12/06/2024
... UTUKUFU WA BWANA USIONDOKE, IKABODI! 1 Samweli 4:19-22
Mkwewe, mke wa Finehasi, alikuwa mjamzito na karibu wakati wa kujifungua. Aliposikia habari kwamba Sanduku la Mungu limetekwa na ya kuwa baba mkwe wake na mumewe wamekufa, akapata utungu naye akajifungua lakini akazidiwa na utungu. Alipokuwa akifa, wanawake waliokuwa wanamhudumia wakamwambia, “Usikate tamaa, umemzaa mwana.” Lakini hakujibu wala kuweka maanani. Alimwita yule mtoto Ikabodi, akisema, “Utukufu umeondoka katika Israeli,” kwa sababu ya kutekwa kwa Sanduku la Mungu na vifo vya baba mkwe na mumewe. Akasema, “Utukufu umeondoka katika Israeli, kwa kuwa Sanduku la Mungu limetekwa.” Ni uchungu na hatari kiwa katika hali ya Ikabodi yaani kuondokewa na utukufu wa Mungu pale utakosa kibali kabisa, utang'ang'ana vibaya, utakataliwa karibu na kila mtu maana huna utukufu! Nakuombea Ikabodi isiwahi kuja kwa maisha yako, mpendeze Mungu Na ufuate maagizo yake, utukufu wake utakujaa. Tukutane Galilaya!