Orkonerei FM Radio

Orkonerei FM Radio 📻 Orkonerei FM 94.3
Sauti ya Jamii – Redio ya kwanza ya kijamii 🇹🇿
Terrat – Simanjiro, Manyara

11/01/2026

Naibu Waziri wa Ujenzi Eng.Godfrey Kasekenya amezungumzia umuhimu wa viongozi mkoani Arusha kutoa elimu kwa wananchi kuhusu namna bora ya kutunza na kulinda miundombinu inayojengwa ili idumu kwa muda mrefu, kupendezesha na kuchochea ukuaji wa mji huo wa utalii nchini.

Diwani wa kata ya monduli Juu Moses Kamaika  na Mkurugenzi wa shirika la Natopiwo,amegawa Mbuzi 41 kwa kinamama 41 wa ki...
11/01/2026

Diwani wa kata ya monduli Juu Moses Kamaika na Mkurugenzi wa shirika la Natopiwo,amegawa Mbuzi 41 kwa kinamama 41 wa kijiji cha Eluwai k**a sehemu ya kuwawezesha kiuchumi.

Kamaika pia amegawa vifaa kwa wanafunzi kumi na moja wa kata ya Monduli juu k**a vile magodoro,trucker, mabegi na madaftari kwajili ya maandalizi ya kufungua Shule Tarehe 13 Januari,2026.

09/01/2026

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Amos Makalla amesema Serikali imewekeza fedha katika kuboresha Masoko yaliyopo Jijini Arusha, lengo likiwa ni kuboresha mazingira ya ufanyaji wa biashara pamoja na kuongeza fursa za kiuchumi kwa wananchi wa Arusha.

Makalla amebainisha hayo leo Ijumaa Januari 09, 2026 wakati wa ziara yake ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa mradi wa soko la Morombo, unaotekelezwa kwa jumla ya shilingi Bilioni 2.2.

Kuanzia tarehe 19 Januari, 2026, wakazi wa Wilaya ya Simanjiro hususan Kata ya Terrat, wanatarajia kuanza kunufaika na h...
08/01/2026

Kuanzia tarehe 19 Januari, 2026, wakazi wa Wilaya ya Simanjiro hususan Kata ya Terrat, wanatarajia kuanza kunufaika na huduma za kisheria, kufuatia kufunguliwa rasmi kwa Mahak**a ya Mwanzo Terrat.

Taarifa iliyotolewa na Jaji Mfawidhi, I.C. Mugeta, imebainisha kuwa hatua hiyo ni sehemu ya utekelezaji wa adhma ya Mahak**a ya Tanzania ya kusogeza huduma za haki karibu na wananchi, kwa kuzingatia matakwa ya Sheria ya Mahak**a za Mahakimu (Sura ya 11, Toleo la 2023).

08/01/2026

Tuandikie maoni yako hapa na yatasomwa kwenye Mchakamchaka Saa 4:00 Asubuhi.
Evander Barnabas

06/01/2026
Wananchi wa Mkoa wa Arusha na Mikoa ya jirani wamemshukuru Rais wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa uwezeshaji...
06/01/2026

Wananchi wa Mkoa wa Arusha na Mikoa ya jirani wamemshukuru Rais wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa uwezeshaji wake wa programu ya vipimo na matibabu bure kwa magonjwa ya moyo inayofanyika kwa ushirikiano Kati ya Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) na Hospitali ya Arusha Lutheran Centre (Seliani).

Leo Jumanne Januari 06, 2025 wakati wa ziara ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. CPA Amos Gabriel Makalla ya kukagua zoezi hilo la matibabu, amesema ujenzi wa Kituo cha JKCI katika Hospitali hiyo kutasaidia pia wananchi, watalii pamoja na washiriki wa michuano ya Mpira wa miguu kwa mataifa huru ya Afrika (AFCON) itakayochezwa Mkoani Arusha mwaka 2027.

Kulingana na Makalla wakati akizungumza na wananchi na watoa huduma katika Programu hiyo, jumla ya wananchi takribani 1,200 wamenufaika na huduma hiyo ya matibabu bure, akiahidi kwamba serikali itawawezesha wananchi wasiokuwa na uwezo na waliopewa rufaa ya kwenda kutibiwa zaidi kwenye Taasisi ya Moyo JKCI Mkoani Dar Es Salaam pamoja na kuhamasisha wananchi umuhimu wa Bima ya afya kwa wote.

Na Nyangusi Ole Sang'ida

06/01/2026

Maoni yatasomwa kwenye Mchakamchaka Asubuhi Saa 4:00

06/01/2026

06/01/2026

Unafahamu kiasi Cha Pombe kinachopaswa kutumiwa na Binadamu ?!
Taarifa kamili ya Habari ni saa Moja Kamili za Usiku!

05/01/2026

Ungefanyaje ingekuwa ni wewe? Maoni yatasomwa kwenye Mchakamchaka Asubuhi

04/01/2026

Mkuu wa Wilaya ya Arusha Jiji, Joseph Mkude, ametoa ufafanuzi na wito kwa wananchi kujitokeza kwa wingi kwenye kambi ya matibabu ya magonjwa ya moyo inayoendelea Hospitali ya Selian. Uchunguzi na matibabu BURE.
Tayari zaidi ya 800 wamehudumiwa – wazima 700 na watoto 100.

Address

P O Box 12785 Arusha
Arusha
27613-16

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Orkonerei FM Radio posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Category