Imara média Imara média, c'est le media sous régionale pour la recherche de la paix et la réconciliation.

DRC : Usalama/ Kivu Kaskazini.""""""""""""""""""""""""""""""""""'"""""""""Hali yautulivi yaripotiwa baada ya mapigano pa...
20/08/2023

DRC : Usalama/ Kivu Kaskazini.
""""""""""""""""""""""""""""""""""'"""""""""

Hali yautulivi yaripotiwa baada ya mapigano pakali kuripotiwa siku ya jumamosi kati ya jeshi la Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kwa ushirikiano na vikosi vya MONUSCO dhidi ya wanamgambo wa ADF. Mapigano hayo yameripotiwa kijijini Luna, tarafa la Beni, jimboni Kivu Kaskazini.

Taarifa kutoka kwa mkuu wa baraza la vijana eneo la Eringeti, Germain Kakule Vatsurana amesema kua idadi kubwa ya raïa ambao walikua wamekimbia kijiji cha Luna na kuomba hifadhi Eringeti wameanza kurejelea makani yao.

Jeshi kwa upande wake limesema kua linaendeleza operesheni za kuwasaka wanamgambo hao hadi lihakikishe limewatokomeza.

Eneo la mashariki mwa DRC, limekua likikumbwa na hali ya vurugu ambazo zinasababishwa na makundi yenyekumiliki silaha kutoka nje na ndani ya nchi yapata sasa takribani miongo mitatu.

DRC: JESHI LA EAC LARIZISHWA NA HATUA AMBAYO LIMEFIKIA./ By Madiba Mahoye.""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""'"""...
18/08/2023

DRC: JESHI LA EAC LARIZISHWA NA HATUA AMBAYO LIMEFIKIA./ By Madiba Mahoye.
""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""'"""""""""""""""""""""""""""""""""""""""

Jumuiya ya Afrika Mashariki, imesema kikosi chake kilichoko nchini Jamuhiri ya Kidemokrasia ya Kongo, kimepata mafanikio makubwa katika kurejesha hali ya amani na utulivu mashariki mwa nchi hiyo.

Wanajeshi wa EAC wamekuwa wakiendelea kuwalinda raia kutokana na makundi ya watu wenye silaha mashariki wa DRC kwa ushirikiano na wale wa FARDC.

Vikosi hivyo vilitumwa mashariki ya taifa hilo kujaribu kutatua changamoto za kiusalama zinazowakabili raia katika eneo hilo.

Aidha katibu Mkuu wa Jumuiya hiyo Peter Mathuki, amekanusha madai kuwa kikosi hicho, kimeshindwa katika majukumu yake.

“Kikosi chetu cha Jumuiya kinafanya kazi nzuri mashariki mwa DRC kwa uongozi wa mwenyekiti wa wanachama rais Évariste Ndayishimiye na marais wengine wanashirkiana vyema kuhakikisha kwamba usalama unarejea na tunashirkiana pia na kikosi cha MONUSCO.” alisema Peter Mathuki.
Haya yanajiri wakati huu tume ya haki za binadamu ya umoja wa Mataifa nchini DRC, juma hili imetoa ripoti yake inayoonesha kuwa vitendo vya mauaji na ukiukaji mwingine wa haki za binadalu vimeongezeka maradufu katika nusu ya kwanza yam waka huu.

Akizungumza na wanahabari jijini New York, msemaji wa umoja wa Mataifa, Staphane Dujarric, amesema vitendo hivyo vimekuwa na madhara zaidi kwa raia hasa wa eneo la mashariki.
Aidha kiongozi huyo alisema kuwa katika miezi sita ya mwaka 2023, wastani wa raia tisa waliuawa kila siku mashariki mwa DRC.

Ripoti hii imetolewa wakati huu makundi yenye silaha mashariki mwa nchi hiyo yakiendelea kuua raia licha ya uwepo wa vikosi vya UN na vile vya nchi za ukanda.

DRC:Usalama/ NCHI WANACHAMA WA SADEC ZAKUBALI KUTUMA WANAJESHI NCHINI DRC. / By Madiba Mahoye.""""""""""'"""""""""""""""...
18/08/2023

DRC:Usalama/ NCHI WANACHAMA WA SADEC ZAKUBALI KUTUMA WANAJESHI NCHINI DRC. / By Madiba Mahoye.
""""""""""'""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""
Viongozi wa jumuiya ya maendeleo ya Kusini mwa Afrika SADC wamekubaliana kupeleka wanajeshi nchini DRC, na kuongeza muda wa ujumbe wa kijeshi wa jumuiya hiyo nchini Msumbiji, katika hatua ambayo wanasema inalenga kuleta amani katika eneo hilo.

Maazimio hayo yametolewa baada ya Mkutano wa 43 wa Kawaida wa Wakuu wa nchi jana jijini Luanda nchini Angola.

Kikosi cha SADC kitakuwa cha tatu, baada ya kile cha Jumuiya ya Afrika Mashariki na Umoja wa Mataifa, MONUSCO.

Wadadisi wa mambo wanasema mpango wa kupelekwa kwa kikosi cha SADC kinachopendelewa na rais Felix Tshisekedi, kitashirikiana na kile cha Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Kikosi cha Jumuiya ya EAC kina hadi mwezi Septemba, kuendelea na operesheni zake, na iwapo hakitaongezewa muda na Kinshasa, huenda hatua hiyo inasukuma ujio wa kikosi cha SADC ambayo haijafahamika ni lini kitakuja.

Kauli hii ya SADC inakuja wakati katibu mkuu wa umoja wa mataifa Antonio Guterres akitangaza kuwa kuanzia mwezi Desemba, MONUSCO itaanzisha mchakato wa kuanza kuondoa vikosi vyake Mashariki mwa nchi.

DRC- Bukavu: MUUNGANO WA AKINAMAMA KWA AJILI YA AMANI JIMBONI KIVU KUSINI WAOMBA WAHAMASISHA KINAMAMA KUPEWA KIPAU MBELE...
16/08/2023

DRC- Bukavu: MUUNGANO WA AKINAMAMA KWA AJILI YA AMANI JIMBONI KIVU KUSINI WAOMBA WAHAMASISHA KINAMAMA KUPEWA KIPAU MBELE KWENYE ORODHA YA WAGOMBEA KWENYE UBUNGE./ By Madiba Mahoye.
""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""
Muungano wa kinamama kwa ajili ya amani jimboni Kivu ya Kusini , jumanne hii tare 15 August wamekua mbioni kwa kuhamasisha vyama vya kisiasa kuwapa kipao mbele wanawake kwenye nafasi za kugombea ubunge.

Bi Solange Lwashinga amefanya ombi hilo wakati wakiko huku akiwahamasisha wanawake mjini Bukavu.

Shughulizo zinafanywa kwa malengo ya mradi wa >.

Solange Lwashinga ametumia fursa hivyo kwa kuvikumbusha vyama vya kisiasa kua kueshimu kipengeli nambari 13 cha sheria za uchaguz, kipengeli hicho kinasema kua

DRC- ITURI: WATU 11 WARIFIWA KUUAWA NA KUNDI LA WANAMGAMBO WA CODECO. /By Madiba Mahoye.""""""""""""""""""""""""""""""""...
16/08/2023

DRC- ITURI: WATU 11 WARIFIWA KUUAWA NA KUNDI LA WANAMGAMBO WA CODECO. /By Madiba Mahoye.
"""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""
Watu 11 wameua na wengine wamejuruhiwa na wanamgambo wanaosadikiwa kua ni wnamgambo wa CODECO, siku ya jumanne tare 15 August katika kijiji cha Ngongo na Bukela tarafani Irumu Jimboni Ituri.

Duru kutoka eneo hilo zaeleza kua nyumba zipatazo 40 zimechomwa moto na wanamgambo hao na kusababisha watu kuyhama makazi yao.

Duru hizo zimeendelea kusema watu wanaosadikiwa kua wanamgambo wa CODECO wamevishambulia vijiji hivyo wakiwa wamebeba bunduki na silaha za jadi katika vijiji hivyo vinavyopatikna kwenye umbali wa karibu kilometa 12 na mji wa Bunia.

Wamepiga risasi raïa wasio na hatiya , wengi wao wakiwa ni wachimbaji wa dini kwenye migidi.
Shirika la raïa lataja idadi ya watu 15walio uaawa na makumi ya majeruhi.

DRC: Goma/  ASKARI JESHI WA FARDC AHUKUMIWA KIFO KWA KOSA LA MAUAJI./ By Madiba Mahoye."""""""""""""""""""""""""""""""""...
16/08/2023

DRC: Goma/ ASKARI JESHI WA FARDC AHUKUMIWA KIFO KWA KOSA LA MAUAJI./ By Madiba Mahoye.
""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""
Korti kuu ya mahak**a ya kijeshi mjini Goma jumanne tarehe 15 August 2023 imetoa hukumu ya kifo kwa askari jeshi wa FARDC baada ya kesi hiyo kuskilizwa kwenye mahak**a ya kesi za jumla katika mtaa wa Sake.

Mshukiwa huyo wa mauaji amekutwa na kosa hilo baada ya kumuua muendesha piki piki maarufu boda boda mwishoni mwa week-end ilio pita katika eneo la Mubambiro tarafani Masisi.

Raïa wa eneo hilo wameonesha kurizishwa na hukumu hiyo na kusema kua kuskilizwa kwa kesi hizo za jumla na kutoa adhabu k**a hizo kwa wanajeshi wenye mwenendo m'baya ni funzo na mfano bora kwa wengine wanajeshi wanao fanya makosa ya maksudi dhidi ya raïa wasio na hatiya.

Askari huyo ambae amehukuwi adhabu ya kifo anaïtwa Mopati Mikasi Ebende ,alikua anafanyia kazi eneo la Rusayu tarafani Nyiragongo, baada ya kufanya mauaji hayo alifika anakimbia anaïba piki piki ya muhanga ambae alikua amemaliza kumuua pia amekutwa na kosa la kutokuheshimu amri za viongozi kwa kutoka katika eneo lakazi bila izini ya viongozi wake.

Mahak**a imeamua kua askari huyo anapashwa kutoa fidia kwa familiale ya marehemu kiwango cha dolla 25.000$ US, pia atapashwa kulipa dola 5.000 kwa mwenye piki piki k**a fidia.

12/08/2023

DRC - BARAKA/ FIZI:
Vijana wa Baraka watakiwa kujiepusha na hotba za uchochezi wa chuki za ubaguzi wa kikabila. Hayo ni kwa mujiba wa kiongozi wa Baraza la vijana wa mjini Baraka ABAHENYA Patient Rafiki katika maadhimisho ya siku kuu ya Vijana ulimwenguni akiwa katika ukumbi wa Meladen Club mjini Baraka siku ya jumamosi tare 12 Agoust 2023.

Baraka: BARAZA LA VIJANA WABARAKA WASHEHEREKEA SIKUKUU YA KIMATAÏFA YA VIJANA ULIMWENGUNI./ By Madiba Mahoye."""""""""""...
12/08/2023

Baraka: BARAZA LA VIJANA WABARAKA WASHEHEREKEA SIKUKUU YA KIMATAÏFA YA VIJANA ULIMWENGUNI./ By Madiba Mahoye.
"""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""
Kilaïfikapo tare 12 August ya kilamwaka vijana ulumwenguni husheherekea siku kuu ya kimataïfa ilioteuliwa na Umoja wa Mataïfa kwa ajili yao.

Mantiki ya kuteuliwa siku hii, ni kuwapa fursa vijana kutazamia kwa pamoja changa moto zinazo wakabili vijana ikiwemo ukosefu wa ajira na madawa ya kulevya ambayo yamekithiri ulimwenguni.

Baraza la vijana wa mji na manispa ya Baraka, wamesheherekea siku hii k**a wengine katika ukumbi wa MELADEN CLUB chini ya kauli mbiu isemayo " Vijana tuepukane na hotba za uchochezi wa kikabila zinazo tolewa na wanasiasa wanaogombea uraïsi, viti bungeni ngazi za madiwani katika kipindi hiki kinacho elekea kampeni za uchaguzi mkuu". Ameyasema hayo katika hutba ya ufunguzi wa sherehe hizo kiongozi wa baraza la vijana wa mji wa Baraka bwana Abahenya Patient Rafiki.

Baada ya hotba hiyo ya ufunguzi, imefatiwa na mjadala ulio tolewa na mualikwa katika hafla hiyo bwana YAMONEA Orphée Kamengele, kiongozi wa shirika la vijana linalo jihusisha na maendeleo la " Kumekucha Tujenge Kwetu" KTK kwa kifupi.

Orphée amejaribu kufafanua maana ya chuki zinazo weza kusababisha mazara ya mgawanyiko katika jamii na kukemea vikali batabia hizo huku akibaïni kua chuki za misingi ya kikabila ni adui wa maendeleo kwa taïfa la kesho.

Baada ya muhadhara huo, vijana waliohudhuria katika sherehe hizo kutoka vikundi na mashirika mbali mbali vya maendeleo vyenye makao mjini Baraka na Tarafani Fizi wamejikubalisha kua hawato wapa nafasi wanasiasa watakao kuja na hotba za uchochezi wa ubaguzi wa makabila.

Kwa upandeo vijana kutoka shirika la "Vision Jeunes pour Agir" kwa kifupi V.J.A, linaloongozwa na bwana Théophile BASOSHI IUBE, wameliomba baraza la vijana wa Baraka kuendeleza mihadhara k**a hiyo kwenye kumbi mbali mbali na kwenye vyombo vya habari " Radios " na kadhalika ili mafunzo hayo ya wafike hata raïa wa tarafa la Fizi kwa ujumla.

Sherehe hizo zimeshindikizwa na michezo ya kuigiza ilio chezwa na vijana wasani waïgizaji na wanamuziki wa mjini Baraka ambapo watoa nasaha kupitia michezo na nyimbo kwa kupinga aïna yoyote ya ubaguzi wa kikabila.

DRC/ Bukavu:  JENGO LA SHULE LAPOROMOKA NA KUWAUA WATU 10./ By Mahoye Madiba."""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""...
11/08/2023

DRC/ Bukavu: JENGO LA SHULE LAPOROMOKA NA KUWAUA WATU 10./ By Mahoye Madiba.
"""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""

Takriban watu kumi waliuawa Alhamisi Agosti 10 huko Bukavu, kufuatia kuporomoka kwa jengo lililokuwa na shule ya kibinafsi. Kulingana na mashahidi, mkasa huo ulitokea saa sita mchana katika wilaya ya Bagira.

lakini kwa kweli tuko katika shida kubwa. Nimekosa kreni, kwa sababu, niliambiwa kuna watu ambao wamekwama chini ya lango ambalo lina uzito mkubwa, na kwamba hakuna mtu anayeweza kuliinua isipokuwa kreni, "alisema Meya wa Bagira, Patience Bengehya Wangwabo Alhamisi jioni kulingana na Radio Okapi.

Amesema kutofuata viwango vya ujenzi ndio chanzo cha janga hili:

"Kwa kweli, chanzo cha mkasa huu ni ujenzi usio sahihi. Walikuwa katika ujenzi, hivyo jengo likaporomoka. Afisa mmoja wa ngazi ya juu katika wilaya hiyo na watu wengine wengi walikuwa ndani jengo hili. Tayari tumeshatoa miili minne, pia kuna majeruhi ambao wamepelekwa hospitalini. Zoezi la kutafuta miili na watu ambao inawezka bado wako hai linaendelea, lakini kwa mikono ni kazi ngumu, tunahitaji kreni".

DRC/ CICR: WATU 600.000 WARIPOTIWA KUYAHAMA MAKAZI YAO KWA KIPINDI CHA MYEZI SITA./ by Mahoye Madiba."""""""""""""""""""...
11/08/2023

DRC/ CICR: WATU 600.000 WARIPOTIWA KUYAHAMA MAKAZI YAO KWA KIPINDI CHA MYEZI SITA./ by Mahoye Madiba.
""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""'"""""""""""""""""""""""""""""""""""""""

Ripoti mpya ya Kamati ya Kimataifa ya Msalaba Mwekundu (ICRC) imeonyesha kuwa watu takribani laki sita wamelazimika kukimbia makaazi yao kufuatia mapigano kati ya makundi ya wapiganaji wenye silaha, na jeshi la serikali mkoani Kivu Kaskazini, mashariki mwa DRC kwa muda wa miezi sita pekee.

Wafanyakazi wa misaada wa ICRC wa Kongo wanasaidia watu waliohamishwa makazi yao ambao wanakaribia kupokea msaada wa chakula, huko Kibati, Novemba 5, 2008.
Wafanyakazi wa misaada wa ICRC wa Kongo wanasaidia watu waliohamishwa makazi yao ambao wanakaribia kupokea msaada wa chakula, huko Kibati, Novemba 5, 2008.

Katika taarifa yake kwa Vyombo vya habari iliyochapishwa Agosti 10, Kamati hiyo ya ICRC, imesema asilimia 18 ya watu walioyahama makazi yao wanaishi katika viunga vya mji wa Goma katika makanisana shule.

ICRC imeendelea kusema kuwa asilimia 82 wanaishi katika familia zilizowapokea, na kwamba wengi wao hawana msaada wowote.

Kamati hiyo ya Msalaba mwekundu pia imesema kuongezeka kwa ukosefu wa usalama kunatatiza utoaji wa misaada katika maeneo yaliyoathiriwa zaidi na vurugu, na kwamba kwa muda wa miezi sita pekee watu k**a laki sita kukimbia makwao, ni idadi kubwa zaidi kuwahi kushuhudiwa katika Ulimwengu.

Mbali na Goma, ripoti hiyo imeonyesha kuwa wakazi wachache waliobaki kwenye mji wa Oicha, wenye wakazi laki tatu na sitini kaskazini mwa jiji la Beni, wanakabiliwa na ukosefu wa usalama.

Wakaazi hao wamekuwa wakikabiliwa na mashambulio yanayohusishwa na ADF ambao wamekuwa wakisakwa na majeshi ya FARDC ambayo yanashirikiana na jeshi la Uganda UPDF, hali ambayo pia imesababisha baadhi ya raia kukimbia nyumba zao na kuelekea mjini Beni.

Anne-Sylvie Linder, mkuu wa wajumbe wa ICRC mjini Goma, amewataka wafadhili kuendelea kusaidia makundi mbalimbali ya kibinadamu ambayo yanafanya kazi katika eneo hilo, katika kuhakikisha misaada ya kibinadamu inawafikia wanaohitaji licha ya kwamba mashirika ya kibinadamu yanakabiliwa na ukosefu wa ufadhili na vikwazo vya kufikia jamii zinazohitaji msaada.

DRC: MOTO WATEKETEZA ZAÏDI YA NYUMBA 50 MJINI BUKAVU USIKU WA SIKU YA JUMATANO KUAMKIA ALHAMISI. / by Mahoye Madiba.""""...
10/08/2023

DRC: MOTO WATEKETEZA ZAÏDI YA NYUMBA 50 MJINI BUKAVU USIKU WA SIKU YA JUMATANO KUAMKIA ALHAMISI. / by Mahoye Madiba.
"""""""""""""''""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""

Zaidi ya hamsini na maduka zaidi ya kumi yameteketea moto usiku wa kuamkia Alhamisi katika maeneo ya Panzi na Mudaka kwenye viunga vya mji wa Bukavu katika jimboni Kivu Kusini.

Mashuhuda wanasema moto mkali umewaka Jumatano jioni na kuteketeza baadhi ya nyumba zilizojengwa kwa mbao katika eneo la Panzi/Mulungulungu, bila kufafanua zaidi chanzo cha moto huo.

Moto mwingine umeteketeza maduka kadhaa kwenye soko la Mudaka, likiwa soko la pili kiuchumi katika wilaya ya Kabare linalopatikana kwenye umbali wa kilomita 20 kaskazini mwa mji wa Bukavu ambapo pia raia wa Bukavu hununua bidhaa mbalimbali.

Katika taarifa ya hivi karibuni, huduma ya ukingo wa raia Kivu kusini imehakikisha kwamba tangu Aprili mwaka huu tayari watu 18 wamepoteza maisha, watu wawili wamejeruhiwa na zaidi ya nyumba elfu moja kuteketea katika mfululizo wa ajali za moto zinazokadiriwa kuwa zaidi ya 20 mjini Bukavu.

Alipotangaza takwimu hizo, Aimé Lubago ambaye ni kiongozi wa huduma hiyo kwenye ofisi ya meya wa Bukavu, amesema familia zaidi ya elfu mbili zimebaki bila makazi zikiwa pia na matatizo makubwa ya kiuchumi.

Kiongozi huyo amenyoshea kidole ujenzi wa kiholela, kamba za moto wa umeme zilizotelekezwa kiholela na haswa zaidi mafuta ya gari yanayohifadhiwa na wauzaji wadogowadogo katika baadhi ya nyumba za Bukavu.

Huduma ya zimamoto imeonya wakaazi wa Bukavu kuwa waangalifu, ikihakikisha kwamba mji huo una magari matatu pekee ya zimamoto ambayo hadi sasa, yana matatizo ya kiufundi ambayo yanatafutiwa suluhisho.

Hivi karibuni Spika wa baraza la seneti nchini Congo Modeste Bahati Lukwebo amenunua magari tano ya zimamoto na kuyakabidhi viongozi wa mitaa ya Bukavu, ila wadadisi wa mambo wanahisi kwamba hadi sasa magari hayo hayajatumika k**a ilivyotarajiwa, kukiwa pia na tatizo la ujenzi kiholela unaozuia magari ya zimamoto kufika ya ajali ya moto.

Aliyekuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Augustin Matata Ponyo, ametangaza kuwa atawania urais, wakati...
04/08/2023

Aliyekuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Augustin Matata Ponyo, ametangaza kuwa atawania urais, wakati wa uchaguzi mkuu uliopangwa kufanyika Desemba 20.

Matata Mponyo, anaugana na wanasiasa wengine k**a Moise Katumbi, ambaye pia ameonesha nia ya kuwania urais kupambana na rais Felix Tshisekedi.

Ametoa tangazo hilo akiwa mjini Kindu, alipokutana na wafuasi wake na kueleza ni kwa nini anataka kuongoza nchi hiyo.

“Tuna mpango kabambe wa kurekebisha serikali na kuifanya kuwa ya kisasa ilikuifanya iwe na ufanisi wa kuishindani na lazima tujenge jeshi bora na jeshi la polisi lenye ufanisi na kuwa na ujerani mwema.” alisema Matata Ponyo

Kuhusu mpango wake anaosema ni wa kuifanya nchi ya DRC kutimiza ndoto zake Matata Ponyo anaamini anasema anaamini Kongo imara ambayo kila raia ana uhuru na nyenzo za kufanya kazi kwa mafanikio yake na taifa.

Aidha mwanasiasa huyo anasema maono yake ni kuitoa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kutoka katika kundi la nchi maskini zaidi duniani ndani ya miaka 5, na kuipandisha kwenye daraja la nchi zenye uchumi wa kati.

Haya yanajiri wakati huu tume ya Umoja wa Mataifa nchini humo MONUSCO ikisema itachunguza kifo cha mwanasiasa wa upinzani Cherubin Okende, aliyepatikana ameuawa jijini Kinshasa, Julai 13.

Jenerali Mody Berethe anayehusika na masuala ya kipolisi , ameteuliwa kuongoza uchunguzi huo.

“Polisi na wataalam wanaofuatilia shughuli hiyo, watafanya kazi chini ya mamlaka ya vyombo vya sheria, timu ya wachunguzi wetu itajiunga na wataalam wengine ambao wako tayari.” alisema Jenerali Mody Bereth.

Aidha Mody ameeleza kuwa upande wa DRC kuna timu tatu na mchango wao k**a MONUSCO utakuwa wa kiufundi kulingana na maarifa walio nayo k**a polisi stadi wenye taaluma ya kisayansi.

UGANDA: WATU 20 WAFARIKI KATIKA AJALI YA BOTI./ By Madiba Mahoye""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""...
04/08/2023

UGANDA: WATU 20 WAFARIKI KATIKA AJALI YA BOTI./ By Madiba Mahoye
""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""

Watu 20 wamethibitishwa kufariki baada ya boti waliyokuwa wakisafiria kuzama maji kwenye Ziwa Victoria nchini Uganda, ajali iliyotokea maajira ya saa tano asubuhi ya leo.

Boti hiyo ilikuwa na watu 34 na ilikuwa ikitokea kisiwa cha Bukasa kuelekea Entebbe, ambapo polisi wanasema watu 9 wameokolewa, huku chanzo cha ajali hiyo kimethibitishwa kuwa ni upakiaji kupita kiasi na hali mbaya ya hewa

Kwa mujibu wa maofisa wa polisi nchini humo, boti hiyo ambayo ilikuwa imejaa kupita kiasi, ilikuwa pia imebeba magunia ya makaa, chakula na bidhaa nyengine.

DRC/ Diplomasia:  MONUSCO YATAKIWA KUBAKI NCHINI DRC, HATABAADA YA 2024./ By Madiba Mahoye.""""""""""""""""""""""""'""""...
21/07/2023

DRC/ Diplomasia: MONUSCO YATAKIWA KUBAKI NCHINI DRC, HATABAADA YA 2024./ By Madiba Mahoye.
""""""""""""""""""""""""'""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""

Akiwa katika ziara ya kazi eneo la mashariki mwa ijumaa hii tare 21 Julay 2023 muakilishi wa katibu mkuu wa Umoja wa Mataïfa nchini Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, BINTOU KEITA akiambatana na mkuu wa ofisi ya MONUSCO Uvira wakishindikizwa na k**anda wa brigade ya 12 kwenye kanda ya operesheni ya Minembwe Jemedari EHENZO André Uketi , wamewasili Mikenge kijiji kinachopatikana ndani ya sekta ya Itombwe tarafa la Mwenga , jimbo la Kivu ya Kusini mashariki mwa DRC.

Ziara hiyo imegubikwa na malengo ya kukutana na raïa wanao eshi eneo hilo ambalo limekumbwa na mizozo ya kikabila kwa malengo ya kutazamia kwa pamoja kipindi hiki cha myazi 18 ambacho MONUSCO imepewa na serikali ilifunge virago na kuondoka nchini Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

Raïa waeneo hilo kwa upande wao wameiomba MONUSCO kubaki nchini mpaka pale amani na usalama vitakuwa vimerejea nchini, hasa katika eneo la mashariki ambalo limekumbwa na usalama mdogo takriban miongo mitatu na serikali haïjawa tayari kudhibiti hali ya mambo.

Maafisaa hao pia wamezungumza na raïa waliokimbia vijiji na majumba yao kwa malengo ya kutaka kujua hali za usalama wao na kiutu.

Fizi/ Siasa:  TCHETCHE ZA KUWANIA UBUNGE ZA ANZA KUONEKANA TARAFANI FIZI. / By Madiba Mahoye."""""""""""""""""""""""""""...
21/07/2023

Fizi/ Siasa: TCHETCHE ZA KUWANIA UBUNGE ZA ANZA KUONEKANA TARAFANI FIZI. / By Madiba Mahoye.
"""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""

Kukiwa kumebaki myezi kadhaa ili uchaguzi mkuu ufanyi nchini Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, vijana wengi wamejikita kwenye uwanja wa siasa.

Leo tunamzungumzia kijana MISANGA Benjamin. Wafwasi wake hupendelea kumwita "mtu wa vitendo, maendeleo kwa jamii". Benjamin amewasili katika kijiji cha Alùsilù na Alemi Nambala ndani ya Sekta ya Lúlenge tarafani Fizi.

Kuwasili kwake kijijini hapo amepokelewa kwa shangwe na nderemo huku ngoma na nyimbo zikitumbwizwa.

MISANGA Benjamin, ni miongoni mwa wagombea wanaogombea ubunge tarafani Fizi wakiwa nyuma ya m'bunge AMBATOBE Nyongolo Amy chini ya pendera ya > ya raïs Félix Antoine TSHISEKEDI TSHILOMBO.

Muhula huu vijana wa tarafa la Fizi wamepania kuwachagua vijana wenzao ili walete maendeleo tarani humu.

# Like na ukomenti #

Kigali: RWANDA YATOA ONYO KWA DRC KUTOJARIBU KUSHAMBULIA ARDHI YAKE./ by Madiba Mahoye."""""""""""""""""""""""""""""""""...
20/07/2023

Kigali: RWANDA YATOA ONYO KWA DRC KUTOJARIBU KUSHAMBULIA ARDHI YAKE./ by Madiba Mahoye.
"""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""""

Siku moja baada ya jeshi la DRC, kudai kuwa limepata taarifa za kiintelijensia kuonesha kuwa Rwanda inapanga kutuma wanajeshi wake jimbon Kivu Kaskazini, utawala wa Kigali, umekanusha madai hayo, huku nao ukiionya Congo dhidi ya jaribio lolote la kufanya mashambulio kwenye ardhi yake.

Jeshi la DRC limesema lina taarifa kwamba Rwanda inapanga kutuma wanajeshi wake jimbon Kivu Kaskazini
Jeshi la DRC limesema lina taarifa kwamba Rwanda inapanga kutuma wanajeshi wake jimbon Kivu Kaskazini.
Kwa mujibu wa jeshi la Congo, lengo la majeshi ya Rwanda ni kuongeza uwepo wao katika ardhi ya mashariki mwa nchi hiyo, likiituhumu Rwanda kushirikiana na waasi wa M23 kutekeleza vitendo vya kihalifu ikiwemo mauaji.

Hata hivyo jeshi la Rwanda limekanusha madai ya DRC, likiionya nchi hiyo kutojaribu kufanya shambulio kwenye ardhi yake, Kigali ikisema utawala wa Kinshasa unatafuta sababu ya kuendeleza mzozo uliopo.

Wakati huu ripoti za wataaalamu wa UN zikithibitisha Rwanda kuwasaidia waasi wa M23, Kigali inaituhumi Serikali ya Congo kwa uchokozi na hata kuanzisha vita dhidi yake.

Uhusiano kati ya Kinshasa na Kigali umetatizika kwa zaidi yam waka mmoja, DRC ikiituhumu Rwanda kushirikiana na waasi wa M23 huku Rwanda ikiituhumu Kinshasa kushirikiana na waasi wa FDLR

Adresse

Bukavu

Téléphone

+243975571265

Notifications

Soyez le premier à savoir et laissez-nous vous envoyer un courriel lorsque Imara média publie des nouvelles et des promotions. Votre adresse e-mail ne sera pas utilisée à d'autres fins, et vous pouvez vous désabonner à tout moment.

Vidéos

Partager