Orkonerei FM Radio

Orkonerei FM Radio Orkonerei FM Radio
Radio ya Kwanza ya Kijamii Nchini Tanzania.

Ushoroba wa Kwakuchinja, ukanda muhimu wa wanyamapori Kaskazini mwa Tanzania, si tu huchangia uhifadhi wa mazingira bali...
21/01/2025

Ushoroba wa Kwakuchinja, ukanda muhimu wa wanyamapori Kaskazini mwa Tanzania, si tu huchangia uhifadhi wa mazingira bali pia maendeleo ya kiuchumi kwa jamii zinazouzunguka. Kupitia miundombinu ya hoteli, wakazi wa vijiji 10 vinavyounda Burunge WMA wanapata fursa za ajira, elimu ya uhifadhi, na kipato mbadala kupitia shughuli k**a kilimo, biashara ndogo ndogo, na burudani za asili.

Zaidi ya watu 700 wamepata ajira za moja kwa moja, huku wengine wengi wakifaidika kupitia huduma za hoteli. Hii imesaidia kupunguza utegemezi wa jamii kwenye rasilimali za asili k**a ukataji wa miti na uzalishaji wa mkaa.

Kwa ufahamu zaidi kuhusu jinsi hoteli zinavyoleta ajira na maendeleo katika ushoroba wa Kwakuchinja, sikiliza makala yetu kamili kwa sauti pia na kusoma kupitia www.ors-radio.co.tz.

Katika Mkutano Mkuu Maalum wa Chama Cha Mapinduzi uliofanyika Januari 18-19, 2025, Dkt. Emmanuel John Nchimbi alipitishw...
20/01/2025

Katika Mkutano Mkuu Maalum wa Chama Cha Mapinduzi uliofanyika Januari 18-19, 2025, Dkt. Emmanuel John Nchimbi alipitishwa kuwa mgombea mwenza wa Rais Samia Suluhu Hassan kwa Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu.

Dkt. Nchimbi ni Nani?:
Alizaliwa Desemba 24, 1971, Songea, Tanzania, Dkt. Nchimbi amekuwa sehemu muhimu ya siasa na utawala wa Tanzania. Ana Shahada ya Uzamivu (Ph.D.) katika masuala ya uongozi kutoka Chuo Kikuu cha Open University of Tanzania.

Safari yake ya kisiasa ilianza mwaka 1998 alipokuwa Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM). Mwaka 2005, alichaguliwa kuwa Mbunge wa Jimbo la Songea Mjini, nafasi aliyoitumikia kwa miaka 10. Katika kipindi hicho, alishika nyadhifa mbalimbali serikalini, ikiwa ni pamoja na:

Naibu Waziri wa Kazi, Ajira na Vijana (2006-2008)
Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo (2010-2012)
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi (2012-2013)

Baada ya utumishi wake wa kibunge, Dkt. Nchimbi alihamia kwenye nyanja ya kidiplomasia, ambako aliwahi kuwa: Balozi wa Tanzania nchini Brazil na Balozi wa Tanzania nchini Misri.

Mnamo Januari 2024, aliteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa CCM, akiimarisha mfumo wa chama hicho na kuhakikisha usimamizi wa sera zake kwa ufanisi mkubwa.

Uteuzi wake k**a mgombea mwenza unaakisi uzoefu wake wa muda mrefu, umahiri wa uongozi, na utayari wa kushirikiana na Rais Samia kuendeleza kile walichokianza ndani ya chama hicho kikongwe cha siasa Barani Afrika.

🎉🎙️ Happy Birthday Grace Nyaki! 🎂✨Leo ni siku maalum tunaposherehekea maisha na mchango wa kipekee wa mtangazaji na mwan...
19/01/2025

🎉🎙️ Happy Birthday Grace Nyaki! 🎂✨
Leo ni siku maalum tunaposherehekea maisha na mchango wa kipekee wa mtangazaji na mwandishi wetu mahiri, Grace Nyaki! 🎧📖

Asante kwa kujituma, ubunifu, na sauti yako yenye nguvu inayowahamasisha na kuelimisha jamii kupitia . Tunajivunia kuwa na wewe kwenye timu yetu! 🌟💪

Tunakutakia maisha marefu, yenye afya, furaha, na mafanikio tele! Endelea kung'ara, Grace! 🌸💜

🎈 Tuungane kumpa Grace maneno ya heri siku hii ya kumbukizi yake ya kuzaliwa! 💬👇

18/01/2025

Mtaalamu wa sheria, Ndg. Saitabau Laadapi, mwanafunzi wa shahada ya sheria katika Chuo Kikuu cha Tumaini Makumira jijini Arusha anasema kijiji kisajiliwe ila kwa mtu binafsi basi hakikisha umekabidhiwa ardhi kisheria.

17/01/2025

Afisa Tarafa ya Terrat, Bwana Lekishon Kiruswa, amewakumbusha viongozi na wakuu wa idara za Tarafa ya Terrat kuhusu umuhimu wa kushirikiana na kutekeleza majukumu yao kwa weledi. 🌟

🚨 Suala la ulinzi na usalama pia limepewa kipaumbele! Kamanda wa Polisi James Matei amesisitiza mpango wa kuwatambua askari mgambo ili kuimarisha usalama vijijini. 👮‍♂️

🎥 Tazama sehemu ya kikao hicho kwenye video. Je, ushirikiano wa viongozi ni suluhisho la changamoto za maendeleo?

📌

"Mimi ninashauri uandikishaji uanzie kwa wenyeviti wa vitongoji maana wao ndiyo wanawatu na wanawafahamu" Mwalimu mkuu s...
16/01/2025

"Mimi ninashauri uandikishaji uanzie kwa wenyeviti wa vitongoji maana wao ndiyo wanawatu na wanawafahamu" Mwalimu mkuu shule ya msingi Engonongoi Samwel Dahaye

"Mtoto mmoja tu ndiyo ameandikishwa shule ya awali,lakini kwa shule ya msingi wamefika shuleni watoto 8 kati ya 86 walio...
16/01/2025

"Mtoto mmoja tu ndiyo ameandikishwa shule ya awali,lakini kwa shule ya msingi wamefika shuleni watoto 8 kati ya 86 walioandikishwa"Mwalimu mkuu shule ya Msingi Engonongoi Samwel Dahaye

"Kuna korongo linatoka mjini Ngaramtoni,mafuriko ya korongo lile yanaingia mpaka shuleni ni changamoto nyingine,na shule...
16/01/2025

"Kuna korongo linatoka mjini Ngaramtoni,mafuriko ya korongo lile yanaingia mpaka shuleni ni changamoto nyingine,na shule yetu pia haina uzio na mifugo inaingia kuharibu mazingira ya shule" K/Mwalimu mkuu shule ya Msingi Endupoto Godwin Kidio

kutoka katika kikao kazi cha Tarafa ya Terrat tarehe 16/01/2025

"Shule yetu haina huduma ya maji wala umeme hiyo inatufanya tufuate maji km 3 kutoka shuleni,...Changamoto nyingine ni u...
16/01/2025

"Shule yetu haina huduma ya maji wala umeme hiyo inatufanya tufuate maji km 3 kutoka shuleni,...Changamoto nyingine ni utoro" Mwalimu mkuu shule ya Msingi Endupoto Godwin Kidio

💧 MAJI NI UHAI! 🌍 Umefikiria mwili wako unavyoteseka unapokaa muda mrefu bila kunywa maji? 🥵 🔑 Ukweli ni kwamba maji yan...
16/01/2025

💧 MAJI NI UHAI! 🌍 Umefikiria mwili wako unavyoteseka unapokaa muda mrefu bila kunywa maji? 🥵 🔑 Ukweli ni kwamba maji yanasaidia kuboresha afya yako, kuongeza nishati, na hata kung'arisha ngozi yako! 🫧 Usisahau kwamba kunywa maji ni mojawapo ya hatua rahisi za kudumisha afya bora. 🍃

Swali letu kwako: UMEWAHI KUKAA KWA MUDA GANI BILA KUNYWA MAJI? Tuambie kwenye comments! 👇👇

"Suala la taaluma kwakweli hatujafanya vizuri Darasa la Saba tuna ufaulu wa asilimia 43,Darasa la Nne tunaufaulu wa asil...
16/01/2025

"Suala la taaluma kwakweli hatujafanya vizuri Darasa la Saba tuna ufaulu wa asilimia 43,Darasa la Nne tunaufaulu wa asilimia 39,Changamoto kubwa ni utoro lakini bahati nzuri tumekwisha kuweka mikakati kwahivyo tunaendelea kujipanga, Nashukuru sana" Japhari Sombi Mkuu wa shule ya Msingi Loorg'oswani

"Mimi nilikutana na hiyo kesi mwaka jana Kwamba mzazi jina tumeletewa shule lingine na mtoto aliyeletwa shule ni mwingin...
16/01/2025

"Mimi nilikutana na hiyo kesi mwaka jana Kwamba mzazi jina tumeletewa shule lingine na mtoto aliyeletwa shule ni mwingine k**a ushahidi tu na mtoto hafanani kabisa na yule jina liloletwa,kwahivyo wazazi haswa wa kiume wanawachepusha watoto shule,hawawaleti shule,afadhali na akina mama kidogo wanamuamko" Mwalimu Japhari Sombi Mkuu wa shule ya Msingi Loorg'oswani Terrat ,Simanjiro.

Kutoka katika kikao kazi kilichoitishwa na Afisa Tarafa Tarafa ya Terrat.

"Mimi ni mama na watoto wangu wanasoma,sasa siwezi kukaa hapa nikawashudia watoto hawaendi shule,nasema tutawatafuta wat...
16/01/2025

"Mimi ni mama na watoto wangu wanasoma,sasa siwezi kukaa hapa nikawashudia watoto hawaendi shule,nasema tutawatafuta watoto ikibidi hadi uvunguni ili waende shule" Afisa Mtendaji wa kata ya Terrat Bi.Dorothea Johnson
Kutoka katika kikao kazi cha kupeana maelekezo tarafa ya Terrat.

"Kuhusu hilo la Grocery (Baa) haiwezekani baa zikafunguliwa hadi saa 8 Usiku,Utakuwa unamuuzia nani? hapo ndipo uwalifu ...
16/01/2025

"Kuhusu hilo la Grocery (Baa) haiwezekani baa zikafunguliwa hadi saa 8 Usiku,Utakuwa unamuuzia nani? hapo ndipo uwalifu wakati mwingine unatokea,sasa viongozi wa vijiji,hadi kata shuhulikieni hilo,lakini kwa kukagua leseni za biashara,na sidhani k**a huku kwetu vijijini kuna leseni za kufanya biashara usiku kucha"Lekishon Kiruswa Afisa Tarafa wa Tarafa ya Terrat-Simanjiro.

Ameyasema hayo Katika kikao kazi cha kupeana maelekezo kilichoketi leo Tarehe 16 January 2024 shule ya sekondari Terrat,ambapo kimehudhuriwa na Wenyeviti wa Vitongoji na Vijiji,watendaji wa Vijiji na kata,waalimu wa kuu wa shule za msingi na sekondari na wakuu wa idara na wataalamu katika Tarafa ya Terrat.

"Tarehe 29 mwezi huu tutakuwa na kikao na mkuu wa Wilaya   kuhusu wanafunzi kuhudhuria na kuandikishwa shule haswa shule...
16/01/2025

"Tarehe 29 mwezi huu tutakuwa na kikao na mkuu wa Wilaya kuhusu wanafunzi kuhudhuria na kuandikishwa shule haswa shule za sekondari,Nataka tukubaliane hapa kuwa kwa Tarafa yetu mwisho tufanye tarehe 25 ili nikifika huko kwenye kikao nawasilisha sisi tukiwa tumekamilika"Afisa Tarafa- Terrat Lekishon Kiruswa

16/01/2025

Mbegu feki zilizokuwa zinasambazwa kwa wananchi wa Kata ya Emboret zimek**atwa! Mkuu wa Wilaya ya Simanjiro, , ameapa kuchukua hatua kali dhidi ya wanaohusika. "Tutahakikisha wakulima wetu hawatumii mbegu feki..!" 🗣️🔥

Cc
📌

Kati ya kula vizuri na kuvaa vizuri, wewe ungechagua nini? 🥗👗 Hebu tuambie chaguo lako na sababu hapa👇!                 ...
15/01/2025

Kati ya kula vizuri na kuvaa vizuri, wewe ungechagua nini? 🥗👗 Hebu tuambie chaguo lako na sababu hapa👇!

14/01/2025

Nani mmiliki halali wa ardhi ya mpaka kati ya Kijiji cha Terrat na Sukuro? 🤔 Mgogoro huu umeibua hisia kali kwenye mkutano wa kijiji cha Terrat! Mwenyekiti wa kijiji, viongozi wa zamani, na wananchi wanapishana kauli kuhusu nani anayemiliki ardhi hii. Je, ni haki ya kijiji au mali binafsi?

🎥 Tazama video kamili kupitia kurasa zetu na utuambie maoni yako kwenye comments! 👇

📌 Je, siasa zinachangia mgogoro huu au ni changamoto ya usimamizi wa ardhi vijijini?

💬 Tupatie maoni yako: Kipi kifanyike kutatua mgogoro huu mara moja?

🎙️

🌾






Address

P O Box 12785 Arusha
Arusha
27613-16

Telephone

+255785396786

Website

https://ors-radio.co.tz/

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Orkonerei FM Radio posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Orkonerei FM Radio:

Videos

Share

Category