Magnet Radio

Magnet Radio Powered by IPO SIKU MEDIA{ISM}

Magnet Radio~Stick With Us! ISM~Your Getaway to Digital Excellence!
(1)

 Nyimbo za "Ruto Must Go" zimeshuhudiwa  Kisumu Leo jioni kufuatia kushindwa kwa Raila Odinga katika kinyang'anyiro cha ...
15/02/2025


Nyimbo za "Ruto Must Go" zimeshuhudiwa Kisumu Leo jioni kufuatia kushindwa kwa Raila Odinga katika kinyang'anyiro cha uenyekiti wa Tume ya AU.

Wakaazi wamemlaumu Rais William Ruto kwa kumhadaa Raila katika ombi lililofeli na kumtaka kiongozi huyo wa upinzani arejee nyumbani na kuangazia upya kuwatetea Wakenya dhidi ya ukandamizaji wa serikali k**a alivyofanya hapo awali.

 DJIBOUTI YANYAKUWA AUCMahmoud Ali Youssouf, Waziri wa Mambo ya Nje wa Djibouti, amechaguliwa kuwa Mwenyekiti mpya wa Tu...
15/02/2025


DJIBOUTI YANYAKUWA AUC
Mahmoud Ali Youssouf, Waziri wa Mambo ya Nje wa Djibouti, amechaguliwa kuwa Mwenyekiti mpya wa Tume ya Umoja wa Afrika (AUC).

Baada ya ushindani mkali na mchakato wa upigaji kura, Youssouf ameishinda kwa kupata kura za wengi (33 round ya saba).

 AZMA YA ODINGA AUC YAFELIMuwaniaji wa uenyekiti wa AUC Kutoka humu Nchini Raila Odinga amejiondoa kwenye kinyanganyiro ...
15/02/2025


AZMA YA ODINGA AUC YAFELI
Muwaniaji wa uenyekiti wa AUC Kutoka humu Nchini Raila Odinga amejiondoa kwenye kinyanganyiro cha uchaguzi huo baada ya kushindwa na muwaniaji wa Djibouti Mahmoud Yussouf Ali Kwa Kura 26, Odinga amekuwa akiongoza kwenye awamu ya Kwanza na ya Tatu kabla ya maji kuzidi unga.

 RUTO ATIMIZA AHADI!Rais William Ruto ametimiza ahadi yake ya shilingi milioni moja kwa wahudumu wa bodaboda aliyotowa w...
15/02/2025


RUTO ATIMIZA AHADI!
Rais William Ruto ametimiza ahadi yake ya shilingi milioni moja kwa wahudumu wa bodaboda aliyotowa wakati wa ziara yake kaunti ya Busia hivi maajuzi.

Akiwakabidhi wahudumu hao wa bodaboda fedha hizo katika afisi ya NG,CDF Nambale mbunge Geoffrey Mulanya ametaka fedha hizo kutumika vyama kuendeleza miradi kwenye vikundi vya wahudumu hao wa bodaboda eneo bunge hilo.

15/02/2025

Mtangazaji mkongwe Leonard Mambo Mbotela azikwa katika makaburi ya Lang’ata jijini Nairobi; alifariki wiki iliyopita akiwa na umri wa miaka 84, baada ya kuugua kwa muda mfupi.
Lala salama Mzee Mbotela

 Uchaguzi wa mwenyekiti na naibu mwenyekiti wa Tume ya Umoja wa Afrika (AUC) Unaendelea hivi sasa Kule Addis Ababa mji m...
15/02/2025


Uchaguzi wa mwenyekiti na naibu mwenyekiti wa Tume ya Umoja wa Afrika (AUC) Unaendelea hivi sasa Kule Addis Ababa mji mkuu wa Ethiopia.

Uchaguzi huo utaamua hatima ya wagombea watatu wanaowania nafasi ya mwenyekiti hii nchini Ethiopia. Marais na wakuu wa mataifa wasiopungua 50 wanashiriki katika upigaji kura.
Wagombea wa nafasi hiyo ni;

· Mahmoud Ali Youssouf kutoka Djibouti,

· Raila Amollo Odinga kutoka Kenya, na

· Richard Randriamandrato kutoka Madagascar.

Umoja wa Afrika ulianzisha utaratibu wa kisasa na wa uwazi katika uchaguzi wa Mwenyekiti wa Tume la Umoja wa Afrika 2025.

 Sehemu ya barabara kuu ya Thika inatarajiwa kufungwa Kwa siku nne, Kulingana na taarifa ya Mkurugenzi Mkuu wa KeNHA, En...
15/02/2025


Sehemu ya barabara kuu ya Thika inatarajiwa kufungwa Kwa siku nne, Kulingana na taarifa ya Mkurugenzi Mkuu wa KeNHA, Eng. Kung’u Ndungu, barabara hiyo itafungwa kwa siku nne kuanzia Jumamosi, Februari 15, 2025, hadi Jumanne, Februari 18, 2025, kati ya saa tano usiku na saa kumi na mbili asubuhi.

Hatua hii imechukuliwa ili kuruhusu ujenzi wa daraja jipya la watembea kwa miguu.

Madereva wanaoelekea Nairobi wametakiwa kutumia barabara ya mzunguko iliyo nyuma ya kituo cha mafuta cha Lex Petrol kabla ya kuungana tena na Thika Superhighway.

 Wizara ya Afya imethibitisha visa vipya vitatu vya ugonjwa wa Mpox, na kufikisha jumla ya visa 41 tangu mlipuko ulipoan...
15/02/2025


Wizara ya Afya imethibitisha visa vipya vitatu vya ugonjwa wa Mpox, na kufikisha jumla ya visa 41 tangu mlipuko ulipoanza Julai 2024.

Katibu wa Idara ya Afya ya Umma na Viwango vya Kitaaluma, Mary Muthoni Muriuki, alisema jumla ya watu 271 waliotangamana na wagonjwa hao 41 wamebainishwa.

Uchaguzi wa AU umepangwa kufanyika kuanzia saa sita hadi saa nane mchana (saa za Kenya).Kwa sasa ni mazungumzo na hotuba...
15/02/2025

Uchaguzi wa AU umepangwa kufanyika kuanzia saa sita hadi saa nane mchana (saa za Kenya).
Kwa sasa ni mazungumzo na hotuba Kutoka Kwa viongozi.

Picha za moja Kwa moja viongozi wa Kenya wakiwa Kule Addis Ababa mji mkuu wa Ethiopia.
15/02/2025

Picha za moja Kwa moja viongozi wa Kenya wakiwa Kule Addis Ababa mji mkuu wa Ethiopia.

15/02/2025

Muwaniaji wa kiti cha umoja wa Afrika AUC Raila Odinga amesafiria Kwa gari moja na Rais hii leo wakielekea Katika makao makuu ya AUC Addis Ababa mji mkuu wa Ethiopia.
Picha Kwa Hisani

 Maafisa 3 wa polisi wametiwa mbaroni na maafisa wa upelelezi wa EACC baada ya kuchukua hongo ya shilingi alfu 48 kutoka...
14/02/2025


Maafisa 3 wa polisi wametiwa mbaroni na maafisa wa upelelezi wa EACC baada ya kuchukua hongo ya shilingi alfu 48 kutoka kwa madereva na raia ndani ya saa 2 katikati Mwa jiji kuu la Nairobi.

Watatu hao ni Koplo Oscar Serem Biwott, Konstebo Simon Kiplagat Nyunyutik na Konstebo Edwin Benedict Mubweka, walinaswa kwenye mzunguko wa Globe Cinema wakiwa wamekusanya hongo ya shilingi alfu 48,250 ndani ya saa mbili.

14/02/2025

Kanda ya video Kutoka makao makuu ya AUC Addis Ababa mji mkuu wa Ethiopia...

 Kiongozi wa chama cha DAP Kenya Eugene Wamalwa amemtaka gavana wa Busia Dr Paul Otuoma kukoma kutoa vitisho kwa viongoz...
14/02/2025


Kiongozi wa chama cha DAP Kenya Eugene Wamalwa amemtaka gavana wa Busia Dr Paul Otuoma kukoma kutoa vitisho kwa viongozi wa upinzani nchini wanaolenga kuzuru kaunti ya Busia kutafuta uungwaji mkono.

Akizungumza katika chuo anuai cha Butula wakati wa hafla ya mazishi ya aliyekuwa naibu gavana wa Busia Moses Mulomi, Wamalwa amesema kila mkenya anauhuru wa kuzuru mahali popote nchini kuuza sera zake bila kuzuiliwa na mtu yeyote.

Didmus Barasa, Mbunge wa Kimilili, ana imani kwamba uboreshaji wa kisasa na uendelezaji wa madarasa mapya katika Shule y...
14/02/2025

Didmus Barasa, Mbunge wa Kimilili, ana imani kwamba uboreshaji wa kisasa na uendelezaji wa madarasa mapya katika Shule ya Msingi ya Nasianda utaboresha kwa kiasi kikubwa uzoefu wa kielimu kwa wanafunzi na kuwapa motisha ya kufikia viwango vya juu vya kufaulu kitaaluma.

Unamwambia nini Odinga na kikosi chake kabla ya uchaguzi wa mwenyekiti wa umoja wa Afrika AUC??
14/02/2025

Unamwambia nini Odinga na kikosi chake kabla ya uchaguzi wa mwenyekiti wa umoja wa Afrika AUC??

Seneta wa Nandi Samson Cherargei ameeleza kuwa ana imani Raila Odinga atapata ushindi mnono katika uchaguzi wa mwenyekit...
14/02/2025

Seneta wa Nandi Samson Cherargei ameeleza kuwa ana imani Raila Odinga atapata ushindi mnono katika uchaguzi wa mwenyekiti wa Umoja wa Afrika Jumamosi hii, na kuthibitisha ujumbe huu kwa taifa zima.

Inasikitisha kuona kwamba nguli Leonard Mambo Mbotela atazikwa katika Makaburi ya Lang’ata, ambapo kuna uwezekano kaburi...
14/02/2025

Inasikitisha kuona kwamba nguli Leonard Mambo Mbotela atazikwa katika Makaburi ya Lang’ata, ambapo kuna uwezekano kaburi lake likae juu ya jingine kutokana na msongamano wa watu eneo hilo, mbona watu mashuhuri k**a hao wasitengewe mahali maalim." Spika wa Bunge la Kitaifa Moses Wetangula

Address

St Marys Kibomet-Kitale
Kitale

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Magnet Radio posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Magnet Radio:

Videos

Share