenini hata ile mechi ambayo tulipoteza ilikuwa ni makosa yetu na baada ya hapo vijana wakabadilika, ’’ -Amesema Azim Dewji

Klabu ya Simba imepokea maamuzi kutoka Shirikisho la mpira wa miguu barani Afrika (CAF) kuhusu vurugu zilizojitokeza kat...
14/01/2025

Klabu ya Simba imepokea maamuzi kutoka Shirikisho la mpira wa miguu barani Afrika (CAF) kuhusu vurugu zilizojitokeza katika mchezo wetu dhidi ya CS Sfaxien uliofanyika Disemba 15, 2024.

Uamuzi huo wa CAF umeifungia klabu yetu mechi mbili, hata hivyo adhabu hiyo imepunguzwa kuwa mechi moja kucheza bila mashabiki pamoja na faini ya Dola elfu 40,000.

Hivyo tunapenda kuufahamisha umma kuwa tunaendelea kufanya taratibu ili kushughulikia uamuzi huo. Kwa maamuzi hayo klabu inasitisha mauzo ya tiketi ya mchezo wetu dhidi ya Cs Constantine na kwa mashabiki ambao wameshanunua tiketi tunaomba tiketi hizo zitatumika kwenye mchezo ujao wa robo fainali.

Klabu ya Simba itaendelea kusimamia taratibu, kanuni na sheria zinazozingatia usalama wa jumla katika michezo.

Meneja wa habari na mawasiliano klabu ya Simba SC ametoa kauli yake baada ya Simba SC kupata pointi moja kwenye michuano...
14/01/2025

Meneja wa habari na mawasiliano klabu ya Simba SC ametoa kauli yake baada ya Simba SC kupata pointi moja kwenye michuano yao dhidi ya Bravos ya Angola.

“Kazi ya kwanza kutinga robo fainali imefanikiwa,bado kazi ya pili kuongoza kwenye msimamo wa Kombe la Shirikisho Afrika kundi la A,’’ Ahmed Ally amesema baada ya Simba SC kuenda sare.

Mkufunzi wa Manchester City  Pep Guardiola na mkewe Cristina Serra wametengana baada ya miaka 30 pamoja, kulingana na ri...
13/01/2025

Mkufunzi wa Manchester City Pep Guardiola na mkewe Cristina Serra wametengana baada ya miaka 30 pamoja, kulingana na ripoti nchini Uhispania. Mkufunzi wa Manchester City Guardiola, 53, na Serra walifunga ndoa katika sherehe ya karibu viungani mwa Barcelona mnamo 2014 lakini sasa wameamua kuachana.

Habari za mgawanyiko wao ziliripotiwa kwanza na jarida la Uhispania la Sport. Wanandoa hao waliokutana mwaka 1994, walikuwa wakiishi tofauti kwa zaidi ya miaka mitano baada ya Serra kurejea Barcelona, ​​huku Guardiola akibaki Manchester. Wana watoto watatu pamoja: Maria, 24, Marius, 22, na Valentina, 17. Guardiola na Serra, mwandishi wa habari wa Brazili, walikuwa wamebaki kuwa wanandoa licha ya kwamba hawakuishi katika jiji moja na wamekuwa wakipigwa picha za pamoja mara kwa mara katika miaka hiyo.

Sport inaripoti kwamba uamuzi wa kuvunja ndoa yao ulifanywa mnamo Desemba, na watu wa karibu tu ndio waliojua juu ya mgawanyiko huo. Marafiki na familia zao wanaoaminika pia wameambiwa wasifichue habari yoyote zaidi, kulingana na uchapishaji huo.

Bernard Morrison,  Luis Miquissone na Saido Ntibanzonkiza wanakutana tena Kengold FC Hii ni hatari sio?.
13/01/2025

Bernard Morrison, Luis Miquissone na Saido Ntibanzonkiza wanakutana tena Kengold FC

Hii ni hatari sio?.

Klabu ya Kengold FC ipo kwenye hatua za mwisho za kukamilisha usajili kiungo Mshambuliaji Luis Miquissone (29)  kutoka U...
13/01/2025

Klabu ya Kengold FC ipo kwenye hatua za mwisho za kukamilisha usajili kiungo Mshambuliaji Luis Miquissone (29) kutoka UD Songo.

Miquissone ameshatua jijini Mbeya na leo amefanya mazoezi na klabu hiyo.

Ken Gold FC hadi sasa imewasili wachezaji Obrey Chirwa, Bernard Morrison, Steven Dua, Kelvin Yondani, Sadala Lipangile, Emmanuel Asante.

Uongozi wa Ken Gold FC pia upo kwenye mkakati wa kumsajili Ntibanzokiza ambae wanaendelea na mazungumzo.

13/01/2025

Huko msimbazi ni shangwe tuu. Follow ||

Address


Telephone

+255655177370

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Nesto Shayo posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Nesto Shayo:

Videos

Shortcuts

  • Address
  • Telephone
  • Alerts
  • Contact The Business
  • Videos
  • Claim ownership or report listing
  • Want your business to be the top-listed Media Company?

Share